MUHTASARI WA MAHUBIRI YA LEO TAREHE 05/07/2020 SIKU KUU YA VIJANA

MASOMO
Zaburi 37:25-40
1samwel 17:38-45
Mathayo 11:25

Wazo la wiki:NGUVU YA VIJANA KATIKA KANISA
____________________________

Somo:MAISHA YA USHINDI YA KIJANA MKRISTO

Fungu:1 YOHANA 2: 12 – 17

UTANGULIZI
• Jumapili ya Leo Tunajifunza maisha ya ushindi ya kijana Mkristo. Yohana ambaye alianza huduma ya uanafunzi wa Yesu akiwa na umri mdogo tu wa miaka 16 na sasa amekuwa mzee na anawaandikia wakristo wote akiwapa ushauri jinsi ya kuendenda kwenye ulimwengu huu huku wakihakikisha kuwa wanaupata ufalme wa Mungu.

• Katika mistari hii tuliyoisoma katika waraka huu Yohana anawagawanya wasomaji wake katika makundi matatu

TOBA NI MWANZO WA ULINZI WA MUNGU KATIKA MAISHA YETU.
• Kundi la kwanza ni watoto ambao wao ndio wameupokea ukristo anawaambia kuwa safari yao ya Ukristo inaanza na msamaha wa dhambi na anawahakikishia kuwa uhusiano wao na Mungu umerudishwa kama uhusiano wa baba na mtoto.

• Kundi la pili na la kina baba, hawa ni wakristo wa muda mrefu anawaonyesha uhuhimu wa kuwa na kumbukumbu katika maisha yao na kujua kuwa hata kama wana uzoefu wa Kiroho namna gani huwezi kumshinda Mungu bado unapaswa kuendelea kumtegemea wakati wote.

• Kundi la tatu ni vijana, anazungumza na kundi hili akilionyesha kuwa lina nguvu, limekuwa na uwezo wa kumshinda shetani na neno la Mungu linakaa kwa wingi ndani yao.

• Sifa hizi ni sifa za kundi hili la vijana, kuwa wana nguvu, neno la Mungu linakaa ndani yao na limewawezesha kumshinda yule mwovu.

• Analiambia kundi hili kuwa mapambano yapo katika maisha yao ila uwezekano wa kushinda upo sababu wapo kwenye nafasi nzuri ya kushinda.

• Neno la Mungu lililopo kwa wingi ndani yao ni chanzo chema cha hekima ya kujua jinsi ya kumpinga yule mwovu. ( Lk 4:1 – 13, Mt 4:1 – 11)

• Makundi yote haya matatu Yohana anayataka, kwanza, yanapaswa kupendana na pili yanapaswa kuchukia mambo ya giza ambayo anayaita mambo ya dunia na anatutaka tujitenge mbali na dunia kwa sababu hatuwezi kupenda dunia na Mungu ( 1Yoh 2:15, Mt 6:24)

a. Ni Dunia gani anayoizungumzia Yohana?
b. Dunia hii ni ya aina gani?
c. Dunia hii ina sifa hani?
d. Je, tunaweza vipi kuishinda dunia hii?

NI DUNIA GANI ANAYOIZUNGUMZIA YOHANA?
• Yohana hazungumzii dunia hii iliyoumbwa na Mungu ( Mdo 17:24) wala kuhusu dunia ya utu wa mtu ( Yn 3:16)

• Dunia anayoitaja Yohana inatokana na neno Kosmos lenye maana ya utaratibu au mpango wa mfumo wa utaratibu wa mwanadamu

• Dunia hii ni mfumo wa mawazo na matendo yanayomhusu mtu katika jambo Fulani. MF. Juma yupo kwenye dunia ya siasa, maana yake Juma anajishughulisha na siasa zaidi.

• Dunia hii ni maisha na mpango wa mwanadamu vinavyotengenezwa bila kumkali Mungu na mapenzi yake na katika hali hiyo ni chini ya shetani

DUNIA HII NI YA AINA GANI?
• Dunia hii na tamaa zake zitapita sio za milele na yule anayeitegemea pia hatadumu (1Yoh 2:17) na hata kama mtu huyo anaonyesha kushinda sasa ila mwisho wake utafika ( Uf 20:7 – 10, uf 21:1- 4)

• Dunia hii inamshambulia mwanadamu katika ukamilifu wake ( 1Thes 5:23) Kiroho, kimwili na kisaikolojia. Anatushambulia kiroho ili tusimpende Mungu, kimwili ili tusiweze kuishi kwa ajili ya Mungu na kisaikolojia ili tushindwe kujifunza kwa Mungu. Mfano wakati wa anguko. ( Mwa 3)

a. Hawa aliona mti unapendeza macho na kumuondoa katika kumpenda Mungu(mashambulizi ya rohoni)
b. Mti Watamanika kwa Maarifa, hapo shetani anamuondoa Hawa katika kujifunza kwa Mungu( mashambulizi ya kisaikolojia)
c. Wafaa kwa chakula anamuondoa Hawa katika maisha ya kuishi kwa ajili ya Mungu na kumtegemea yeye (mashambulizi ya Kimwili)

DUNIA HII INA SIFA GANI?
Biblia inatueleza wazi sifa za Dunia hii
a) Dunia ya namna hii ina kiongozi wake ambaye ni shetani ( 2Kor 4:14, Yn 12:31)
b) Ni dunia ya uovu ( 1Yoh 5:19)
c) Dunia hii ina watoto wake ( Lk 16:8)
d) Dunia hii ina hekima yake yenyewe ( 1Kor 2:6)
e) Dunia hii ni chafu ( 2Pet 1:4)
f) Dunia hii ndio iliyomsulubisha Yesu ( 1Kor 2:8)

TUNAWEZAJE KUSHINDA DUNIA HII?
Ili kuwaeza kuishida dunia hii lazima upambane nayo kimwili, Kiroho na kisaikolojia (nafsi)
a) Njia ya kushinda ulimwengu huu kimwili ni kujitenga na dhambi(1Thes 5:22) Ruhusu hamu yako ya kuishi kwa ajili ya Mungu iongoze njia na kazi zako
b) Ili uweze kuishinda dunia hii kisaikolojia ( 1 Yoh 5:4b) Ruhusu hamu ya kujifunza kwa Mungu ikuze ufahamu wako na uelewa wako
c) Ili uweze kupambana Kiroho ni kujisalimisha kwa Mungu ( Yak 4:7) Ruhusu hamu ya kumpenda Mungu iongoze maamuzi yako.

HITIMISHO
• Tunapaswa kujua kuwa ulimwengu unapita ila Mungu atadumu nasi milele ( 1 Tim 6: 11 – 12)