MAHUBIRI YA SIKU YA 10 BAADA YA UTATU

SOMO: LUKA 19: 41  – 44

UTANGULIZI
• Mungu ametupa kibali kukumbushana kuwa HAKI HUINUA TAIFA BALI DHAMBI NI AIBU KW WATU WOWOTE, msemo huu ni hakika hebu tuangalie mistari hii “kwa hiyo, kama kwa mtu mmoja, dhambi iliiingia ulimwenguni, na kwa dhambi hiyo mauti; na hivyo mauti ikawafikia watu wote kwa sababu wote wamefanya dhambi” (Warumi 5:12)

• Dhambi ya mtu mmoja ilitufanya watu wote tuwe wadhambi ndio maana jamani hiii kitu dhambi ni aibu kwa watu wowote wanaojihususha nayo. Zaidi hebu tuone na hii “Basi tena, kama kwa kosa moja, watu wote walihukumiwa adhabu, kadhalika kwa tendo moja la haki watu wote walihesabiwa haki yenye uzima kwa sababu kama kwa kuasi kwake mtm mmoja watu wengi waliingizwa katika hali ya wenye dhambi kadhalika kwa kutii kwake mmoja watu wengi wameingizwa katika hali ya haki”(Rumi 5: 18 – 19)

• Wewe ukitenda haki taifa zima linapata kuinuliwa kwa haki uliyoitenda. Kila mmoja ajitahidi kuhakikisha taifa lake linainuliwa.

• Kwa mwaka huu kanisa letu linatukumbusha kwa kupitia injili iliyoandikwa na Luka kuwa ili uweze kuliinua taifa lako unapaswa KUZITAMBUA SIKU

• Kisa hiki ni cha Yesu akiingia Yerusalemu kwa shangwe yeye aliulilia mji wa Yerusalemu kwa kutokufahamu siku na muda wake wa kujiliwa. Katika kisa hiki tunajifunza

1. MUNGU ANAHUZUNIKA KWA WEWE KUTOKUZINGATIA MUDA WAKO
• Yesu anapoukaribia Mji anaulilia na kusikitika kwa wao kutokutambua kuwa kwa kuja kwake walipaswa kwenda kumpokea kwa furaha kwa sababu kwa kuja kwake ilikuwa ndio ukobozi wa Israel.

• Siku ya kujiliwa ni siku ya kufurahi, kuabudu, kusifu na ni siku ya amani kwa watu wote.

• Kwa nini watu hawaoni wala kutambua umuhimu wa siku ya Mungu.

a. Kwa sababu wanaongozwa na viongozi vipofu ambao hawaoni yatakayotokea mbeleni.

b. Wengine hawaoni sababu ya nafasi walizonazo, kama vile cheo, mal ink

c. Wengine wamekosa kuiona siku ya Mungu kwa sababu ya kujiinua na kujiona wao wanathamani kuliko kumuabudu Mungu

• Hata sasa wapo watu hawatambui nguvu za Mungu wala hawaoni umuhimu wa kuhudhuria ibada, jumuiya na matukio ya kiibada kwa mojawapo ya sababu nilizozitaja hapo juu, viongozi wengine wamewafanya watu kuwaona wao na kuwaabudu wao kuliko Mungu.

2. IPO HASARA KUBWA KWA WALE WALIO MBALI NA MUNGU
• Kwa wa Israel kutokutambua nyakati kwa sababu mbalimbali Yesu anaona mabaya juu ya mji wao wa Yerusalemu kuwa

a. Hekalu litabomolewa
b. Mji wa Yerusalem kuharibiwa na uzuri wake kupoea
c. Maadui zake watatawala juu ya Yerusalemu

• Hayo yote yanatokea kwa sababu tu wameshindwa kutambua wakati wa kujiliwa kwao. Kutambua na kuheshimu uwepo wa Mungu utakuepusha na matatizo mengi.

• Tujitahidi kwa wingi kuhakikisha kuwa Mungu anakuwa pamoja nasi wakati wote. Tukiutambua wakati amani itatulia juu ya maisha yetu na juu ya familia na taifa letu kwa ujuma.

HITIMISHO
• Yesu akiwa ndani yetu, akawa kiongozi wetu kwa neema yake atatuwezesha kutenda haki kwa ajili yetu na kwa ajili ya taifa letu.

• Kutenda dhambi sio tu kunamchukiza Mungu na kutupati mauti bali pia inasababisha taifa kuwa katika mabaya na machukizo mbele ya Mungu.

• Tujitahidi wote kutenda haki kwa neema ya Mungu ili baraka zake zidumu nasi milele na aweze kututahadharisha juu ya kesho yetu.

AMEN
Ev.john

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *