ASKOFU SHOO,MUNGA NA MALASUSA WATOA NENO JUU YA COVID19

MKUU wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Askofu Dk. Fredrick Shoo pamoja na Maaskofu Dk. Alex Malasusa na Stephen Munga
wametoa maagizo kwa washarika katika kuukabili ugonjwa wa COVID-19 unaosababishwa na virusi vya corona.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti kwenye Dayosisi wanazoziongoza Maaskofu hao pia wameagiza Wakristo kuoba kwa bidii juu ya ugonjwa huo.

Mkuu wa Kanisa ambaye pia ni Askofu wa Dayosisi ya Kaskazini, aliesme kuwa pamoja na yote yanayoendela kamwe Kanisa hilo halitaacha kumuabudu Mungu.

“Naomba ifahamike kuwa, pamoja na yote endapo ugonjwa huu utaendelea japo siyo ombi letu, tupo tayari kufanya mabadiliko ya taratibu zetu za Ibada lakini hatutuacha kumwabudu Mungu,” alisema Askofu Dk. Shoo.

Akihubiri kwenye Ibada ya kumuingiza kazini Mkuu mpya wa jimbo la Hai, Mch. Biniel Mallyo Askofu Dk. Shoo alisema kuwa huu ni wakati wa kumkaribia Mungu, kwa kuwa inaonekana kwa nguvu na akili za kibinadamu, hatuwezi zaidi ya kimkimbilia yeye.

“Niwasihi kila mmoja wetu kuacha hofu na tung’ang’ane kwa kufanya maombi ya toba kwa Mungu wetu,” alisema Askofu Dk. Shoo.

Mkuu huyo wa Kanisa aliwapa matumaini Watanzania, akieleza kuwa ugonjwa huo utapita maana Mungu amesema atatulinda dhidi ya mauti na magonjwa.

Aliwasihi Wakristo kuwaombea watumishi wa sekta ya afya ili wasiathirike pindi wanapotoa huduma kwa wale waliothibitika kuugua ugonjwa huo.

Aidha Askofu Shoo alisema Kanisa hilo litafanya maombi maalum yanayofanana ili kumsihi Mungu aliepushe Taifa na ongezeko la virusi vya corona na katika Ibada hiyo makundi mbalimbali yalifanya maombi maalumu ya kuomba toba kwa Mungu.

MUNGA ATAKA MAOMBI YA KUFUNGA

Askofu wa Dayosisi ya Kaskazini Mashariki (DKMs), Dk. Stephen Munga ameandika waraka maalumu ambao umesambazwa kwenye Sharika zote za Dayosisi hiyo, juu ya hatua za kuchukua kuhusiana na ugonjwa huo unaotajwa na Shirika la Afya Duniani (WHO), kuwa ni janga la dunia.

“Ninaandika waka huu kwenu nikijua kwamba ulimwengu kwa ujumla na Taifa letu linapita katika kipindi kigumu cha mapambano dhidi ya gonjwa la COVID 19,” alisema Askofu Dk. Munga kupitia waraka huo.

Kupitia waraka huo, Askofu Dk. Munga alinukuu maneno ya Mungu kutoka kitabu cha Yeremia 17: 14 unaosema; “Uniponye ee Bwana nami nitaponyeka, uniokoe nami nitaokoka kwa maana wewe ndiwe uliye sifa zangu.”

Aidha Mkuu huyo wa DKMs alionya juu ya watu wanaopuuza ugonjwa huo na kuwatahadharisha kuwa makini na manabii wa uongo wanaotaka waone kuwa ugonjwa huo siyo kitu. “Ieleweke kwamba tunashughulika na janga.”

Alitoa wito wa maombi kwa wanakanisa na kutubu katika kipindi hichi cha kwaresma.

“Nawaalika wana DKMs kuungana na watakatifu wengine hapa Tanzania na duniani katika kuomba na kufunga,” ulisema waraka wa Askofu na kuongeza;

“ Tena kwa sababu tumo katika kipindi cha Kwaresima hembu tukumbushwe kuingia ndani zaidi katika roho ya toba.

Tumuombe Mungu msamaha wa dhambi zetu, msamaha wa dhambi za Taifa letu na dhambi ya ukengeufu wa ulimwengu wa kumuacha Mungu na kujivunia maarifa na nguvu za wanadamu,” iliongeza sehemu ya waraka huo wa Askofu Dk. Munga.

Askofu Munga alisema kuwa maombi hayo yafanyike katika siku zote zilizobaki za majira ya Kwaresma ba kuhitimishwa katika siku ya pili ya Pasaka.

MALAUSA: TOMBE KWA ROHO, TUOMBE KWA AKILI

Naye Askofu Dk. Malasusa wa Dayosisi ya Mashariki na Pwani aliwaambia washarika wa Dayosisi hiyo kuwa ni lazima wajitunze kwa kuzingatia wataalamu wa afya wanavyosema.

“Tusisubiri viongozi wa serikali ndiyo watuambie namna ya kutunza hekalu la Bwana, sisi ni lazima tutunze usafi wetu, kwa hiyo tunapoambiwa kunawa, tusisalimiane hayo ni mambo ambayo sisi tunatakiwa tuwe mstari wa mbele na kuwa mabalozi wa kuyafanya hayo.

“Tunaposema kuwa tunapunguza makusanyiko ya katikati ya wiki siyo kwamba hatutaki Ibada, lakini kwa sababu ya hali halisi ilivyo imebidi tusimame kidogo si kwamba hatuzipendi na si kwamba hatutaki kumuabudu Mungu lakini tuombe kwa roho na tuombe kwa akili,” alisema Askofu Dk. Malasusa.

Mkuu wa DMP alisema ni wakati wa kuomba kwa roho na akili na pale hali itakapokuwa njema watu wataendelea kukutana.

RAIS WA WALUTHERI ATOA NENO

Corona ambayo imetikisa dunia pia imefanya Fungamano la Makanisa ya Kilutheri Duniani (FMKD-LWF) nalo kuandika barua maalumu kwa makanisa yake wanachama duniani kote kusisitiza jambo hilo la maombi.

Katika barua hiyo iliyosainiwa na Rais wa Fungamano hilo Askofu Mkuu Dk. Filibus Musa na Katibu Mkuu Dk. Martin Junge FMKD imewataka wanachama wake kusimamia mstari wa kitabu cha 2Tim 1:2 unaosema Maana Mungu hakutupa roho ya woga, bali ya nguvu na ya upendo na moyo wa kiasi.

“Huu ni wakati wa kuendelea kuamini uwepo wa huruma za Mungu katika maisha ya mwanadamu. Tunao ujasiri tukijua kuwa Mungu hatuachi kamwe, hata kama itamaanisha kupitia mateso ya msalaba.

“Tunauona msalaba wa Yesu Kristo kama alama ya nguvu na tumaini letu. Tunaalika makanisa wanachama kuombeana hasa kwa nchi na makanisa ambayo yako katika kiini cha mlipuko wa virusi hivyo,” ilisema barua hiyo.

FMKD imeorodhesha maombi 12 ambayo wanachama wake watayaomba juu ya ugonjwa huo.

Mojawapo ya maombi hayo yalisema; “Uwe msaada wetu hasa wakati huu ambapo virusi vya corona vinazidi kusambaa ulimwenguni, uponye wagonjwa, uzisaidie na kuzilinda familia zao na marafiki ili wasiathirike. Ee Mungu, sikia kilio chetu.”

Makanisa na watumishi mbalimbali wa Mungu wanaendela kutoa wito wa kuomba juu ya ugonjwa huo ambao kwa hapa nchini tayari umesababisha kifo cha mtu mmoja huku wagonjwa wakiwa 20 ambao 17 kati yao, kwa mujibu wa Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Ummy Mwalimu wanaendele vizuri wawili wakiwa wamepona.

COVID-19 ilianzia nchini China Desemaba mwaka jana na hadi sasa imeenea dunia nzima.

MJUE ADUI YAKO.

Watu wengi tuna hasira, uchungu, ghadhabu, maumivu, mapambano, chuki na kisasi na mashindano mengi moyoni, tukiamini kabisa kuna watu waliotusababishia hali hiyo, watu tunawaona wabaya, maadui, tunawaita wakarofi na majina mengi tuwezavyo kuwaita. Wanaweza kuwa watu wa mbali ama wa karibu, aweza kuwa mke au mume, mchumba au rafiki, jirani, mfanyakazi mwenzako, ama yeyote yule unayehisi kakukosea.
Lakini leo nataka nikuambie adui yako mkubwa wala si huyo unayemdhani, huyo ni msaidizi tu wa adui yako, adui yako yuko ndani yako mwenyewe, anayekuumiza, anayekutukana, anayekuadhibu, anayekunyanyasa yuko ndani yako na kwa kuwa umeshindwa kummudu ndio maana hasira zako na lawama zako umezihamishia kwa msaidizi wa adui yako ambaye ndio yule unayemdhania.

Umewahi jiuliza? Kabla hujachukia ndani yako lazima kuna sauti mbili zilishindana, moja ikakuambia usichukie nyingine ikakuambia haiwezekani utaonekana mjinga, ile sauti iliyoshinda ya ubaya ndiyo adui yako mkubwa, maana kinyume cha hapo wala usingefanya maamuzi hayo. Umemuadhibu bure mtu wa mbali lakini ulipaswa kumwadibisha mtu wako wa ndani kwa wema na hapo ungeweza kujisamehe kabla hujaadhibu unayedhani kakukosea.

Adui wa ndani ni mbaya kuliko wa nje, maana kama nje kukiharibika utakimbilia ndani kupata usalama, ila ndani kukiharibika jua huna pa kukimbilia, na huyo adui akikushinda kabisa atakuua au kukusababishia madhara mengi kiakili na kiafya, NDIO MAANA USISHANGAE MTU KAJIUA AU KAJIDHURU JUA KASHINDWA VIBAYA NA ADUI YAKE WA KARIBU AMBAYE NI YEYE MWENYEWE.

Biblia haijakosea inaposea LINDA SANA MOYO WAKO, KULIKO YOTE UYALINDAYO, MAANA HUKO NDIKO ZITOKAKO CHEMICHEMI ZA UZIMA. najua mpaka sasa adui wa ndani bado anakushawishi uupuuze ujumbe huu, ni lazima umshinde kama kweli unataka amani ya ndoa yako, kazi yako, jirani yako, ndugu zako nk. Ukimshinda adui wa ndani hakuna adui nje kamwe ila ukishindwa na adui wa ndani basi kila atakayekugusa iwe bahati mbaya au makusudi basi atakuwa adui yako.

Mungu akupe kuelewa haya

KIPIMO CHA IMANI

Tangu nimeokoka nimebahatika kusikia mafundisho mengi sana mazuri kuhusu imani, wakati mwingine nilijifunza kuwa huhitaji imani kubwa kung’oa mlima, na nilipoijaribu imani ndogo kung’oa mlima, mlima uliishinda imani yangu ndogo. Je! Wapi hasa nilikosea mpaka kushindwa kuung’oa mlima mkubwa kwa imani ndogo? ( nadhani nilihitaji imani inayokua kama mbegu ya haladali, mpaka kuzidi ukubwa wa mlima ndipo niung’oe)

Leo ninataka kukueleza kipimo cha imani yako kwa maelezo haya.

Kama imani yako ya kufa ni kubwa kuliko ya kuishi basi jua huna imani au imani yako ni haba, hivyo kikubwa lazima kishinde kidogo.

Kama imani yako ya kutokupona ina nguvu kuliko kupona basi huna imani, au imani yako haba na chenye nguvu kitashinda.

Kama imani yako ya kukosa ni hakika kuliko ya kupata basi imani yako ni ndogo hivyo kukosa kutashinda, na kama imani yako ya laana ni zaidi ya baraka nakuhakikishia kila utakapoongea, utakachowaza, utakachoota, utakacokiona na kukikiri kitakuwa ni laana, balaa, mikosi na chenye nguvu kwenye akili yako, moyo wako na kinywa chako ndicho kitakachoshinda na kutokea kwenye maisha yako.

Nadhani umeshajipima kwenye eneo lako, sasa ni kazi yako kuhakikisha unaifanya imani yako iwe kubwa kuliko, mlima, magonjwa, madeni, na mahusiano ndipo utakapoweza kubadilisha mwonekano wa kinachokutisha kwa imani. KUMBUKA CHENYE NGUVU, UZITO, NA UHAKIKA NDICHO HUSHINDA.
Wakati wewe unaona haiwezekani kuna watu imewezekana, tofauti yako na yao ni kile unachokiona kigumu wao walikiona chepesi. Iga mwenendo wao utafanikiwa
@official_evjohn
#victoriousyear2020

WAJIBU WAKO

UNAWAJIBIKA NA MAISHA YAKO MWENYEWE. “Maana kila mtu atalichukua furushi lake mwenyewe.” (Wagalatia 6:5) “Basi ni hivyo, kila mtu miongoni mwetu atatoa habari/hesabu zake mwenyewe mbele za Mungu.” (Warumi 14:12) “Roho itendayo dhambi, ndiyo itakayokufa; mwana hatauchukua uovu wa baba yake, wala baba hatauchukua uovu wa mwanawe, haki yake mwenye haki itakuwa juu yake, na uovu wake mwenye uovu utakuwa juu yake.”
(Ezekieli 18:20)

Kwa msisitizo wa kipekee kabisa maandiko haya yanatuonesha kwamba kila mtu anawajibika na maisha yake mwenyewe. Hata mbele za Mungu hakuna atakaye hukumiwa kwa dhambi za mtu mwingine. Kwa maana hiyo hiyo basi hakuna anayewajibika na maisha ya mtu mwingine. Kwa mujibu wa maandiko haya ni makosa makubwa kuwa na MAWAZO TEGEMEZI, AKILI TEGEMEZI. Ile dhana ya KULAUMU WATU KWA SABABU HAWAJAKUSAIDIA inakemewa vikali na maandiko haya.
Simama upiganie maisha yako mwenyewe sio lazima watu wakusaidie hata kama uwezo wanao. Jukumu la kwanza la Baba yako ni kwa mke wake. Wewe ukishafika Miaka 18 unapaswa kuwaza kesho yako itakuwaje. Jukumu kubwa la Kaka na Dada zako ni maisha yao na watoto wao. Wewe sio jukumu lao. Acha kulaumu watu na usimame kutengeneza maisha yako mwenyewe.

Kama unataka kufunga Ndoa fanya unachomudu, usijiwekee bajeti kubwa kwa kuangalia mifuko ya watu. Kama hauna fedha achana na kusherekea Birthday, kunywa maji mshukuru Mungu. Kama umekosa kodi kalale kanisani saidiana na mlinzi ukiumwa mbu utapata akili ya kutafuta hela. Lakini usiwe mzigo kwa mtu yeyote na kulaumu na kuchukia watu. “Oh hawanisadii chochote!” Nani alikwambia unapaswa kusaidiwa!? KASIRIKA, CHUKIA, NUNA LAKINI UJUMBE NDIO UMEUPATA, PIGANIA MAISHA YAKO. KAMA AMBAVYO UTAHUKUMIWA KWA DHAMBI ZAKO MWENYEWE BASI VIVYO HIVYO AMUA KUFANIKIWA KWA JASHO LAKO MWENYEWE. -evjohn whatsup 0767386606
#2020

SIJAVIZOEA

SIJAVIZOEA.: 1 Samweli 17:38 Ndipo Sauli akamvika Daudi mavazi yake ya vita, akamtia chapeo cha shaba kichwani, akamvika dirii. 1 Samweli 17:39 Naye Daudi akajifunga upanga juu ya mavazi yake, akajaribu kwenda; maana alikuwa hajavijaribu. Daudi akamwambia Sauli, SIWEZI KWENDA na VITU HIVI, MAANA SIKUVIJARIBU (SIJAWAHI KUVITUMIA/SIJAVIZOEA). BASI DAUDI AKAVIVUA. 1 Samweli 17:40 AKAICHUKUA FIMBO YAKE MIKONONI, AKAJICHAGULIA MAWE LAINI MATANO KATIKA KIJITO CHA MAJI, AKAYATIA KATIKA MFUKO WA KICHUNGAJI ALIOKUWA NAO, MAANA NI MKOBA WAKE, NA KOMBEO LAKE ALIKUWA NALO MKONONI MWAKE, AKAMKARIBIA YULE MFILISTI. Mara nyingi huwa tunasubiri Mungu atupe wazo jipya la biashara au namna mpya ya utendaji ili tuweze kufanikiwa na tunasumbuka sana kuiga mifumo ya watu wengine na kuacha kuboresha kile ambacho tunakijua na kufanya kwa ubora tunasubiri wazo jipya na namna mpya ili kufanikiwa na kujikuta tunajichelewesha. Nimegundua mara nyingi sana Mungu huwa anatumia kile tunachokijua na kukiboresha ndipo hapo anatufanya kuwa bora na tofauti. Anamuuliza Musa “BWANA akamwambia, Ni nini hiyo uliyo nayo mkononi mwako? Akasema, NI FIMBO. Akamwambia, Itupe chini; akaitupa chini, nayo ikawa nyoka; Musa akakimbia mbele yake.” (Kutoka 4:2-3) Kipawa hicho unachokidharau, huduma hiyo hiyo unayoichukulia kawaida, biashara hiyo hiyo ya kawaida, ujuzi na uwezo ulionao ndio Mungu huwa anatumia kukufanya kuwa Mkuu. Usitafute sana kubuni ndege nyingine wakati unaweza kuboresha hii iliyopo na ukatajirika. USIHANGAIKE KUFUNGUA CHAMPAGNE 🍾 NA VIDOLE WAKATI UMEZOEA KUFUNGUA SODA KWA MENO, TUMIA UJUZI WAKO, ANAYEKUONA MSHAMBA NI KWA SABABU ANA NAMNA YAKE YA KUFANYA. KUWA BORA KATIKA NAMNA YAKO. – Ev.john