MUHTASARI WA MAHUBIRI YA LEO 19/07/2020

Somo:HURUMA YA MUNGU

MASOMO
zaburi1:1-69
2Wakoritho7:5-10
Mathayo9:1-8*
UTANGULIZI
▶Jumapili ya leo tunajifunza juu ya huruma ya Mungu kwa wanadamu
▶Katika tafakari hii ya huruma za Mungu tumepewa kutoka injili ya mathayo9:1-8, ambapo tunamwona Yesu akiwa anaponya na kupoza wagonjwa ambapo kila alieponywa aliambiwa “umesamehewa dhambi zako” chukua godoro lako na uende zako
▶Kitendo hicho cha kusema “umesamehewa dhambi” zako kiliwaudhi mafarisayo wakaanza kusemezana wao kwa wao huyu ninani hata asamehe dhambi lakini wasitambue nini wana kisema.
▶Mafarisayo waliendelea kusemezana wao kwawao nanafsi zao kwamba Yesu anakufuru(anaasi) kusema kwa mgonjwa amesamehewa dhambi hii ili kuwa nikutotambua mamlaka ya Yesu duniani ama Kristu ninani.
▶Kupitia kisa hiki cha Mathayo9:1-8Tunajifunza mambo yafuatayo juu ya huruma ya Mungu

1.MATESO NA MASUMBUFU TUNAYOPITIA WAKRISTO NI KUTOKANA NA DHAMBI
▶Ndugu zanguni Wakristo Mungu anasema amejaa huruma na neema nyingi lakini utashangaa wakristo wengi wanapita katika magumu nikutokana na dhambi. Ukitaka kuishi maisha ya raha tunza Utakatifu wako.
▶ Kuna wakati unajikuta unapita kwenye majaribu mazito sana kumbe nikutokana na dhambi kumbe dawa ya kuishi maisha ya raha ni kukimbilia huruma za kristo Yesu
▶Tunamwona mwanamke aliopooza aliambiwa umesamehewa dhambi zake .

2.MAGONJWA MENGI HULETWA NA DHAMBI
▶Ukiangalia dunia ya sasa inakabiriwa na magonjwa mazito mfano ukimwi kama tutamua kufuata kanuni nasheria ambazo Mungu ameagiza hakika hatutoweza kupigwa na magonjwa ya ajabu
▶lakini kwa huruma yake anasema “atatuponya magonjwa yetu yote na ataukomboa uhai wetu na kaburi” kumbe hata kama tumemtenda dhambi Tuombe toba ili huruma yake iendelee kutembea nasi.

3.TUNATAKIWA KUTAFAKARI MASHAURI YETU MBELE ZA MUNGU
▶Wakati Yesu anaponya wagonjwa mafarisayo walianza kusema inakuaje anasamehe dhambi hili lili kuwa nishauri ambilo kwao waliona ni kufuru.
▶Wakristo wa leo ili kuikimbikia huruma ya Bwana tunatakiwa kulifuata shauri la Bwana tutakuwa salama maana ndimo huruma ya kristo hutembea kuwahudumia walio wake.(Zaburi1:1-6)

4.MUNGU PEKEE NDIO MFARIJI WA KWELI
▶Ndugu zangu washarika tunatakiwa tutambue kuwa Yesu kristo ndio mfariji pekee ama chaguo la kwanza la kukimbilia wengine huenda kutafuta faraja kwa wagaga,marafiki,na watu wengine lakini faraja yao ni ya mda tu kimbia sasa mbio mbele za kristo akufute machozi.2Wakoritho7:5-10
▶Nandiomaana anasema njooni kwangu msumbukao na kulemewa na mizigo nami nitawapumzusha.

MWISHO
▶Siku ya leo tunaitwa na huruma hii katika Isaya 1:18 ya kwamba twende tukasemezane naye iliatubadirishe na kututengeneza haijalishi mwanzo wetu ulikuwaje
KUMBUKA:Mabadiriko huanzia ndani ya Moyo wako
▶Mungu anisaidie na akusaidie ili tuweze kutambua huruma yake maishani mwetu.
AMEN.