MUHTASARI WA MAHUBIRI YA LEO TAREHE 26/07/2020

SOMO: Mwanzo 41:41-45

UTANGULIZI
Bwana Yesu asifiwe, leo tunaangalia juu ya “NEEMA YA MUNGU YATUWEZESHA” yote tunayofanikiwa kuyafanya hapa duniani pamoja na magumu yote tunayopitia neema ya Mungu peke yake ndio inayotuwezesha kuonekana tulivyo, hatuwezi kujivunia akili zetu wala nguvu zetu wenyewe ila wakati wote yote tuyafanyayo tujue kuwa ni Mungu ametuwezesha.
Waandishi na mafarisayo wao walikuwa ni watu wa kushika sheria sana na kujitahidi kwa nguvu zao kuonyesha kuwa wanafahamu juu ya usafi na uchafu wa mtu ila Yesu anapotokea kwao anataka kuwabadiisha namna ya kufiki na kutambua mapenzi ya Mungu na kuondokana na mapokeo ya wazee.
Kwa somo hili tunajifunza haya yafuatayo

1. ASILI YA KWELI YA UNAJISI.
• Wayahudi walikuwa na sheria mbalimbali juu ya vyakula wakionyesha vingine ni safi na vingine ni najisi na hata jinsi ya kujiandaa kula. Walipoona wanafunzi wa Yesu wanakula bila kunawa mikono waliwahesabu kuwa ni najisi.
• Yesu anawataka watu wake kuelewa kuwa unajisi wa kweli hauwezi kuasilishwa na nguvu za nje bali kwa nguvu za ndani.
• Kile unachokipokea na kukiingiza katika mwili wako ndio kinachosababisha nguvu ya kutoa kile kilichopo ndani yako hivyo tunapaswa kuwa makini zaidi.

2. UTAMADUNI/MAZOEA YANAWEZA KUKUFANYA USIMUELEWE YESU
• Wanafunziwakiwa ni miongoni mwa wayahudi kwa kusikia mafundisho ya Yesu juu ya UNAJISI kutokana na maelekezo na torati walizoishi nazo kwa muda mrefu (Walawi 11: 1 – 47, Mt 5:17 – 18) hawakuelewa fundisho la Yesu walifikiri kuwa amekosea na kutaka mafafanuzi zaidi.
• Yesu aliwashangaa kwa kuzingatia walichokizoea zaidi kuliko kuisikiliza sauti yake na kuelewa ukweli wa neno la Mungu kama ilivyo kwetu sasa watu wengi kutokana na mazoea ya maishahawasikilizi Mungu anawata kufanya nini.

3. MATOKEO MAZURI AU MABAYA YA MAISHA YA MTU YANATOKA MOYONI
• Moyo wa mwanadamu ndio unaoleta matokeo ya aina zote ya mwanadamu, yawe mazuri au mabaya. (mithali 4:23)
• Moyo ukiathiriwa na dhambi ndiko ambapo mabaya yote hutokea (Mhubiri 9:3, Yer 17:9) na huwa mwanzo wa maovu yote (Mk 7: 20 – 23)

HITIMISHO
Wote tunapaswa kuelekeza macho yetu na umakini wetu wote katika mioyo yetu na kuilinda isiingiliwe na dhambi na kusababisha sisi kuwa waasi mbele za Mungu. ( Efeso 4:17 – 24, 1Petro 4: 1-3,) Haya yote yanawezekana ikiwa tutakuwa watii kwa neno la Mungu wakati wote na kujifunza kwa Mungu ( Mdo 2:28, 22: 16)
Kwa akili zetu ni Ngumu ila neema ya Mungu iliyokuu sana Kwetu inatuwezesha kufanya yote.
AMEN

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *