MAHUBIRI YA JUMAPILI TAREHE 28/06/2020

Somo:NEEMA YA MUNGU ITUOKOAYO
Masomo:
Zaburi 59:1-9
Matendo 11:1-15
*Luka 8:26-39

SHABAHA: Wasikilizaji waweze kuelewa kuwa ili kupata ahadi za Mungu tunapaswa kumtegemea Mungu.

“Kwa kuwa mwana wa Adamu alikuja kutafuta na kuokoa kile kilichopotea” (Lk 19:10)

UTANGULIZI: Leo ikiwa ni siku ya tatu baada ya utatu tunaangalia mada izungumzayo juu ya Neema ya Mungu ambayo inatuwezesha sisi kuupata wokovu.

> Neema maana yake ni mafanikio aliyonayo mtu kutokana na majaaliwa ya mwenyezi Mungu au kwa juhudi zake mwenyewe.

> Hivyo:- tunaweza kusema kuwa leo tunazungumzia juu ya mafanikio aliyonayo mtu kutoka kwa mwenyezi Mungu ambayo yanaleta wokovu katika maisha ya mtu.

> Katika kutafakari Neema hii ya Mungu iletayo wokovu tumepewa kisa kutoka katika biblia Luka 8:26 – 39. Kisa hiki ambacho kimeelezwa hapa pia kimeelezwa katika kitabu cha mathayo 8:28-34 na kitabu cha Marko 5:1-20 ikizungumza habari ya mtu aliyepagawa na pepo wachafu ambao wamejitambulisha kwa jina la Legion maana yake ni jeshi kubwa la warumi lenye nguvu lililokwa na idadi ya wanajeshi 6000.

Katika kisa hiki unajifunza mambo yafuatayo:-

SHETANI NI MHARIBIFU

Mtu huyu ambaye amepagawa nna pepo tunaambiwa kuwa alikuwa Uchi, aliishi makaburini, na alikuwa akijikatakata na mawe (Marko 5:3) Shetani anapoingia kwetu hahurumii hata miilil yetu atatutaabisha na kuwa wahitaji wakati wote.

ULINZI WA KIBINADAMU HAUJITOSHELEZI

Mtu huyu alifungwa kwa pingu na hata kwa minyororo ila aliikata yote na wanadamu wakakata tama nay eye na kumuacha alivyo. Unaweza kutegemea wanadamu wanaweza kukusaidia ila ni kwa kitambo kidogo na utabaki katika shida yako.

BINADAMU WENGI WANAANGALIA KITU KULIKO UTU

Tunaelezwa kuwa baada ya mtu huyu kuponywa watu wa mji ule walimfukuza Yesu kwa sababu walipiga hesabu ya hasara ya nguruwe 2000 waliofia majini waliona mwenzao amepata hasara kubwa sasa hawakujua nani angefuata wakaogopasana wakaamua kumwambia aondoke kwao.

MUNGU ANAJISHUGHULISHA NA MAHITAJI YETU

Yesu alivyoona kuwa mtu huyu yupo uchi, anaishi makaburini mbali na watu na alikuwa akijikata mwili kwa mawe alijua kuwa anahitaji msaada hivyo aliona nguruwe hawana umuhimu kama mtu wake akayaelekeza mapepo kwa nguruwe na kumponya yule kijana. Mapepo yalikwepa kwenda kuzimu yakidani kuwa yakiingia kwa nguruwe yatakuwa salama ila baada ya kuingia nguruwe walikufa wote na mapepo bado yakaenda kuzimu.

UKIMKUBALI MUNGU UTAKUWA SALAMA

Baada ya mtu huyu kuponywa alitulia chini ya miguu ya Mungu akiwa amevaa nguo na akiwa na akili yake timamu. Amani ya kweli inapatikana kwa kumkubali Yesu

MEMA ANAYOKUTENDEA MUNGU ANATAKA UMTUMIKIE

Mtu aliyeponywa alitaka kandamana na Yesu ila yesu alimwambia aende kuelezea habari njema za Yesu kwa watu wa nyumbani kwake kwa kuwa eneo lile liikuwa ni eneoo la wapagani nao waone wema wake. Baraka tunazopata tunatumwa tukahubiri.

HITIMISHO

Bora kuwa mlinzi wa getini kwa Mungu kuliko kuwa mfalme au malkia nje ya Mungu sababu huko hakuna mafanikio ya kweli, mafanikio ya kweli yaletayo wokovu yanapatikana kwa Mungu tu.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *