MUHTASARI WA MAHUBIRI YA LEO 12/07/2020

SOMO: UFUASI NA UANAFUNZI

Yohana 6:66-71
Yeremia 1:17-19

UTANGULIZI
 Jumapili ya leo tunajifunza juu ya Ufuasi na Uanafaunzi
 UFUASI ni hali ya kufuata itikadi, mwenendo au kitu Fulani
 UANAFUNZI ni hali ya kuwa katika mafunzo
 Kwa maelezo haya mtu huwezi kuwa mwanafunzi kabla kuwa mfuasi, sababu lazima uwe na itikadi ambayo unataka kujifunza ili uweze kuwa mwanafunzi
 Mkristo ni mtu aliyekubali kumfuata Yesu Kristo na Yesu anamfanya kuwa mwanafunzi wake ili aweze kujifunza kwake(Yesu) ( Luka 9:62)
 Somo ambalo tunatafakari leo juu ya mada hii ni kutoka Yeremia 1:17 – 19
 Nabii Yeremia ni mfuasi na mwanafunzi wa Yesu ambapo katika mistari hii Mungu Mungu anamwambia Yeremia pamoja na sisi jinsi ya kuwa mfuasi na mwanafunzi mzuri kwake.

1. UFUASI NA UANAFUNZI UNAHITAJI UTII NA UAMINIFU
 Mtumishi mwaminifu wa Mungu anakuwa mtii kwa yote anayoelezwa na Mungu. Mtumishi asiyemwaminifu Mungu anasema mtu wa namna hiyoa ataadhibiwa sana
 Mungu anatutaka tuifanye kazi yake kama alivyotupa wito tulipokubali kuwa wafuasi na wanafunzi wake.

2. UFUASI NA UANAFUZNI UNAHITAJI UVUMILIVU NA USTAHIMILIVU
 Mkristo anao uwezo wa kukabiliana na changamoto zote anazokabiliana nazo kwa kulifahamu neno la Mungu (Mt 4: 1 – 11)
 Wanaokuchukia wasikuyumbishe wala kukurudisha nyuma katika ufuasu na uanafunzi wako kwa sababu ni wale ambao wanapinga kweli ya neno la Mungu ( Yn 15:18 – 25)
 Pamoja na upinzani wote mfuasi na mwanafunzi wa Yesu anapaswa kusimamia neno la Mungu katika uaminifu na utakatifu wake huku akilisema neno la Mungu bila upendeleo wowote.

3. UFUASI NA UANAFUZNI UNAHITAJI KUTOKUYUMBISHWA.
 Majaribu na vikwazo ni sehemu ya utumishi wetu, hivyo tusiogope maana Mungu yu pamoja nasi ( Yer 37:16, Yer 38:6)
 Mtumishi anayemtii Mungu lazima atashinda pamoja na changamoto zote atakazokutana nazo ( Rum 8:35 – 39)

HITIMISHO
 Mungu alikuja kwa watu wake na wote waliompokea aliwapa uwezo wa kufanyika watoto wake na hao ndio wale waliaminio jina lake.
 Mungu atusaidie ili tuwe wafuasi na wanafunzi waaminifu kwa Mungu wetu na tufanyike watoto wake.
AMEN.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *