SIKU YA BWANA YA 13 BAADA YA UTATU

wazo la wiki: JIRANI YANGU

Masomo:
Zaburi 28:1-4
Mathayo 12:46-50
Matendo 28:7-10*
Rangi: KiJANI
Wimbo:TMW 410
UTANGULIZI
Leo tunatafakari juu ya mada ya Jirani zetu tukilitazama neno la Mungu kutoka
Matendo 28:7-10
> Jirani kulingana na tafsiri ya Kiswahili ni mtu yeyote aliye karibu na mahali
unapoishi.
> Jirani mi mtu muhimu sana katika maisha ya kila mtu, yawezekana anaweza kuwa
rafiki yako au adui zako.(Hekima inahitajika kuishi nae)
> Biblia tangu Agano la kale inaelekeza kuwa kila mtu anapaswa kumpenda jirani
yake kama nafsi yake( Law 19:17 – 18)
> Upendo wa namna hii haukuwa rahisi hivyo watu wengi walijitahidi kukwepa
wajibu huo na mara nyingi walihoji ni watu gani wanapaswa kuwa majirani.
Hata kipindi cha Yesu watu walijitahidi kumuuliza swali hili, na Yesu aliweka wazi
kuwa jirani ni :-
a. Mtu yeyote aliye na dhiki ni jirani yetu ( Lk 10: 29 – 37)
b. Jirani ni watu wote hata kama ni adui yetu ( Mt 5: 43 – 47)
Wajibu mkubwa aliopewa mwanadamu ni kumpenda Mungu na Jirani ( Mt 22:36-40,
Rum 13:8-10,Gal5:14,Yak2:8, 1 Yoh 4:20, Mt 3:28, 14:21)
Somo ambalo tumepewa kujifunza juu ya jirani kwa mwaka huu tunajifunza juu ya
jinsi ya kumtendea jirani hasa wale ambao tunafikiria hawawezi kuwa majirani.
1. AMRI IPO TUNAPOSHINDWA KUJITAWALA JUU YA JIRANI ZETU
> Mtu akifanyiwa ovu hupenda kulipa ovu kubwa zaidi na kuanzisha mashindano
baina ya watu waliogombana au kufanyiana maovu.
> Kutokana na kushindwa huku kujitawala hisia zao, kulisababisha haki kukosekana
katikati ya watu.(Law 24: 19 -20)
> Watu walipewa sheria ili iweze kusaidia ili adhabu iweze kulingana na Kosa.
2. WANA WA MUNGU WANAWAZA MEMA JUU YA JIRANI ZAO
> Kama nilivyoeleza kuwa jirani ni mtu yeyote mwenye dhiki hata kama akiwa adui
yako na unapaswa kumpenda kama nafsi yako
> Wajibu huu mzito wa kumpenda jirani kama nafsi yako uliendelea kuwatesa watu
wengi hadi kipindi cha Yesu.
> Kazi kubwa ya kukamilisha torati aliyoifanya Yesu katika mahubiri ya mlimani pia
aligusia suala la jinsi ya kukaa na watu kwa mtazamo mpya wa wana wa Mungu.
 Anawataka watu wa Mungu wasiwe na Mashindano juu ya uovu. Ukishindana
na uovu utajikuta inakuondolea uthamani wa kuwa mwana wa Mungu.
 Mtu akikufanyia jambo la kukuonea wewe usinung’unike fanya kwa upendo
utakaomshangaza mtesi wako; Jitahidi kuwa mkarimu kwake (Rum 12:20)
 Tusing’ang’ane kukariri neno la Mungu pasipo upendo wa kweli ndani yetu
kwa Mungu na jirani zetu
 Kuweka haja za wenzetu mbele kuliko matakwa yetu
 Tuwe na mizigo juu ya wengine (Mith 3:29)
3. MATENDO MEMA KWA JIRANI YANA MALIPO YAKE.
Jirani mtendee mema hata kama unaona hastahili, sababu unavyofanya hivyo sio
kwake tu bali unajitengenezea malipo yako Mbinguni na kujipa kibali cha kuwa
mwana wa Mungu ( Lk 6:35)
HITIMISHO
Mungu atuwezeshe tuweze kutambua thamani ya watu wengine zaidi kuliko makosa
wanayotutendea ili tuweze kuwatendea mema hata pale wanapotuudhi.
AMEN.
imeandaliwa na
Ev.John

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *