Category Archives: Uncategorized

MUHTASARI WA MAHUBIRI YA LEO 19/07/2020

Somo:HURUMA YA MUNGU

MASOMO
zaburi1:1-69
2Wakoritho7:5-10
Mathayo9:1-8*
UTANGULIZI
▶Jumapili ya leo tunajifunza juu ya huruma ya Mungu kwa wanadamu
▶Katika tafakari hii ya huruma za Mungu tumepewa kutoka injili ya mathayo9:1-8, ambapo tunamwona Yesu akiwa anaponya na kupoza wagonjwa ambapo kila alieponywa aliambiwa “umesamehewa dhambi zako” chukua godoro lako na uende zako
▶Kitendo hicho cha kusema “umesamehewa dhambi” zako kiliwaudhi mafarisayo wakaanza kusemezana wao kwa wao huyu ninani hata asamehe dhambi lakini wasitambue nini wana kisema.
▶Mafarisayo waliendelea kusemezana wao kwawao nanafsi zao kwamba Yesu anakufuru(anaasi) kusema kwa mgonjwa amesamehewa dhambi hii ili kuwa nikutotambua mamlaka ya Yesu duniani ama Kristu ninani.
▶Kupitia kisa hiki cha Mathayo9:1-8Tunajifunza mambo yafuatayo juu ya huruma ya Mungu

1.MATESO NA MASUMBUFU TUNAYOPITIA WAKRISTO NI KUTOKANA NA DHAMBI
▶Ndugu zanguni Wakristo Mungu anasema amejaa huruma na neema nyingi lakini utashangaa wakristo wengi wanapita katika magumu nikutokana na dhambi. Ukitaka kuishi maisha ya raha tunza Utakatifu wako.
▶ Kuna wakati unajikuta unapita kwenye majaribu mazito sana kumbe nikutokana na dhambi kumbe dawa ya kuishi maisha ya raha ni kukimbilia huruma za kristo Yesu
▶Tunamwona mwanamke aliopooza aliambiwa umesamehewa dhambi zake .

2.MAGONJWA MENGI HULETWA NA DHAMBI
▶Ukiangalia dunia ya sasa inakabiriwa na magonjwa mazito mfano ukimwi kama tutamua kufuata kanuni nasheria ambazo Mungu ameagiza hakika hatutoweza kupigwa na magonjwa ya ajabu
▶lakini kwa huruma yake anasema “atatuponya magonjwa yetu yote na ataukomboa uhai wetu na kaburi” kumbe hata kama tumemtenda dhambi Tuombe toba ili huruma yake iendelee kutembea nasi.

3.TUNATAKIWA KUTAFAKARI MASHAURI YETU MBELE ZA MUNGU
▶Wakati Yesu anaponya wagonjwa mafarisayo walianza kusema inakuaje anasamehe dhambi hili lili kuwa nishauri ambilo kwao waliona ni kufuru.
▶Wakristo wa leo ili kuikimbikia huruma ya Bwana tunatakiwa kulifuata shauri la Bwana tutakuwa salama maana ndimo huruma ya kristo hutembea kuwahudumia walio wake.(Zaburi1:1-6)

4.MUNGU PEKEE NDIO MFARIJI WA KWELI
▶Ndugu zangu washarika tunatakiwa tutambue kuwa Yesu kristo ndio mfariji pekee ama chaguo la kwanza la kukimbilia wengine huenda kutafuta faraja kwa wagaga,marafiki,na watu wengine lakini faraja yao ni ya mda tu kimbia sasa mbio mbele za kristo akufute machozi.2Wakoritho7:5-10
▶Nandiomaana anasema njooni kwangu msumbukao na kulemewa na mizigo nami nitawapumzusha.

MWISHO
▶Siku ya leo tunaitwa na huruma hii katika Isaya 1:18 ya kwamba twende tukasemezane naye iliatubadirishe na kututengeneza haijalishi mwanzo wetu ulikuwaje
KUMBUKA:Mabadiriko huanzia ndani ya Moyo wako
▶Mungu anisaidie na akusaidie ili tuweze kutambua huruma yake maishani mwetu.
AMEN.

MUHTASARI WA MAHUBIRI YA LEO 12/07/2020

SOMO: UFUASI NA UANAFUNZI

Yohana 6:66-71
Yeremia 1:17-19

UTANGULIZI
 Jumapili ya leo tunajifunza juu ya Ufuasi na Uanafaunzi
 UFUASI ni hali ya kufuata itikadi, mwenendo au kitu Fulani
 UANAFUNZI ni hali ya kuwa katika mafunzo
 Kwa maelezo haya mtu huwezi kuwa mwanafunzi kabla kuwa mfuasi, sababu lazima uwe na itikadi ambayo unataka kujifunza ili uweze kuwa mwanafunzi
 Mkristo ni mtu aliyekubali kumfuata Yesu Kristo na Yesu anamfanya kuwa mwanafunzi wake ili aweze kujifunza kwake(Yesu) ( Luka 9:62)
 Somo ambalo tunatafakari leo juu ya mada hii ni kutoka Yeremia 1:17 – 19
 Nabii Yeremia ni mfuasi na mwanafunzi wa Yesu ambapo katika mistari hii Mungu Mungu anamwambia Yeremia pamoja na sisi jinsi ya kuwa mfuasi na mwanafunzi mzuri kwake.

1. UFUASI NA UANAFUNZI UNAHITAJI UTII NA UAMINIFU
 Mtumishi mwaminifu wa Mungu anakuwa mtii kwa yote anayoelezwa na Mungu. Mtumishi asiyemwaminifu Mungu anasema mtu wa namna hiyoa ataadhibiwa sana
 Mungu anatutaka tuifanye kazi yake kama alivyotupa wito tulipokubali kuwa wafuasi na wanafunzi wake.

2. UFUASI NA UANAFUZNI UNAHITAJI UVUMILIVU NA USTAHIMILIVU
 Mkristo anao uwezo wa kukabiliana na changamoto zote anazokabiliana nazo kwa kulifahamu neno la Mungu (Mt 4: 1 – 11)
 Wanaokuchukia wasikuyumbishe wala kukurudisha nyuma katika ufuasu na uanafunzi wako kwa sababu ni wale ambao wanapinga kweli ya neno la Mungu ( Yn 15:18 – 25)
 Pamoja na upinzani wote mfuasi na mwanafunzi wa Yesu anapaswa kusimamia neno la Mungu katika uaminifu na utakatifu wake huku akilisema neno la Mungu bila upendeleo wowote.

3. UFUASI NA UANAFUZNI UNAHITAJI KUTOKUYUMBISHWA.
 Majaribu na vikwazo ni sehemu ya utumishi wetu, hivyo tusiogope maana Mungu yu pamoja nasi ( Yer 37:16, Yer 38:6)
 Mtumishi anayemtii Mungu lazima atashinda pamoja na changamoto zote atakazokutana nazo ( Rum 8:35 – 39)

HITIMISHO
 Mungu alikuja kwa watu wake na wote waliompokea aliwapa uwezo wa kufanyika watoto wake na hao ndio wale waliaminio jina lake.
 Mungu atusaidie ili tuwe wafuasi na wanafunzi waaminifu kwa Mungu wetu na tufanyike watoto wake.
AMEN.

MUHTASARI WA MAHUBIRI YA LEO TAREHE 05/07/2020 SIKU KUU YA VIJANA

MASOMO
Zaburi 37:25-40
1samwel 17:38-45
Mathayo 11:25

Wazo la wiki:NGUVU YA VIJANA KATIKA KANISA
____________________________

Somo:MAISHA YA USHINDI YA KIJANA MKRISTO

Fungu:1 YOHANA 2: 12 – 17

UTANGULIZI
• Jumapili ya Leo Tunajifunza maisha ya ushindi ya kijana Mkristo. Yohana ambaye alianza huduma ya uanafunzi wa Yesu akiwa na umri mdogo tu wa miaka 16 na sasa amekuwa mzee na anawaandikia wakristo wote akiwapa ushauri jinsi ya kuendenda kwenye ulimwengu huu huku wakihakikisha kuwa wanaupata ufalme wa Mungu.

• Katika mistari hii tuliyoisoma katika waraka huu Yohana anawagawanya wasomaji wake katika makundi matatu

TOBA NI MWANZO WA ULINZI WA MUNGU KATIKA MAISHA YETU.
• Kundi la kwanza ni watoto ambao wao ndio wameupokea ukristo anawaambia kuwa safari yao ya Ukristo inaanza na msamaha wa dhambi na anawahakikishia kuwa uhusiano wao na Mungu umerudishwa kama uhusiano wa baba na mtoto.

• Kundi la pili na la kina baba, hawa ni wakristo wa muda mrefu anawaonyesha uhuhimu wa kuwa na kumbukumbu katika maisha yao na kujua kuwa hata kama wana uzoefu wa Kiroho namna gani huwezi kumshinda Mungu bado unapaswa kuendelea kumtegemea wakati wote.

• Kundi la tatu ni vijana, anazungumza na kundi hili akilionyesha kuwa lina nguvu, limekuwa na uwezo wa kumshinda shetani na neno la Mungu linakaa kwa wingi ndani yao.

• Sifa hizi ni sifa za kundi hili la vijana, kuwa wana nguvu, neno la Mungu linakaa ndani yao na limewawezesha kumshinda yule mwovu.

• Analiambia kundi hili kuwa mapambano yapo katika maisha yao ila uwezekano wa kushinda upo sababu wapo kwenye nafasi nzuri ya kushinda.

• Neno la Mungu lililopo kwa wingi ndani yao ni chanzo chema cha hekima ya kujua jinsi ya kumpinga yule mwovu. ( Lk 4:1 – 13, Mt 4:1 – 11)

• Makundi yote haya matatu Yohana anayataka, kwanza, yanapaswa kupendana na pili yanapaswa kuchukia mambo ya giza ambayo anayaita mambo ya dunia na anatutaka tujitenge mbali na dunia kwa sababu hatuwezi kupenda dunia na Mungu ( 1Yoh 2:15, Mt 6:24)

a. Ni Dunia gani anayoizungumzia Yohana?
b. Dunia hii ni ya aina gani?
c. Dunia hii ina sifa hani?
d. Je, tunaweza vipi kuishinda dunia hii?

NI DUNIA GANI ANAYOIZUNGUMZIA YOHANA?
• Yohana hazungumzii dunia hii iliyoumbwa na Mungu ( Mdo 17:24) wala kuhusu dunia ya utu wa mtu ( Yn 3:16)

• Dunia anayoitaja Yohana inatokana na neno Kosmos lenye maana ya utaratibu au mpango wa mfumo wa utaratibu wa mwanadamu

• Dunia hii ni mfumo wa mawazo na matendo yanayomhusu mtu katika jambo Fulani. MF. Juma yupo kwenye dunia ya siasa, maana yake Juma anajishughulisha na siasa zaidi.

• Dunia hii ni maisha na mpango wa mwanadamu vinavyotengenezwa bila kumkali Mungu na mapenzi yake na katika hali hiyo ni chini ya shetani

DUNIA HII NI YA AINA GANI?
• Dunia hii na tamaa zake zitapita sio za milele na yule anayeitegemea pia hatadumu (1Yoh 2:17) na hata kama mtu huyo anaonyesha kushinda sasa ila mwisho wake utafika ( Uf 20:7 – 10, uf 21:1- 4)

• Dunia hii inamshambulia mwanadamu katika ukamilifu wake ( 1Thes 5:23) Kiroho, kimwili na kisaikolojia. Anatushambulia kiroho ili tusimpende Mungu, kimwili ili tusiweze kuishi kwa ajili ya Mungu na kisaikolojia ili tushindwe kujifunza kwa Mungu. Mfano wakati wa anguko. ( Mwa 3)

a. Hawa aliona mti unapendeza macho na kumuondoa katika kumpenda Mungu(mashambulizi ya rohoni)
b. Mti Watamanika kwa Maarifa, hapo shetani anamuondoa Hawa katika kujifunza kwa Mungu( mashambulizi ya kisaikolojia)
c. Wafaa kwa chakula anamuondoa Hawa katika maisha ya kuishi kwa ajili ya Mungu na kumtegemea yeye (mashambulizi ya Kimwili)

DUNIA HII INA SIFA GANI?
Biblia inatueleza wazi sifa za Dunia hii
a) Dunia ya namna hii ina kiongozi wake ambaye ni shetani ( 2Kor 4:14, Yn 12:31)
b) Ni dunia ya uovu ( 1Yoh 5:19)
c) Dunia hii ina watoto wake ( Lk 16:8)
d) Dunia hii ina hekima yake yenyewe ( 1Kor 2:6)
e) Dunia hii ni chafu ( 2Pet 1:4)
f) Dunia hii ndio iliyomsulubisha Yesu ( 1Kor 2:8)

TUNAWEZAJE KUSHINDA DUNIA HII?
Ili kuwaeza kuishida dunia hii lazima upambane nayo kimwili, Kiroho na kisaikolojia (nafsi)
a) Njia ya kushinda ulimwengu huu kimwili ni kujitenga na dhambi(1Thes 5:22) Ruhusu hamu yako ya kuishi kwa ajili ya Mungu iongoze njia na kazi zako
b) Ili uweze kuishinda dunia hii kisaikolojia ( 1 Yoh 5:4b) Ruhusu hamu ya kujifunza kwa Mungu ikuze ufahamu wako na uelewa wako
c) Ili uweze kupambana Kiroho ni kujisalimisha kwa Mungu ( Yak 4:7) Ruhusu hamu ya kumpenda Mungu iongoze maamuzi yako.

HITIMISHO
• Tunapaswa kujua kuwa ulimwengu unapita ila Mungu atadumu nasi milele ( 1 Tim 6: 11 – 12)

MAHUBIRI YA JUMAPILI TAREHE 28/06/2020

Somo:NEEMA YA MUNGU ITUOKOAYO
Masomo:
Zaburi 59:1-9
Matendo 11:1-15
*Luka 8:26-39

SHABAHA: Wasikilizaji waweze kuelewa kuwa ili kupata ahadi za Mungu tunapaswa kumtegemea Mungu.

“Kwa kuwa mwana wa Adamu alikuja kutafuta na kuokoa kile kilichopotea” (Lk 19:10)

UTANGULIZI: Leo ikiwa ni siku ya tatu baada ya utatu tunaangalia mada izungumzayo juu ya Neema ya Mungu ambayo inatuwezesha sisi kuupata wokovu.

> Neema maana yake ni mafanikio aliyonayo mtu kutokana na majaaliwa ya mwenyezi Mungu au kwa juhudi zake mwenyewe.

> Hivyo:- tunaweza kusema kuwa leo tunazungumzia juu ya mafanikio aliyonayo mtu kutoka kwa mwenyezi Mungu ambayo yanaleta wokovu katika maisha ya mtu.

> Katika kutafakari Neema hii ya Mungu iletayo wokovu tumepewa kisa kutoka katika biblia Luka 8:26 – 39. Kisa hiki ambacho kimeelezwa hapa pia kimeelezwa katika kitabu cha mathayo 8:28-34 na kitabu cha Marko 5:1-20 ikizungumza habari ya mtu aliyepagawa na pepo wachafu ambao wamejitambulisha kwa jina la Legion maana yake ni jeshi kubwa la warumi lenye nguvu lililokwa na idadi ya wanajeshi 6000.

Katika kisa hiki unajifunza mambo yafuatayo:-

SHETANI NI MHARIBIFU

Mtu huyu ambaye amepagawa nna pepo tunaambiwa kuwa alikuwa Uchi, aliishi makaburini, na alikuwa akijikatakata na mawe (Marko 5:3) Shetani anapoingia kwetu hahurumii hata miilil yetu atatutaabisha na kuwa wahitaji wakati wote.

ULINZI WA KIBINADAMU HAUJITOSHELEZI

Mtu huyu alifungwa kwa pingu na hata kwa minyororo ila aliikata yote na wanadamu wakakata tama nay eye na kumuacha alivyo. Unaweza kutegemea wanadamu wanaweza kukusaidia ila ni kwa kitambo kidogo na utabaki katika shida yako.

BINADAMU WENGI WANAANGALIA KITU KULIKO UTU

Tunaelezwa kuwa baada ya mtu huyu kuponywa watu wa mji ule walimfukuza Yesu kwa sababu walipiga hesabu ya hasara ya nguruwe 2000 waliofia majini waliona mwenzao amepata hasara kubwa sasa hawakujua nani angefuata wakaogopasana wakaamua kumwambia aondoke kwao.

MUNGU ANAJISHUGHULISHA NA MAHITAJI YETU

Yesu alivyoona kuwa mtu huyu yupo uchi, anaishi makaburini mbali na watu na alikuwa akijikata mwili kwa mawe alijua kuwa anahitaji msaada hivyo aliona nguruwe hawana umuhimu kama mtu wake akayaelekeza mapepo kwa nguruwe na kumponya yule kijana. Mapepo yalikwepa kwenda kuzimu yakidani kuwa yakiingia kwa nguruwe yatakuwa salama ila baada ya kuingia nguruwe walikufa wote na mapepo bado yakaenda kuzimu.

UKIMKUBALI MUNGU UTAKUWA SALAMA

Baada ya mtu huyu kuponywa alitulia chini ya miguu ya Mungu akiwa amevaa nguo na akiwa na akili yake timamu. Amani ya kweli inapatikana kwa kumkubali Yesu

MEMA ANAYOKUTENDEA MUNGU ANATAKA UMTUMIKIE

Mtu aliyeponywa alitaka kandamana na Yesu ila yesu alimwambia aende kuelezea habari njema za Yesu kwa watu wa nyumbani kwake kwa kuwa eneo lile liikuwa ni eneoo la wapagani nao waone wema wake. Baraka tunazopata tunatumwa tukahubiri.

HITIMISHO

Bora kuwa mlinzi wa getini kwa Mungu kuliko kuwa mfalme au malkia nje ya Mungu sababu huko hakuna mafanikio ya kweli, mafanikio ya kweli yaletayo wokovu yanapatikana kwa Mungu tu.

MUHTASARI WA MAHUBIRI YA LEO TAREHE 21/06/2020

siku ya 2 baada ya utatu

SOMO: TUKAE PAMOJA KWA UMOJA
MASOMO Yohana17:20-21
?Efeso 5:8-14
? Zaburi 133

UTANGULIZI
• Jumapili ya Leo ni sikukuu kubwa ya KKKT, tuanze mafundisho yetu ya leo kwa kumtakia ndugu yako heri ya siku kuu.
• Leo ni jumapili ambayo tunaazimisha kuunganika kwa makanisa saba ya Kilutheri Tanganyika ambayo ni:-
a) Kanisa la kiinjili la Kilutheri la Iraqw
b) Kanisa la Kiinjili la Kilutheri la kaskazini mwa Tanganyika
c) Kanisa la Kiinjili la Kilutheri la Kaskazini Magharibi mwa Tanganyika
d) Kanisa la Kiinjili la Kilutheri la Kati mwa Tanganyika
e) Kanisa la kiinjili la Kilutheri la Kusini mwa Tanganyika
f) Kanisa la Kiinjili la Kilutheri la Usambara Digo
g) Kanisa la Kiinjili la Kilutheri la Uzaramoni – Uluguru

• Makanisa haya saba yalipoungana yalikwa na washarika laki tatu (300,000) tarehe 19/06/1963 hadi kufikia leo hii kanisa moja la Kilutheri lina zaidi ya dayosisi 25 na waumini zaidi ya milioni sita. (6,000,000)
• Siku ya leo tunaadhimisha miaka mia moja na thelathini (133) ya ulutheri Tanzania.
• Mwaka huu neno linalosindikiza sikukuu hii ni kutoka YOHANA 17;20-21 ambalo linaendelea kukaza juu ya umoja katika kanisa.
• Mlango huu wa 17 ni mlango wenye sala ya Yesu, kwanza anaanza kwa kujiombea yeye mwenyewe, kisha anawaombewa wanafunzi wake na anahitimisha kwa kuwaombea waumini wote wawe na umoja.
• Kipengele tulichosoma kinatufundisha mambo kadhaa

1. YESU NDIE MWANZILISHI WA KANISA
• Aliwaita wanafunzi na kuwaandaa kwa kazi maalumu ya kulihubiri neno lake ( Marko 3:14)
• Aliwaandaa kuifanya kazi aliyokuwa anaifanya yeye mwenyewe
• Aliwataka wawe na umoja ili waweze kuwa na lengo moja
• Maswali ya kujiuliza sisi wenyewe
a) Wewe umeandaa watu wa kufanya kazi ambayo unaifanya?
b) Je, wewe katika kazi/ huduma unayoifanya unazingatia umoja? Au unatengeneza makundi?

2. LENGO LA YESU NI KUONA KANISA MOJA
• Mungu anawataka waumini wote wawe na umoja na kuweka tofauti zao pembeni(Yesu anajua kuwa tunazo tofauti ila tukubali kuziweka pembeni na kuwa na umoja katika lengo moja)
• Umoja huu anataka ufanane na umoja wa Mungu na Yesu yaani umoja usio wa Kinafiki, umoja ambao hauwezi kutenganishwa. ( Umoja wetu katika utofauti wetu ufanye hata watu kushangaa tumeweza vipi kuwa wamoja)
• Umoja huu uwe ni umoja uliofungwa katika upendo wa kweli ( Yohana 13:34 – 35)
• Swali la kujiuliza waumini wale wanaojitenga na ibada kama vile kutokuwa kundini na kuanzisha madhehebu mengine bado Yesu anawahesabu kama wanafunzi wake? Wengine hata kukwepa majukumu ya kazi za umoja kama vile sadaka za umoja nk ni wafuasi wa Yesu Kweli?

3. UMOJA WA KIKRISTO UWE UMOJA WENYE MALENGO
• Umoja huu unapaswa uwe umoja unaoendelea kukua kama tulivyoona historia ya kanisa letu.
• Umoja huu uwe ni umoja wenye imani moja
• Umoja huu uwe ni umoja unaoendeleza utukufu wa Mungu ulimwenguni kote.
• Umoja unaosogeza waumini wote kuwa familia moja, kijiji kimoja. Tukitambua kuwa Yesu ndie mwanzilishi wa utandawazi ( Matayo 28:19 – 20, Mdo 1:8)
• Kanisa la Kiinjili la Kilutheri kwa kutambua kwamba misioni ya Bwana Yesu inaendelea kukua na kupanuka imeendelea kujitahidi kuleta umoja kwa kuweka uwiano wa sadaka za umoja ili kukidhi hitaji hili ambazo zinafanya kazi ya:-
a) Kutuma wachungaji maeneo ya misioni ya ndani na nje ya nchi
b) Kuhisani masomo ya wanafunzi wanaotoka maeneo ya misioni
c) Kuendesha vituo vya kazi za umoja kama vile Ofisi kuu ya kanisa, Shule ya viziwi mwanga na Njombe, Radio sauti ya injili, Seminari ndogo ya Morogoro nk.
Mimi na wewe tumeshiriki vipi katika misioni hii ya Yesu?

HITIMISHO
• Roho mtakatifu atusaidie kutambua kusudi la Yesu kwa kanisa lake nasi kama wafuasi wa kweli tuungane kwa upendo kuliendeleaza kanisa la Mungu.
• Umoja ni silaha kubwa sana katika huduma yetu ya uinjilisti. Ubora wa ushirikiano wetu unawavuta watu wengi kwa Mungu na udhaifu wa umoja wetu unalitawanya kundi la Mungu na kulipoteza huku ushuhuda wetu ukiendelea kuwa dhaifu
• Tuwavute watu kwa Mungu kwa kudumisha umoja miongoni mwetu.
AMEN.