Category Archives: Uncategorized

03/05/2020 JUBILATE – MPIGIENI BWANA KELELE ZA SHANGWE MADA: MAISHA MAPYA NDANI YA KRISTO YESU

KKKT DAYOSISI YA KUSINI,JIMBO LA NJOMBE, USHARIKA WA UWEMBA,
MTAA WA MJIMWEMA

MAHUBIRI YA SIKU YA BWANA YA 3 BAADA YA PASAKA TAREHE 03/05/2020

JUBILATE – MPIGIENI BWANA KELELE ZA SHANGWE

MADA: MAISHA MAPYA NDANI YA KRISTO YESU

MASOMO: ZABURI 107: 25 – 32, MATHAYO 9:14 – 17, *ISAYA 25: 1 – 8

SHABAHA: Wasikilizaji waweze kuelewa kuwa Ndani ya Yesu yanapatikana maisha ya ushindi hivyo wamtegemee daima.

UTANGULIZI
Bwana Yesu asifiwe, Jumapili ya leo tunajifunza juu ya maisha mapya ndani ya Kristo Yesu. Kwa tafsiri yangu juu ya mada hii ni kuwa yapo Maisha ndani ya Yesu ambayo kila mmoja hapa anayo na pia kuna maisha mapya ndani ya Yesu Kristo ambayo baadhi yetu tunayo maisha hayo.

Naweza kusema Maisha ndani ya Yesu Kristo ni maisha yale ya mazoea ambayo unatambua kuwa Yesu yupo, na umesikia akitenda mambo ya ajabu lakini hilo halikuzuii wewe kutenda kwa kiburi, dharau na majivuno.

Na Maisha mapya ndani ya Yesu Kristo ni maisha yenye mabadiliko, maisha yanayomtegemea Mungu na kuziona nguvu zake zikitenda kazi. Yaani ni maisha yenye mafanikio yanayotambua kuwa Mungu ameahidi kutufundisha ili tuweze kupata faida. (Isaya 48:17)

Katika kusindikiza mada tuliyopewa leo ya Maisha Mapya ndani ya Kristo Yesu tumepewa neno la Mungu kutoka Isaya 25: 1 -8 ambapo tunajifunza mambo kadhaa ambayo ni:-

1. LENGO LA MUNGU KURUHUSU ADHABU KATIKA MAISHA YETU NI ILI TUKUMBUKE UWEPO WAKE NA KUMUABUDU.
Kama nilivyoeleza kwenye utangulizi kuwa maisha ndani ya Mungu ni maisha ya mazoea, sasa Mungu anapotaka kuondoa haya mazoea anaruhusu adhabu kidogo ili tuweze kumkumbuka na tumsifu.

Isaya hapa anazungunza katika wimbo wake wa shukrani kuwa Mungu ameviharibu vitu ambavyo wanadamu walivijenga kwa kiburi chao na uwezo wao, maisha yamekuwa ni uchungu mtupu na miji ya kifahari imekuwa magofu hakuna wakaaji kabisa na kwa hilo mataifa watishao wataogopa lakini lengo lake lipo kwenye ule mstari wa tatu ambalo ni ili watu walio hodari katika hali hii wabaki wakimtukuza Mungu.

Kipindi hiki ambacho tunapitia hatari hii ugonjwa huu wa Corona ni kipindi ambacho tunaona kweli maisha yamekuwa machungu, miji mikubwa inabaki kuwa magofu watu wake wanakufa kweli na hata kwetu na mataifa makubwa yanayotisha yannaogopa sana sitaki kusema hili ni pigo kutoka kwa Mungu ili tumrudie ila nasema kwa kupitia hili watu wengi wamemrudia Mungu na wale walio hodari hata katika shida hii hawataacha kumtukuza Mungu.

2. MAISHA MAPYA NDANI YA YESU KRISTO NI MAISHA YA MABADILIKO
Maisha mapya ndani ya Kristo Yesu ni maisha ambayo yanashuhudia mabadiliko kila siku ni maisha ambayo mtu anashuhudia nguvu za Mungu na kuzikiri kweli kweli.

Neno la Mungu katika Isaya linaonyesha wazi kuwa ni maisha ambayo yanatoa nafuu kwa wote wanaoteswa ( ni ngome kwa maskini mhitaji katika dhiki yake, mahali pa kukimbilia wakati tufani) kuwanyamazisha watesi wote wanaojishughulisha na maisha ya watu wa Mungu.(Wale wanaoshangilia kwa kututesa sababu wanaona wameshinda hakika watashushwa)

3. MABADILIKO YA KWELI YANALETA FURAHA KWA MUNGU INAYOLETA MAFANIKIO KATIKA MAISHA YETU
Kama nilivyoeleza tangu awali kuwa maisha mapya ndani ya Kristo Yesu ni maisha yanyoleta mabadiliko na mabadiliko hayo yanapokuwa ya kweli yanaleta mafanikio katika maisha yetu.

Neno la Mungu katika Isaya linaeleza wazi kuwa Mungu atafanya sherehe na wote wanaomtegemea na katika sherehe hiyo Mungu atafanya mambo kadhaa ambayo ni:-

a) Atawaharibu maadui zetu wote

b) Atafuta machozi yote

c) Ataondoa huzuni tote

d) Ataiondoa aibu yote iliyotukabili

e) Ataondoa kifo hata Milele.

Kipindi hiki tumeitwa sana katika kutubu ili Mungu atuondolee ugonjwa huu wa Covid-19 na tukihimizana kurejea kitabu cha Mambo ya Nyakati wa pili 7:14. Ukweli unabaki kuwa toba inahitaji mabadiliko ya kwelikweli ili mabadiliko hayo yaweze kutuondolea adui yetu huyu, kutufuta machozi, kutuondolea huzuni na hata aibu ambayo inaonekana kwetu kwa sababu tumeruhusu ibada kuendelea.

Mabadiliko ya kweli ya rohoni na mwilini. Mwilini tukifuata ushauri wa wataalamu kukabiliana na adui huyu mkubwa kwa sasa Covid -19 kama vile kunawa mikono mara kwa mara, kuvaa barakoa, kukaa umbali wa mita moja kati ya mtu na mtu, kutokuwa na safari zisizokuwa na sababu ya msingi nk
Rohoni tukiendelea kumuomba Mungu kwa nguvu zetu zote na uwezo aliotujalia, tukitubu na kumkataa shetani na kazi zake zote na mambo yake yote.

HITIMISHO
Tuendelee kumtegemea Mungu na kumtumikia kwa uaminifu na hakika upya wa maisha yetu ndani ya Yesu Kristo utaonekana kwa mafanikio.
AMEN.
@Evjohn
0768386606

WAJIBU WAKO

UNAWAJIBIKA NA MAISHA YAKO MWENYEWE. “Maana kila mtu atalichukua furushi lake mwenyewe.” (Wagalatia 6:5) “Basi ni hivyo, kila mtu miongoni mwetu atatoa habari/hesabu zake mwenyewe mbele za Mungu.” (Warumi 14:12) “Roho itendayo dhambi, ndiyo itakayokufa; mwana hatauchukua uovu wa baba yake, wala baba hatauchukua uovu wa mwanawe, haki yake mwenye haki itakuwa juu yake, na uovu wake mwenye uovu utakuwa juu yake.”
(Ezekieli 18:20)

Kwa msisitizo wa kipekee kabisa maandiko haya yanatuonesha kwamba kila mtu anawajibika na maisha yake mwenyewe. Hata mbele za Mungu hakuna atakaye hukumiwa kwa dhambi za mtu mwingine. Kwa maana hiyo hiyo basi hakuna anayewajibika na maisha ya mtu mwingine. Kwa mujibu wa maandiko haya ni makosa makubwa kuwa na MAWAZO TEGEMEZI, AKILI TEGEMEZI. Ile dhana ya KULAUMU WATU KWA SABABU HAWAJAKUSAIDIA inakemewa vikali na maandiko haya.
Simama upiganie maisha yako mwenyewe sio lazima watu wakusaidie hata kama uwezo wanao. Jukumu la kwanza la Baba yako ni kwa mke wake. Wewe ukishafika Miaka 18 unapaswa kuwaza kesho yako itakuwaje. Jukumu kubwa la Kaka na Dada zako ni maisha yao na watoto wao. Wewe sio jukumu lao. Acha kulaumu watu na usimame kutengeneza maisha yako mwenyewe.

Kama unataka kufunga Ndoa fanya unachomudu, usijiwekee bajeti kubwa kwa kuangalia mifuko ya watu. Kama hauna fedha achana na kusherekea Birthday, kunywa maji mshukuru Mungu. Kama umekosa kodi kalale kanisani saidiana na mlinzi ukiumwa mbu utapata akili ya kutafuta hela. Lakini usiwe mzigo kwa mtu yeyote na kulaumu na kuchukia watu. “Oh hawanisadii chochote!” Nani alikwambia unapaswa kusaidiwa!? KASIRIKA, CHUKIA, NUNA LAKINI UJUMBE NDIO UMEUPATA, PIGANIA MAISHA YAKO. KAMA AMBAVYO UTAHUKUMIWA KWA DHAMBI ZAKO MWENYEWE BASI VIVYO HIVYO AMUA KUFANIKIWA KWA JASHO LAKO MWENYEWE. -evjohn whatsup 0767386606
#2020

SIJAVIZOEA

SIJAVIZOEA.: 1 Samweli 17:38 Ndipo Sauli akamvika Daudi mavazi yake ya vita, akamtia chapeo cha shaba kichwani, akamvika dirii. 1 Samweli 17:39 Naye Daudi akajifunga upanga juu ya mavazi yake, akajaribu kwenda; maana alikuwa hajavijaribu. Daudi akamwambia Sauli, SIWEZI KWENDA na VITU HIVI, MAANA SIKUVIJARIBU (SIJAWAHI KUVITUMIA/SIJAVIZOEA). BASI DAUDI AKAVIVUA. 1 Samweli 17:40 AKAICHUKUA FIMBO YAKE MIKONONI, AKAJICHAGULIA MAWE LAINI MATANO KATIKA KIJITO CHA MAJI, AKAYATIA KATIKA MFUKO WA KICHUNGAJI ALIOKUWA NAO, MAANA NI MKOBA WAKE, NA KOMBEO LAKE ALIKUWA NALO MKONONI MWAKE, AKAMKARIBIA YULE MFILISTI. Mara nyingi huwa tunasubiri Mungu atupe wazo jipya la biashara au namna mpya ya utendaji ili tuweze kufanikiwa na tunasumbuka sana kuiga mifumo ya watu wengine na kuacha kuboresha kile ambacho tunakijua na kufanya kwa ubora tunasubiri wazo jipya na namna mpya ili kufanikiwa na kujikuta tunajichelewesha. Nimegundua mara nyingi sana Mungu huwa anatumia kile tunachokijua na kukiboresha ndipo hapo anatufanya kuwa bora na tofauti. Anamuuliza Musa “BWANA akamwambia, Ni nini hiyo uliyo nayo mkononi mwako? Akasema, NI FIMBO. Akamwambia, Itupe chini; akaitupa chini, nayo ikawa nyoka; Musa akakimbia mbele yake.” (Kutoka 4:2-3) Kipawa hicho unachokidharau, huduma hiyo hiyo unayoichukulia kawaida, biashara hiyo hiyo ya kawaida, ujuzi na uwezo ulionao ndio Mungu huwa anatumia kukufanya kuwa Mkuu. Usitafute sana kubuni ndege nyingine wakati unaweza kuboresha hii iliyopo na ukatajirika. USIHANGAIKE KUFUNGUA CHAMPAGNE 🍾 NA VIDOLE WAKATI UMEZOEA KUFUNGUA SODA KWA MENO, TUMIA UJUZI WAKO, ANAYEKUONA MSHAMBA NI KWA SABABU ANA NAMNA YAKE YA KUFANYA. KUWA BORA KATIKA NAMNA YAKO. – Ev.john

TAFAKURI YA JUMATANO YA MAJIVU 26/04/2020

Kesho nisiku pekee ambayo kanisa linaingia majira mapya yanayoitwa Kwaresma nasisi kama KKKT doyosisi ya kusini tunatoa tafakari fupi ya JUMATANO YA MAJIVU Jumatano ya majivu ni siku ya kwanza kwenye kipindi kiitwacho kwaresma ambapo siku hii inatukumbusha wakristo ya kwamba sisi ni mavumbi na mavumbini tutarudi kadiri ya agizo la Mungu katika mwanzo3:19 …….” hata utakapoirudia ardhi, ambayo katika hiyo ulitwaliwa; kwa maana u mavumbi wewe, nawe mavumbini utarudi” Shabaha ya kuwekwa kwasiku hii nikutaka kuamsha akili za waumini ama washarika kutambua nafasi ya toba katika maisha haya mafupi Jumatano ya majivu kwamakanisa mengine kama oxthodox na katoliki huwapaka waumini wao majivu katika paji la uso wao ili kuwakumbusha inatupasa tuwe watu watoba lakini hiyo niishara ya nje ambayo hata mitume na manabiib waliitumia wakati wakifunga walivaa magunia nakujipaka majivu kuonyesha wanaomboleza ama unyenyekevu mbele za Mungu SHABAHA YA HII SIKU Kwet kama kanisa la kiinjili lakilutheri tumepewa mstari wakesho ambao ni Yoeli3:19a nakichwa ama wazo linasema KUTUBU NA KUREJEA KWA BWANA kwanza mkristo unatakiwa ujitathimini maisha yako je unaishi maisha yatoba ama unasubiri mpaka itokee kwenye kwaresma?? Kitu kingine mkristo anatakiwa ajifanyie hesabu ama tafakari fupi tokea kwarsma ya mwaka jana mapaka leo umesimama vizuri kwenye imani ambayo Yesu alituachia ama umekuwa mguu pande. KUTUBU NA KUREJEA KWA BWANA Ndugu zangu waamini …Bwana asifiwe tunapoanza majira haya ya toba siku 40 umejipangaje iliuwe kamili mbele za Mungu kumbuka yesu anatuambia “njoni kwangu nyinyi nyote msumbukao na kulemewa na mizigo ya dhambi nami nitawapumzisha” Mizigo mingapi inakulemea ndugu yangu kiasi kwamba hujapata mahali pakutua lakini yesu anatuambia utue kwake. Itaendelea kesho………@Evjohn