SIJAVIZOEA

SIJAVIZOEA.: 1 Samweli 17:38 Ndipo Sauli akamvika Daudi mavazi yake ya vita, akamtia chapeo cha shaba kichwani, akamvika dirii. 1 Samweli 17:39 Naye Daudi akajifunga upanga juu ya mavazi yake, akajaribu kwenda; maana alikuwa hajavijaribu. Daudi akamwambia Sauli, SIWEZI KWENDA na VITU HIVI, MAANA SIKUVIJARIBU (SIJAWAHI KUVITUMIA/SIJAVIZOEA). BASI DAUDI AKAVIVUA. 1 Samweli 17:40 AKAICHUKUA FIMBO YAKE MIKONONI, AKAJICHAGULIA MAWE LAINI MATANO KATIKA KIJITO CHA MAJI, AKAYATIA KATIKA MFUKO WA KICHUNGAJI ALIOKUWA NAO, MAANA NI MKOBA WAKE, NA KOMBEO LAKE ALIKUWA NALO MKONONI MWAKE, AKAMKARIBIA YULE MFILISTI. Mara nyingi huwa tunasubiri Mungu atupe wazo jipya la biashara au namna mpya ya utendaji ili tuweze kufanikiwa na tunasumbuka sana kuiga mifumo ya watu wengine na kuacha kuboresha kile ambacho tunakijua na kufanya kwa ubora tunasubiri wazo jipya na namna mpya ili kufanikiwa na kujikuta tunajichelewesha. Nimegundua mara nyingi sana Mungu huwa anatumia kile tunachokijua na kukiboresha ndipo hapo anatufanya kuwa bora na tofauti. Anamuuliza Musa “BWANA akamwambia, Ni nini hiyo uliyo nayo mkononi mwako? Akasema, NI FIMBO. Akamwambia, Itupe chini; akaitupa chini, nayo ikawa nyoka; Musa akakimbia mbele yake.” (Kutoka 4:2-3) Kipawa hicho unachokidharau, huduma hiyo hiyo unayoichukulia kawaida, biashara hiyo hiyo ya kawaida, ujuzi na uwezo ulionao ndio Mungu huwa anatumia kukufanya kuwa Mkuu. Usitafute sana kubuni ndege nyingine wakati unaweza kuboresha hii iliyopo na ukatajirika. USIHANGAIKE KUFUNGUA CHAMPAGNE 🍾 NA VIDOLE WAKATI UMEZOEA KUFUNGUA SODA KWA MENO, TUMIA UJUZI WAKO, ANAYEKUONA MSHAMBA NI KWA SABABU ANA NAMNA YAKE YA KUFANYA. KUWA BORA KATIKA NAMNA YAKO. – Ev.john

TAFAKURI YA JUMATANO YA MAJIVU 26/04/2020

Kesho nisiku pekee ambayo kanisa linaingia majira mapya yanayoitwa Kwaresma nasisi kama KKKT doyosisi ya kusini tunatoa tafakari fupi ya JUMATANO YA MAJIVU Jumatano ya majivu ni siku ya kwanza kwenye kipindi kiitwacho kwaresma ambapo siku hii inatukumbusha wakristo ya kwamba sisi ni mavumbi na mavumbini tutarudi kadiri ya agizo la Mungu katika mwanzo3:19 …….” hata utakapoirudia ardhi, ambayo katika hiyo ulitwaliwa; kwa maana u mavumbi wewe, nawe mavumbini utarudi” Shabaha ya kuwekwa kwasiku hii nikutaka kuamsha akili za waumini ama washarika kutambua nafasi ya toba katika maisha haya mafupi Jumatano ya majivu kwamakanisa mengine kama oxthodox na katoliki huwapaka waumini wao majivu katika paji la uso wao ili kuwakumbusha inatupasa tuwe watu watoba lakini hiyo niishara ya nje ambayo hata mitume na manabiib waliitumia wakati wakifunga walivaa magunia nakujipaka majivu kuonyesha wanaomboleza ama unyenyekevu mbele za Mungu SHABAHA YA HII SIKU Kwet kama kanisa la kiinjili lakilutheri tumepewa mstari wakesho ambao ni Yoeli3:19a nakichwa ama wazo linasema KUTUBU NA KUREJEA KWA BWANA kwanza mkristo unatakiwa ujitathimini maisha yako je unaishi maisha yatoba ama unasubiri mpaka itokee kwenye kwaresma?? Kitu kingine mkristo anatakiwa ajifanyie hesabu ama tafakari fupi tokea kwarsma ya mwaka jana mapaka leo umesimama vizuri kwenye imani ambayo Yesu alituachia ama umekuwa mguu pande. KUTUBU NA KUREJEA KWA BWANA Ndugu zangu waamini …Bwana asifiwe tunapoanza majira haya ya toba siku 40 umejipangaje iliuwe kamili mbele za Mungu kumbuka yesu anatuambia “njoni kwangu nyinyi nyote msumbukao na kulemewa na mizigo ya dhambi nami nitawapumzisha” Mizigo mingapi inakulemea ndugu yangu kiasi kwamba hujapata mahali pakutua lakini yesu anatuambia utue kwake. Itaendelea kesho………@Evjohn