MJUE ADUI YAKO.

Watu wengi tuna hasira, uchungu, ghadhabu, maumivu, mapambano, chuki na kisasi na mashindano mengi moyoni, tukiamini kabisa kuna watu waliotusababishia hali hiyo, watu tunawaona wabaya, maadui, tunawaita wakarofi na majina mengi tuwezavyo kuwaita. Wanaweza kuwa watu wa mbali ama wa karibu, aweza kuwa mke au mume, mchumba au rafiki, jirani, mfanyakazi mwenzako, ama yeyote yule unayehisi kakukosea.
Lakini leo nataka nikuambie adui yako mkubwa wala si huyo unayemdhani, huyo ni msaidizi tu wa adui yako, adui yako yuko ndani yako mwenyewe, anayekuumiza, anayekutukana, anayekuadhibu, anayekunyanyasa yuko ndani yako na kwa kuwa umeshindwa kummudu ndio maana hasira zako na lawama zako umezihamishia kwa msaidizi wa adui yako ambaye ndio yule unayemdhania.

Umewahi jiuliza? Kabla hujachukia ndani yako lazima kuna sauti mbili zilishindana, moja ikakuambia usichukie nyingine ikakuambia haiwezekani utaonekana mjinga, ile sauti iliyoshinda ya ubaya ndiyo adui yako mkubwa, maana kinyume cha hapo wala usingefanya maamuzi hayo. Umemuadhibu bure mtu wa mbali lakini ulipaswa kumwadibisha mtu wako wa ndani kwa wema na hapo ungeweza kujisamehe kabla hujaadhibu unayedhani kakukosea.

Adui wa ndani ni mbaya kuliko wa nje, maana kama nje kukiharibika utakimbilia ndani kupata usalama, ila ndani kukiharibika jua huna pa kukimbilia, na huyo adui akikushinda kabisa atakuua au kukusababishia madhara mengi kiakili na kiafya, NDIO MAANA USISHANGAE MTU KAJIUA AU KAJIDHURU JUA KASHINDWA VIBAYA NA ADUI YAKE WA KARIBU AMBAYE NI YEYE MWENYEWE.

Biblia haijakosea inaposea LINDA SANA MOYO WAKO, KULIKO YOTE UYALINDAYO, MAANA HUKO NDIKO ZITOKAKO CHEMICHEMI ZA UZIMA. najua mpaka sasa adui wa ndani bado anakushawishi uupuuze ujumbe huu, ni lazima umshinde kama kweli unataka amani ya ndoa yako, kazi yako, jirani yako, ndugu zako nk. Ukimshinda adui wa ndani hakuna adui nje kamwe ila ukishindwa na adui wa ndani basi kila atakayekugusa iwe bahati mbaya au makusudi basi atakuwa adui yako.

Mungu akupe kuelewa haya

KIPIMO CHA IMANI

Tangu nimeokoka nimebahatika kusikia mafundisho mengi sana mazuri kuhusu imani, wakati mwingine nilijifunza kuwa huhitaji imani kubwa kung’oa mlima, na nilipoijaribu imani ndogo kung’oa mlima, mlima uliishinda imani yangu ndogo. Je! Wapi hasa nilikosea mpaka kushindwa kuung’oa mlima mkubwa kwa imani ndogo? ( nadhani nilihitaji imani inayokua kama mbegu ya haladali, mpaka kuzidi ukubwa wa mlima ndipo niung’oe)

Leo ninataka kukueleza kipimo cha imani yako kwa maelezo haya.

Kama imani yako ya kufa ni kubwa kuliko ya kuishi basi jua huna imani au imani yako ni haba, hivyo kikubwa lazima kishinde kidogo.

Kama imani yako ya kutokupona ina nguvu kuliko kupona basi huna imani, au imani yako haba na chenye nguvu kitashinda.

Kama imani yako ya kukosa ni hakika kuliko ya kupata basi imani yako ni ndogo hivyo kukosa kutashinda, na kama imani yako ya laana ni zaidi ya baraka nakuhakikishia kila utakapoongea, utakachowaza, utakachoota, utakacokiona na kukikiri kitakuwa ni laana, balaa, mikosi na chenye nguvu kwenye akili yako, moyo wako na kinywa chako ndicho kitakachoshinda na kutokea kwenye maisha yako.

Nadhani umeshajipima kwenye eneo lako, sasa ni kazi yako kuhakikisha unaifanya imani yako iwe kubwa kuliko, mlima, magonjwa, madeni, na mahusiano ndipo utakapoweza kubadilisha mwonekano wa kinachokutisha kwa imani. KUMBUKA CHENYE NGUVU, UZITO, NA UHAKIKA NDICHO HUSHINDA.
Wakati wewe unaona haiwezekani kuna watu imewezekana, tofauti yako na yao ni kile unachokiona kigumu wao walikiona chepesi. Iga mwenendo wao utafanikiwa
@official_evjohn
#victoriousyear2020

WAJIBU WAKO

UNAWAJIBIKA NA MAISHA YAKO MWENYEWE. “Maana kila mtu atalichukua furushi lake mwenyewe.” (Wagalatia 6:5) “Basi ni hivyo, kila mtu miongoni mwetu atatoa habari/hesabu zake mwenyewe mbele za Mungu.” (Warumi 14:12) “Roho itendayo dhambi, ndiyo itakayokufa; mwana hatauchukua uovu wa baba yake, wala baba hatauchukua uovu wa mwanawe, haki yake mwenye haki itakuwa juu yake, na uovu wake mwenye uovu utakuwa juu yake.”
(Ezekieli 18:20)

Kwa msisitizo wa kipekee kabisa maandiko haya yanatuonesha kwamba kila mtu anawajibika na maisha yake mwenyewe. Hata mbele za Mungu hakuna atakaye hukumiwa kwa dhambi za mtu mwingine. Kwa maana hiyo hiyo basi hakuna anayewajibika na maisha ya mtu mwingine. Kwa mujibu wa maandiko haya ni makosa makubwa kuwa na MAWAZO TEGEMEZI, AKILI TEGEMEZI. Ile dhana ya KULAUMU WATU KWA SABABU HAWAJAKUSAIDIA inakemewa vikali na maandiko haya.
Simama upiganie maisha yako mwenyewe sio lazima watu wakusaidie hata kama uwezo wanao. Jukumu la kwanza la Baba yako ni kwa mke wake. Wewe ukishafika Miaka 18 unapaswa kuwaza kesho yako itakuwaje. Jukumu kubwa la Kaka na Dada zako ni maisha yao na watoto wao. Wewe sio jukumu lao. Acha kulaumu watu na usimame kutengeneza maisha yako mwenyewe.

Kama unataka kufunga Ndoa fanya unachomudu, usijiwekee bajeti kubwa kwa kuangalia mifuko ya watu. Kama hauna fedha achana na kusherekea Birthday, kunywa maji mshukuru Mungu. Kama umekosa kodi kalale kanisani saidiana na mlinzi ukiumwa mbu utapata akili ya kutafuta hela. Lakini usiwe mzigo kwa mtu yeyote na kulaumu na kuchukia watu. “Oh hawanisadii chochote!” Nani alikwambia unapaswa kusaidiwa!? KASIRIKA, CHUKIA, NUNA LAKINI UJUMBE NDIO UMEUPATA, PIGANIA MAISHA YAKO. KAMA AMBAVYO UTAHUKUMIWA KWA DHAMBI ZAKO MWENYEWE BASI VIVYO HIVYO AMUA KUFANIKIWA KWA JASHO LAKO MWENYEWE. -evjohn whatsup 0767386606
#2020