MUHTASARI WA MAHUBIRI YA LEO TAREHE 26/07/2020

SOMO: Mwanzo 41:41-45

UTANGULIZI
Bwana Yesu asifiwe, leo tunaangalia juu ya “NEEMA YA MUNGU YATUWEZESHA” yote tunayofanikiwa kuyafanya hapa duniani pamoja na magumu yote tunayopitia neema ya Mungu peke yake ndio inayotuwezesha kuonekana tulivyo, hatuwezi kujivunia akili zetu wala nguvu zetu wenyewe ila wakati wote yote tuyafanyayo tujue kuwa ni Mungu ametuwezesha.
Waandishi na mafarisayo wao walikuwa ni watu wa kushika sheria sana na kujitahidi kwa nguvu zao kuonyesha kuwa wanafahamu juu ya usafi na uchafu wa mtu ila Yesu anapotokea kwao anataka kuwabadiisha namna ya kufiki na kutambua mapenzi ya Mungu na kuondokana na mapokeo ya wazee.
Kwa somo hili tunajifunza haya yafuatayo

1. ASILI YA KWELI YA UNAJISI.
• Wayahudi walikuwa na sheria mbalimbali juu ya vyakula wakionyesha vingine ni safi na vingine ni najisi na hata jinsi ya kujiandaa kula. Walipoona wanafunzi wa Yesu wanakula bila kunawa mikono waliwahesabu kuwa ni najisi.
• Yesu anawataka watu wake kuelewa kuwa unajisi wa kweli hauwezi kuasilishwa na nguvu za nje bali kwa nguvu za ndani.
• Kile unachokipokea na kukiingiza katika mwili wako ndio kinachosababisha nguvu ya kutoa kile kilichopo ndani yako hivyo tunapaswa kuwa makini zaidi.

2. UTAMADUNI/MAZOEA YANAWEZA KUKUFANYA USIMUELEWE YESU
• Wanafunziwakiwa ni miongoni mwa wayahudi kwa kusikia mafundisho ya Yesu juu ya UNAJISI kutokana na maelekezo na torati walizoishi nazo kwa muda mrefu (Walawi 11: 1 – 47, Mt 5:17 – 18) hawakuelewa fundisho la Yesu walifikiri kuwa amekosea na kutaka mafafanuzi zaidi.
• Yesu aliwashangaa kwa kuzingatia walichokizoea zaidi kuliko kuisikiliza sauti yake na kuelewa ukweli wa neno la Mungu kama ilivyo kwetu sasa watu wengi kutokana na mazoea ya maishahawasikilizi Mungu anawata kufanya nini.

3. MATOKEO MAZURI AU MABAYA YA MAISHA YA MTU YANATOKA MOYONI
• Moyo wa mwanadamu ndio unaoleta matokeo ya aina zote ya mwanadamu, yawe mazuri au mabaya. (mithali 4:23)
• Moyo ukiathiriwa na dhambi ndiko ambapo mabaya yote hutokea (Mhubiri 9:3, Yer 17:9) na huwa mwanzo wa maovu yote (Mk 7: 20 – 23)

HITIMISHO
Wote tunapaswa kuelekeza macho yetu na umakini wetu wote katika mioyo yetu na kuilinda isiingiliwe na dhambi na kusababisha sisi kuwa waasi mbele za Mungu. ( Efeso 4:17 – 24, 1Petro 4: 1-3,) Haya yote yanawezekana ikiwa tutakuwa watii kwa neno la Mungu wakati wote na kujifunza kwa Mungu ( Mdo 2:28, 22: 16)
Kwa akili zetu ni Ngumu ila neema ya Mungu iliyokuu sana Kwetu inatuwezesha kufanya yote.
AMEN

MUHTASARI WA MAHUBIRI YA LEO 19/07/2020

Somo:HURUMA YA MUNGU

MASOMO
zaburi1:1-69
2Wakoritho7:5-10
Mathayo9:1-8*
UTANGULIZI
▶Jumapili ya leo tunajifunza juu ya huruma ya Mungu kwa wanadamu
▶Katika tafakari hii ya huruma za Mungu tumepewa kutoka injili ya mathayo9:1-8, ambapo tunamwona Yesu akiwa anaponya na kupoza wagonjwa ambapo kila alieponywa aliambiwa “umesamehewa dhambi zako” chukua godoro lako na uende zako
▶Kitendo hicho cha kusema “umesamehewa dhambi” zako kiliwaudhi mafarisayo wakaanza kusemezana wao kwa wao huyu ninani hata asamehe dhambi lakini wasitambue nini wana kisema.
▶Mafarisayo waliendelea kusemezana wao kwawao nanafsi zao kwamba Yesu anakufuru(anaasi) kusema kwa mgonjwa amesamehewa dhambi hii ili kuwa nikutotambua mamlaka ya Yesu duniani ama Kristu ninani.
▶Kupitia kisa hiki cha Mathayo9:1-8Tunajifunza mambo yafuatayo juu ya huruma ya Mungu

1.MATESO NA MASUMBUFU TUNAYOPITIA WAKRISTO NI KUTOKANA NA DHAMBI
▶Ndugu zanguni Wakristo Mungu anasema amejaa huruma na neema nyingi lakini utashangaa wakristo wengi wanapita katika magumu nikutokana na dhambi. Ukitaka kuishi maisha ya raha tunza Utakatifu wako.
▶ Kuna wakati unajikuta unapita kwenye majaribu mazito sana kumbe nikutokana na dhambi kumbe dawa ya kuishi maisha ya raha ni kukimbilia huruma za kristo Yesu
▶Tunamwona mwanamke aliopooza aliambiwa umesamehewa dhambi zake .

2.MAGONJWA MENGI HULETWA NA DHAMBI
▶Ukiangalia dunia ya sasa inakabiriwa na magonjwa mazito mfano ukimwi kama tutamua kufuata kanuni nasheria ambazo Mungu ameagiza hakika hatutoweza kupigwa na magonjwa ya ajabu
▶lakini kwa huruma yake anasema “atatuponya magonjwa yetu yote na ataukomboa uhai wetu na kaburi” kumbe hata kama tumemtenda dhambi Tuombe toba ili huruma yake iendelee kutembea nasi.

3.TUNATAKIWA KUTAFAKARI MASHAURI YETU MBELE ZA MUNGU
▶Wakati Yesu anaponya wagonjwa mafarisayo walianza kusema inakuaje anasamehe dhambi hili lili kuwa nishauri ambilo kwao waliona ni kufuru.
▶Wakristo wa leo ili kuikimbikia huruma ya Bwana tunatakiwa kulifuata shauri la Bwana tutakuwa salama maana ndimo huruma ya kristo hutembea kuwahudumia walio wake.(Zaburi1:1-6)

4.MUNGU PEKEE NDIO MFARIJI WA KWELI
▶Ndugu zangu washarika tunatakiwa tutambue kuwa Yesu kristo ndio mfariji pekee ama chaguo la kwanza la kukimbilia wengine huenda kutafuta faraja kwa wagaga,marafiki,na watu wengine lakini faraja yao ni ya mda tu kimbia sasa mbio mbele za kristo akufute machozi.2Wakoritho7:5-10
▶Nandiomaana anasema njooni kwangu msumbukao na kulemewa na mizigo nami nitawapumzusha.

MWISHO
▶Siku ya leo tunaitwa na huruma hii katika Isaya 1:18 ya kwamba twende tukasemezane naye iliatubadirishe na kututengeneza haijalishi mwanzo wetu ulikuwaje
KUMBUKA:Mabadiriko huanzia ndani ya Moyo wako
▶Mungu anisaidie na akusaidie ili tuweze kutambua huruma yake maishani mwetu.
AMEN.

MUHTASARI WA MAHUBIRI YA LEO 12/07/2020

SOMO: UFUASI NA UANAFUNZI

Yohana 6:66-71
Yeremia 1:17-19

UTANGULIZI
 Jumapili ya leo tunajifunza juu ya Ufuasi na Uanafaunzi
 UFUASI ni hali ya kufuata itikadi, mwenendo au kitu Fulani
 UANAFUNZI ni hali ya kuwa katika mafunzo
 Kwa maelezo haya mtu huwezi kuwa mwanafunzi kabla kuwa mfuasi, sababu lazima uwe na itikadi ambayo unataka kujifunza ili uweze kuwa mwanafunzi
 Mkristo ni mtu aliyekubali kumfuata Yesu Kristo na Yesu anamfanya kuwa mwanafunzi wake ili aweze kujifunza kwake(Yesu) ( Luka 9:62)
 Somo ambalo tunatafakari leo juu ya mada hii ni kutoka Yeremia 1:17 – 19
 Nabii Yeremia ni mfuasi na mwanafunzi wa Yesu ambapo katika mistari hii Mungu Mungu anamwambia Yeremia pamoja na sisi jinsi ya kuwa mfuasi na mwanafunzi mzuri kwake.

1. UFUASI NA UANAFUNZI UNAHITAJI UTII NA UAMINIFU
 Mtumishi mwaminifu wa Mungu anakuwa mtii kwa yote anayoelezwa na Mungu. Mtumishi asiyemwaminifu Mungu anasema mtu wa namna hiyoa ataadhibiwa sana
 Mungu anatutaka tuifanye kazi yake kama alivyotupa wito tulipokubali kuwa wafuasi na wanafunzi wake.

2. UFUASI NA UANAFUZNI UNAHITAJI UVUMILIVU NA USTAHIMILIVU
 Mkristo anao uwezo wa kukabiliana na changamoto zote anazokabiliana nazo kwa kulifahamu neno la Mungu (Mt 4: 1 – 11)
 Wanaokuchukia wasikuyumbishe wala kukurudisha nyuma katika ufuasu na uanafunzi wako kwa sababu ni wale ambao wanapinga kweli ya neno la Mungu ( Yn 15:18 – 25)
 Pamoja na upinzani wote mfuasi na mwanafunzi wa Yesu anapaswa kusimamia neno la Mungu katika uaminifu na utakatifu wake huku akilisema neno la Mungu bila upendeleo wowote.

3. UFUASI NA UANAFUZNI UNAHITAJI KUTOKUYUMBISHWA.
 Majaribu na vikwazo ni sehemu ya utumishi wetu, hivyo tusiogope maana Mungu yu pamoja nasi ( Yer 37:16, Yer 38:6)
 Mtumishi anayemtii Mungu lazima atashinda pamoja na changamoto zote atakazokutana nazo ( Rum 8:35 – 39)

HITIMISHO
 Mungu alikuja kwa watu wake na wote waliompokea aliwapa uwezo wa kufanyika watoto wake na hao ndio wale waliaminio jina lake.
 Mungu atusaidie ili tuwe wafuasi na wanafunzi waaminifu kwa Mungu wetu na tufanyike watoto wake.
AMEN.

MUHTASARI WA MAHUBIRI YA LEO TAREHE 05/07/2020 SIKU KUU YA VIJANA

MASOMO
Zaburi 37:25-40
1samwel 17:38-45
Mathayo 11:25

Wazo la wiki:NGUVU YA VIJANA KATIKA KANISA
____________________________

Somo:MAISHA YA USHINDI YA KIJANA MKRISTO

Fungu:1 YOHANA 2: 12 – 17

UTANGULIZI
• Jumapili ya Leo Tunajifunza maisha ya ushindi ya kijana Mkristo. Yohana ambaye alianza huduma ya uanafunzi wa Yesu akiwa na umri mdogo tu wa miaka 16 na sasa amekuwa mzee na anawaandikia wakristo wote akiwapa ushauri jinsi ya kuendenda kwenye ulimwengu huu huku wakihakikisha kuwa wanaupata ufalme wa Mungu.

• Katika mistari hii tuliyoisoma katika waraka huu Yohana anawagawanya wasomaji wake katika makundi matatu

TOBA NI MWANZO WA ULINZI WA MUNGU KATIKA MAISHA YETU.
• Kundi la kwanza ni watoto ambao wao ndio wameupokea ukristo anawaambia kuwa safari yao ya Ukristo inaanza na msamaha wa dhambi na anawahakikishia kuwa uhusiano wao na Mungu umerudishwa kama uhusiano wa baba na mtoto.

• Kundi la pili na la kina baba, hawa ni wakristo wa muda mrefu anawaonyesha uhuhimu wa kuwa na kumbukumbu katika maisha yao na kujua kuwa hata kama wana uzoefu wa Kiroho namna gani huwezi kumshinda Mungu bado unapaswa kuendelea kumtegemea wakati wote.

• Kundi la tatu ni vijana, anazungumza na kundi hili akilionyesha kuwa lina nguvu, limekuwa na uwezo wa kumshinda shetani na neno la Mungu linakaa kwa wingi ndani yao.

• Sifa hizi ni sifa za kundi hili la vijana, kuwa wana nguvu, neno la Mungu linakaa ndani yao na limewawezesha kumshinda yule mwovu.

• Analiambia kundi hili kuwa mapambano yapo katika maisha yao ila uwezekano wa kushinda upo sababu wapo kwenye nafasi nzuri ya kushinda.

• Neno la Mungu lililopo kwa wingi ndani yao ni chanzo chema cha hekima ya kujua jinsi ya kumpinga yule mwovu. ( Lk 4:1 – 13, Mt 4:1 – 11)

• Makundi yote haya matatu Yohana anayataka, kwanza, yanapaswa kupendana na pili yanapaswa kuchukia mambo ya giza ambayo anayaita mambo ya dunia na anatutaka tujitenge mbali na dunia kwa sababu hatuwezi kupenda dunia na Mungu ( 1Yoh 2:15, Mt 6:24)

a. Ni Dunia gani anayoizungumzia Yohana?
b. Dunia hii ni ya aina gani?
c. Dunia hii ina sifa hani?
d. Je, tunaweza vipi kuishinda dunia hii?

NI DUNIA GANI ANAYOIZUNGUMZIA YOHANA?
• Yohana hazungumzii dunia hii iliyoumbwa na Mungu ( Mdo 17:24) wala kuhusu dunia ya utu wa mtu ( Yn 3:16)

• Dunia anayoitaja Yohana inatokana na neno Kosmos lenye maana ya utaratibu au mpango wa mfumo wa utaratibu wa mwanadamu

• Dunia hii ni mfumo wa mawazo na matendo yanayomhusu mtu katika jambo Fulani. MF. Juma yupo kwenye dunia ya siasa, maana yake Juma anajishughulisha na siasa zaidi.

• Dunia hii ni maisha na mpango wa mwanadamu vinavyotengenezwa bila kumkali Mungu na mapenzi yake na katika hali hiyo ni chini ya shetani

DUNIA HII NI YA AINA GANI?
• Dunia hii na tamaa zake zitapita sio za milele na yule anayeitegemea pia hatadumu (1Yoh 2:17) na hata kama mtu huyo anaonyesha kushinda sasa ila mwisho wake utafika ( Uf 20:7 – 10, uf 21:1- 4)

• Dunia hii inamshambulia mwanadamu katika ukamilifu wake ( 1Thes 5:23) Kiroho, kimwili na kisaikolojia. Anatushambulia kiroho ili tusimpende Mungu, kimwili ili tusiweze kuishi kwa ajili ya Mungu na kisaikolojia ili tushindwe kujifunza kwa Mungu. Mfano wakati wa anguko. ( Mwa 3)

a. Hawa aliona mti unapendeza macho na kumuondoa katika kumpenda Mungu(mashambulizi ya rohoni)
b. Mti Watamanika kwa Maarifa, hapo shetani anamuondoa Hawa katika kujifunza kwa Mungu( mashambulizi ya kisaikolojia)
c. Wafaa kwa chakula anamuondoa Hawa katika maisha ya kuishi kwa ajili ya Mungu na kumtegemea yeye (mashambulizi ya Kimwili)

DUNIA HII INA SIFA GANI?
Biblia inatueleza wazi sifa za Dunia hii
a) Dunia ya namna hii ina kiongozi wake ambaye ni shetani ( 2Kor 4:14, Yn 12:31)
b) Ni dunia ya uovu ( 1Yoh 5:19)
c) Dunia hii ina watoto wake ( Lk 16:8)
d) Dunia hii ina hekima yake yenyewe ( 1Kor 2:6)
e) Dunia hii ni chafu ( 2Pet 1:4)
f) Dunia hii ndio iliyomsulubisha Yesu ( 1Kor 2:8)

TUNAWEZAJE KUSHINDA DUNIA HII?
Ili kuwaeza kuishida dunia hii lazima upambane nayo kimwili, Kiroho na kisaikolojia (nafsi)
a) Njia ya kushinda ulimwengu huu kimwili ni kujitenga na dhambi(1Thes 5:22) Ruhusu hamu yako ya kuishi kwa ajili ya Mungu iongoze njia na kazi zako
b) Ili uweze kuishinda dunia hii kisaikolojia ( 1 Yoh 5:4b) Ruhusu hamu ya kujifunza kwa Mungu ikuze ufahamu wako na uelewa wako
c) Ili uweze kupambana Kiroho ni kujisalimisha kwa Mungu ( Yak 4:7) Ruhusu hamu ya kumpenda Mungu iongoze maamuzi yako.

HITIMISHO
• Tunapaswa kujua kuwa ulimwengu unapita ila Mungu atadumu nasi milele ( 1 Tim 6: 11 – 12)