MAHUBIRI YA SIKU YA BWANA YA 8 BAADA YA UTATU

Somo:UCHAGUZI WA BUSARA

Masomo:
Zaburi 37:1-8
Marko 1:40-45
Mathayo8:11-13

UTANGULIZI
✏ Siku ya leo tunajifunza juu ya uchaguzi wa busara natumepewa injili mbili Marko 1:40-45; Mathayo 8:11-13. Uchaguzi ni kitendo chaku angalia ama kuoanisha kipi kinafaa ama kipihakifai.
✏Busara ni hekima au maamuzi sahihi
✏Sasa UCHAGUZI WA BUSARA maana yake ni kitendo cha kuangalia kipi kinafaa tena kwahekima.Maana unaweza ukachagua nakuona kinafaa lakini ukakosa hekima kwenye uchaguzi wako bado utakiacha kinacho faa zaidi kuliko hicho ulicho kichagua.Katika injili mbili za leo pamoja na zaburi tunajifunza mambo yafuatayo kutokana na kichwa hichi cha UCHAGUZI WA BUSARA;
1.HEKIMA KATIKA UCHAGUZI NI MWANZO WA MAFANIKIO
✏ Unaposoma injili ya Marko1:40-45 tunamwona mtu mwenye ukoma alimwendea Yesu akisema “Ukitaka, waweza kunitakasa” kwakauli hiyo alitumia hekima ya hali ya juu kumwomba Yesu amtakase kwamba kama Yesu mapenzi yake nikumuona mzima bas amtakase kama simapenzi yake amuache
✏Sisi kanisa la leo kuna mambo yanahitaji uchaguzi wenye hekima ndani yake ilituweze kufanikiwa kwa mfano unapomchagua kristo kuwa Bwana na mwokozi wa maisha yako tambua huyo Bwana hataki mtu mzembe FANYA KAZI KWA BIDII
✏Lakini pia familia yenye mafanikio huatanguliwa na hekima ndani yao baba akiwa naheshima kwa mama na watoto watafanya hivo kwasababu baba amechagua fungu jema nala baraka

2.MATAIFA WATATUTANGULIA KUINGIA MBINGUNI KABLA YETA SISI TULIO OKOKA.
✏Biblia inasema katika Mathayo 8:12″bali wana wa ufalme watatupwa katika giza la nje, ndiko kutakuwako kilio na kusaga meno”
✏Yesu ananza kwakusema watakuja watu kutoka mashariki na magharibi kaskazini na kusini watakuja kuketi kwa ibarahim,isaka,na Yakobo maana yake walioamini nawasio amini wote wataenda mbio kila moja njia yake lakini wale waliowagiza(wana waufalme mathayo8:13) ndio anasema watatupwa nje katika ufalme wagiza sasa kwanini tulioamini tutatupwa nje ni kwasababu ndani yetu wengi tumemchagua kristo lakini tunashwindwa kwend sawasawa na kanuni zake wengi tumekuwa wasengenyaji na mambo mengi laini mataifa wengine hawasali lakini wanajikita katika kutenda mema nandio maana tusipo kaasawa watatuzidi hata sisi
✏Ndugu zangu nawasihi tufanye kazi ya Mungu kungalibado mchana tuachague natufanye maamuzi saa hii wasitushinde wasio amini sisi tunanguvu zaidi yao.
3.NJIA ZETU NA MIPANGO YETU TUNAPASWA KUMKABIDHI BWANA
✏Mwimba zaburi anatuambia katika zaburi 37; 5 “Umkabidhi Bwana njia yako, Pia umtumaini, naye atafanya”
✏Kumbe sisi tunaomwamini kristo tunatakiwa kumchagua Kristo kuwa kiongozi wa mipango yetu nanirahisi tu nikukabidhi na kutumaini( kutarajiA au kuwa naimani) naye nilizima afanye tu sasa sasa kwanini watu wengi tunamkabidhi lakini hafanyi kwasababu;
✏Tumekuwa tunaishi maisha ya changanya changanya hatujachagua ninani wakusimamia mipango hiyo ingawaje wengine wanaileta kanisani lakini wakitoka wanaenda kwa waganga nandiomaana haifanikiwi kumbe sisi tulio amini tunapaswa kukabidhi na kuamini au kutumaini tu mwisho tusiongeze mengine yasiyo na mantiki
✏Tuanaambiwa kitarajiwacho kikikaiwa moyo huugua ni kwamba Unapo mkabidhi Bwana mipango yako tambua kuwa anafanya kwa mapenzi yake hapelekeshwi na yeyote hivyo jenga moyo wa UVUMILIVU
4.RIDHIKA NA HALI ULIYO NAYO
✏Ukisoma Zaburi 37:6 ” Ataitokeza haki yako kama nuru, Na hukumu yako kama adhuhuri”
✏Unajua mda wingine Mungu huwa anakuweka kwenye zone(sehemu) furani ili ujifunze sasa watu wengi tunapokuwa kwenye eneo hili huwa tunachagua hukumu mfano anapitishwa kwenye gumu fulani imani inashuka kanisani haendi anaacha kabisa kumbe swala ni kumuamini tu yeye ataitokeaza haki yako kama nuru
✏Mungu anatabia ya kujitukuza katika ya pito unalopitia hivyo mpendwa unapopitishwa kwenye gumu ama pito fanya uchaguzi wa busara usikurupuke maana anasema”Ataitokeza haki yako kama nuru,……”
MWISHO
✏Wito wangu kwenu naombeni mfanye maamuzi sahihi siku ya leo kama neno la Mungu linavyosema katika Joshua 24:15 “inasema chagueni hivemaeo mtakaye mtukatika”
AMEN.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *