WAJIBU WAKO

UNAWAJIBIKA NA MAISHA YAKO MWENYEWE. “Maana kila mtu atalichukua furushi lake mwenyewe.” (Wagalatia 6:5) “Basi ni hivyo, kila mtu miongoni mwetu atatoa habari/hesabu zake mwenyewe mbele za Mungu.” (Warumi 14:12) “Roho itendayo dhambi, ndiyo itakayokufa; mwana hatauchukua uovu wa baba yake, wala baba hatauchukua uovu wa mwanawe, haki yake mwenye haki itakuwa juu yake, na uovu wake mwenye uovu utakuwa juu yake.”
(Ezekieli 18:20)

Kwa msisitizo wa kipekee kabisa maandiko haya yanatuonesha kwamba kila mtu anawajibika na maisha yake mwenyewe. Hata mbele za Mungu hakuna atakaye hukumiwa kwa dhambi za mtu mwingine. Kwa maana hiyo hiyo basi hakuna anayewajibika na maisha ya mtu mwingine. Kwa mujibu wa maandiko haya ni makosa makubwa kuwa na MAWAZO TEGEMEZI, AKILI TEGEMEZI. Ile dhana ya KULAUMU WATU KWA SABABU HAWAJAKUSAIDIA inakemewa vikali na maandiko haya.
Simama upiganie maisha yako mwenyewe sio lazima watu wakusaidie hata kama uwezo wanao. Jukumu la kwanza la Baba yako ni kwa mke wake. Wewe ukishafika Miaka 18 unapaswa kuwaza kesho yako itakuwaje. Jukumu kubwa la Kaka na Dada zako ni maisha yao na watoto wao. Wewe sio jukumu lao. Acha kulaumu watu na usimame kutengeneza maisha yako mwenyewe.

Kama unataka kufunga Ndoa fanya unachomudu, usijiwekee bajeti kubwa kwa kuangalia mifuko ya watu. Kama hauna fedha achana na kusherekea Birthday, kunywa maji mshukuru Mungu. Kama umekosa kodi kalale kanisani saidiana na mlinzi ukiumwa mbu utapata akili ya kutafuta hela. Lakini usiwe mzigo kwa mtu yeyote na kulaumu na kuchukia watu. “Oh hawanisadii chochote!” Nani alikwambia unapaswa kusaidiwa!? KASIRIKA, CHUKIA, NUNA LAKINI UJUMBE NDIO UMEUPATA, PIGANIA MAISHA YAKO. KAMA AMBAVYO UTAHUKUMIWA KWA DHAMBI ZAKO MWENYEWE BASI VIVYO HIVYO AMUA KUFANIKIWA KWA JASHO LAKO MWENYEWE. -evjohn whatsup 0767386606
#2020