TAFAKURI YA JUMATANO YA MAJIVU 26/04/2020

Kesho nisiku pekee ambayo kanisa linaingia majira mapya yanayoitwa Kwaresma nasisi kama KKKT doyosisi ya kusini tunatoa tafakari fupi ya JUMATANO YA MAJIVU Jumatano ya majivu ni siku ya kwanza kwenye kipindi kiitwacho kwaresma ambapo siku hii inatukumbusha wakristo ya kwamba sisi ni mavumbi na mavumbini tutarudi kadiri ya agizo la Mungu katika mwanzo3:19 …….” hata utakapoirudia ardhi, ambayo katika hiyo ulitwaliwa; kwa maana u mavumbi wewe, nawe mavumbini utarudi” Shabaha ya kuwekwa kwasiku hii nikutaka kuamsha akili za waumini ama washarika kutambua nafasi ya toba katika maisha haya mafupi Jumatano ya majivu kwamakanisa mengine kama oxthodox na katoliki huwapaka waumini wao majivu katika paji la uso wao ili kuwakumbusha inatupasa tuwe watu watoba lakini hiyo niishara ya nje ambayo hata mitume na manabiib waliitumia wakati wakifunga walivaa magunia nakujipaka majivu kuonyesha wanaomboleza ama unyenyekevu mbele za Mungu SHABAHA YA HII SIKU Kwet kama kanisa la kiinjili lakilutheri tumepewa mstari wakesho ambao ni Yoeli3:19a nakichwa ama wazo linasema KUTUBU NA KUREJEA KWA BWANA kwanza mkristo unatakiwa ujitathimini maisha yako je unaishi maisha yatoba ama unasubiri mpaka itokee kwenye kwaresma?? Kitu kingine mkristo anatakiwa ajifanyie hesabu ama tafakari fupi tokea kwarsma ya mwaka jana mapaka leo umesimama vizuri kwenye imani ambayo Yesu alituachia ama umekuwa mguu pande. KUTUBU NA KUREJEA KWA BWANA Ndugu zangu waamini …Bwana asifiwe tunapoanza majira haya ya toba siku 40 umejipangaje iliuwe kamili mbele za Mungu kumbuka yesu anatuambia “njoni kwangu nyinyi nyote msumbukao na kulemewa na mizigo ya dhambi nami nitawapumzisha” Mizigo mingapi inakulemea ndugu yangu kiasi kwamba hujapata mahali pakutua lakini yesu anatuambia utue kwake. Itaendelea kesho………@Evjohn

One thought on “TAFAKURI YA JUMATANO YA MAJIVU 26/04/2020”

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *