MAHUBIRi Ya SIKU YA BWANA YA 12 BAADA YA UTATU

SOMO: TUTUMIE VYEMA NDIMI ZETU

masomo:
Zaburi 134
Mithali 10:11-13
Mathayo 8:1-4*

SHABAHA: WASIKILIZAJI WAELEWE YA KWAMBA KILA NENO LA ULIMI LAZIMA LITATOLEA HESABU KAMA JEMA AU BAYA SIKU YA HUKUMU

UTANGULIZI
Usemi ni uwezo mmojawapo wa mwanadamu wenye nguvu zaidi, kwa sababu kwa maneno yake anaweza kuleta manufaa makubwa, lakini pia anaweza kuleta hasara kubwa ( Mit 12:18,25; Yak 3:5,9)
Mtu awezaye kutawala ulimi wake anaweza kutawala nafsi yake yote ( Yak 3:1-4,7)
Uovu wa mtu huonekana kwa ulimi ambao haujatawaliwa ( Mk 7:21 – 23; Yak 3:6)
Maneno mengi ya mtu huonyesha upumbavu wake hivyo kila mmoja anapaswa kuutawala ulimi wake, utawala huo lazima uwe wa kweli isiwe ni kutumia maneno matamu tu ili afiche mawazo yake, yeye ni mnafiki na unafiki sio mzuri ( Zab 41: 5-6, Mit 10:18, Mt 22:15 – 18)
Ugeuzi wa maneno kwa ujanja au hila ni aina ya uongo ( Mit 12:19, 2Kor 4:2, Efe 4:25) Iwapo mtu anataka aseme ukweli kila wakati pia anatakiwa afanye hivyo kwa roho ya Upendo na maneno yake yaonyeshe tabia yake ( Mit 10:11, 20 – 21; 16:23; Efe 4:15, Yak 1:19)
Usemi wako unaonyesha hali yako ya kiroho na usemi huo utatumiwa siku ya hukumu kama ushahidi wako ( Mt 12: 36 – 37)
Hakuna neno ambalo Mungu halijui katika yale yote unayonena (Zab 139:4)

• Katika mistari hii miwili kutoka katika kitabu cha mithali inatufundisha mambo muhimu yafuatayo kuhusu matumizi ya Ulimi.

1. USEMI WA MWENYE HAKI UNA HEKIMA NA WEMA
Mtu aliye na hekima wakati wote anajua kuutunza ulimi wake, maneno yake wakati wote ni maneno yaliyokolea busara.
Maneno ya mtu wa haki yanatamani kuona mema kwa wengine na yamejaa hekima(Mith 10:20 – 21)
Mtu mwenye hekima si mwepesi wa kusema na akisema maneno yake yamejaa baraka na mema.

2. USEMI WA MTU MWOVU WAKATI WOTE UNADANGANYA NA KUUMIZA(Zab 10:7)
Mtu mwovu wakati wote huwaza mabaya kwa wengine na hupenda kutamka laana kwa watu wengine(Zab 52: 2 – 4)
Maneno yake yamejaa uongo na kujipendekeza( baadhi ya vitu asivyopenda Mungu Mith 6:17)
Mtu mwovu huwa mnafiki na kutaka kujionyesha kuwa ni mwema mbele za watu tu.

3. ULIMI MWOVU UTAADHIBIWA
Mungu atamharibu na kumuondolea mbali mwenye maneno mbaya ( Mith 10:31)
Atakuondoa katika nyumba yako( Zab 52:5)
Kifo kitampata mwenye ulimi wenye hila (Mith 17:20)

HITIMISHO
Mungu atusaidie tuweze kutumia ulimi wetu vizuri tukijua kuwa maneno yetu ipo siku tutayatolea hesabu.
AMEN.
imeandaliwa na mwinjilist John
KKKT -SD Njombe

#0768386606

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *