All posts by Evangelist John(Charles)

Usharika wa uwemba wa kanisa la kiinjili la kilutheri Tanzania dayosis ya kusini karibu mbarikiwe pamoja nasi

MAHUBIRI YA SIKU YA 10 BAADA YA UTATU

SOMO: LUKA 19: 41  – 44

UTANGULIZI
• Mungu ametupa kibali kukumbushana kuwa HAKI HUINUA TAIFA BALI DHAMBI NI AIBU KW WATU WOWOTE, msemo huu ni hakika hebu tuangalie mistari hii “kwa hiyo, kama kwa mtu mmoja, dhambi iliiingia ulimwenguni, na kwa dhambi hiyo mauti; na hivyo mauti ikawafikia watu wote kwa sababu wote wamefanya dhambi” (Warumi 5:12)

• Dhambi ya mtu mmoja ilitufanya watu wote tuwe wadhambi ndio maana jamani hiii kitu dhambi ni aibu kwa watu wowote wanaojihususha nayo. Zaidi hebu tuone na hii “Basi tena, kama kwa kosa moja, watu wote walihukumiwa adhabu, kadhalika kwa tendo moja la haki watu wote walihesabiwa haki yenye uzima kwa sababu kama kwa kuasi kwake mtm mmoja watu wengi waliingizwa katika hali ya wenye dhambi kadhalika kwa kutii kwake mmoja watu wengi wameingizwa katika hali ya haki”(Rumi 5: 18 – 19)

• Wewe ukitenda haki taifa zima linapata kuinuliwa kwa haki uliyoitenda. Kila mmoja ajitahidi kuhakikisha taifa lake linainuliwa.

• Kwa mwaka huu kanisa letu linatukumbusha kwa kupitia injili iliyoandikwa na Luka kuwa ili uweze kuliinua taifa lako unapaswa KUZITAMBUA SIKU

• Kisa hiki ni cha Yesu akiingia Yerusalemu kwa shangwe yeye aliulilia mji wa Yerusalemu kwa kutokufahamu siku na muda wake wa kujiliwa. Katika kisa hiki tunajifunza

1. MUNGU ANAHUZUNIKA KWA WEWE KUTOKUZINGATIA MUDA WAKO
• Yesu anapoukaribia Mji anaulilia na kusikitika kwa wao kutokutambua kuwa kwa kuja kwake walipaswa kwenda kumpokea kwa furaha kwa sababu kwa kuja kwake ilikuwa ndio ukobozi wa Israel.

• Siku ya kujiliwa ni siku ya kufurahi, kuabudu, kusifu na ni siku ya amani kwa watu wote.

• Kwa nini watu hawaoni wala kutambua umuhimu wa siku ya Mungu.

a. Kwa sababu wanaongozwa na viongozi vipofu ambao hawaoni yatakayotokea mbeleni.

b. Wengine hawaoni sababu ya nafasi walizonazo, kama vile cheo, mal ink

c. Wengine wamekosa kuiona siku ya Mungu kwa sababu ya kujiinua na kujiona wao wanathamani kuliko kumuabudu Mungu

• Hata sasa wapo watu hawatambui nguvu za Mungu wala hawaoni umuhimu wa kuhudhuria ibada, jumuiya na matukio ya kiibada kwa mojawapo ya sababu nilizozitaja hapo juu, viongozi wengine wamewafanya watu kuwaona wao na kuwaabudu wao kuliko Mungu.

2. IPO HASARA KUBWA KWA WALE WALIO MBALI NA MUNGU
• Kwa wa Israel kutokutambua nyakati kwa sababu mbalimbali Yesu anaona mabaya juu ya mji wao wa Yerusalemu kuwa

a. Hekalu litabomolewa
b. Mji wa Yerusalem kuharibiwa na uzuri wake kupoea
c. Maadui zake watatawala juu ya Yerusalemu

• Hayo yote yanatokea kwa sababu tu wameshindwa kutambua wakati wa kujiliwa kwao. Kutambua na kuheshimu uwepo wa Mungu utakuepusha na matatizo mengi.

• Tujitahidi kwa wingi kuhakikisha kuwa Mungu anakuwa pamoja nasi wakati wote. Tukiutambua wakati amani itatulia juu ya maisha yetu na juu ya familia na taifa letu kwa ujuma.

HITIMISHO
• Yesu akiwa ndani yetu, akawa kiongozi wetu kwa neema yake atatuwezesha kutenda haki kwa ajili yetu na kwa ajili ya taifa letu.

• Kutenda dhambi sio tu kunamchukiza Mungu na kutupati mauti bali pia inasababisha taifa kuwa katika mabaya na machukizo mbele ya Mungu.

• Tujitahidi wote kutenda haki kwa neema ya Mungu ili baraka zake zidumu nasi milele na aweze kututahadharisha juu ya kesho yetu.

AMEN
Ev.john

SIKU YA BWANA YA 9 BAADA YA UTATU

IBADA YA TAREHE 09 AGOSTI 2020

TUENENDE KWA HEKIMA
ZABURI 119:25-32; LUKA 12:44-48

MAHUBIRI: KOLOSAI 4:2-6

1. UTANGULIZI
Katika mafafanuzi/mahubiri ya juma lililopita tuliangalia uhusiano uliopo kati ya hekima na busara. Tukawa tumesema kwamba hekima ni pana kuliko busara na ipo kama usukani wa kuiendesha busara. Busara ni namna ya kuamua jambo kwa akili kufuata mazingira. Na pia tukasema busara ni hekima inavyoonekana katika matendo. Na mkazo wetu ulikuwa katika uchaguzi wa busara. Mimi katika mahubiri nilikaza nguvu ya uchaguzi (the power of choice) na nikasema hivi tulivyo ni matokeo ya uchaguzi, nikamnukuu Dkt. John C. Maxwell aliyeandika “life is full of choices and every choice you make, makes you” (maisha yamejaa uchaguzi na kila uchaguzi unaoufanya unakutengeneza wewe). Mwisho niliorodhesha kanuni 4 za kutuongoza tunapofanya uchaguzi ili hekima ijidhihirishe katika maisha yetu.

(a) Zingatia vipaumbele na utabiri matokeo ya uchaguzi wako. Vipaumbele vinaongozwa na tunu ulizo nazo, maono na dhamira (values, vision and mission). Maana, changamoto mara nyingi sio kuchagua kati ya baya na jema bali kati ya zuri na zuri zaidi.

(b) Usikubali hisia zikuongoze. Epuka kufanya uchaguzi ukiwa na furaha sana ama huzuni/hasira
(c) Fikiria njia mbadala nyingi kabla ya kufanya uchaguzi na maamuzi.

(d) Jifunze kusikiliza dhamiri (Roho Mtakatifu). Je, unasikia amani moyoni na lile unalochagua? Amani ya Kristo iamue mioyoni mwenu (Kolosai 3:15).

Leo tunaambiwa tuenende kwa hekima mbele za wasioamini. Na somo letu Kolosai 4:2-6 ligusa suala la uinjilisti tunaweza kufanya kwa njia ya wengine kwa kuwaombea (4:2-4) au tunaweza kufanya wenyewe moja kwa moja kwa kuuendea ulimwengu (4:5-6). Mungu anatutaka tuwe makini na maisha ya sala binafsi na pia namna ya kuhusiana na watu wa dunia hii, namna ya kuishi katika ulimwengu kwa hekima.

2. DUMUNI KATIKA KUOMBA
Yesu aliwahi kufundisha pia juu ya kuomba bila kukoma katika Luka 11:5-10. Mtu aliyefikiwa na rafiki usiku wa manane akiomba asaidiwe mikate kwa ajili ya mgeni, Yesu anasema ataamka kwa vile hataki kuendelea kusumbuliwa. Na pia katika Luka 18:1-8 Yesu alitoa mfano wa kadhi aliyemsaidia mwanamke mjane kwa kuona anamsumbua kila siku kuomba amsaidie.

Paulo akawahimiza Wakolosai kuendelea kuomba kwa bidii kama yeye alivyowaombea pia (Kolosai 1:3-8). Na anaposema dumuni katika kuomba tafsiri nyingine zinatupeleka kwenye maana ya kuwa uwe na nguvu (be strong). Uwe na juhudi kubwa. Huwezi kuendelea katika maombi kama huna pumzi na juhudi katika maombi. Ni kupambana, ni vita ya kuangusha ngome za Shetani.
Maombi sio tukio la mara moja katika maisha ya mkristo. Maombi ni jambo la kila siku mbele za Mungu (1 Thesalonike 5:17).

3. MKESHE KATIKA KUOMBA NA KUSHUKURU

Paulo anawahimiza Wakolosai kuwa macho, kukesha. Hii ni lugha ya kiulinzi au kiaskari. Walinzi hodari husimama usiku mzima ili kuhakikisha lindo lao lipo salama. Kwa hiyo wanapaswa kuwa macho wakati wa maombi wasilale usingizi. Mara nyingi mwana maombi anakumbana na uchovu wa mwili na hivyo kumfanya alale usingizi wakati wa kuomba.

Yesu aliwahimiza wanafunzi wake kukesha katika maombi katika matukio mawili muhimu. Pale alipokuwa nao mlimani katika tukio la kugeuka sura (Luka 9:28-33), Petro, Yakobo na Yohana walilemewa na usingizi na kushindwa kuomba. Mahali pengine ni katika Bustani ya Gethsemani (Mathayo 26:36 -46). Walilala na akawauliza, je, hamkuweza kukesha nami hata saa moja? (26:40).

Ipo vita wakati wa maombi. Unaweza kufikiri ni vita kati ya maombi na usingizi, lakini kama unaona rohoni, kuna nguvu nyuma yake. Hakuna wajibu unaweza kufanyika kwa ufanisi bila maombi. Lakini kila uombapo kuna upinzani! Pamoja na kuomba walipaswa kumshukuru Mungu.

Maombi siyo ”Mungu nipe hiki na kile na kile! Tunasogea mbele zake kwa shangwe na shukrani kwa Mungu. Katika shukrani tunamshukuru Mungu kwa namna alivyo na atendavyo. Ukuu wake, uaminifu wake, upendo wake, neema yake, hekima yake, na mengine mengi! Bila Mungu kututendea kwa namna atendavyo, hatuwezi kudumu hata siku moja.

Katika maombi, tunaomba ufalme wake uje. Ufalme wa Mungu ukija, tunapata mahitaji yetu na kwa namna Mungu aonavyo inafaa. Tunapoomba tunashukuru sio kwa sababu tumepata tayari, bali kwa sababu tunaamini kuwa tunapata, maana Mungu ni mwaminifu. Shukrani inatuhakikishia kuwa tunamwendea Mungu tunayemwamini kuwa anajibu.

4. MTUOMBEE MUNGU ATUFUNGULIE MLANGO WA NENO TUNENE SIRI YA KRISTO
Wakolosai wanahimizwa kuomba kwa ajili ya viongozi wao wa kiroho. Viongozi wa kiroho wasipopata neema au kibali machoni pa Mungu watakwamisha shughuli za kiroho. Paulo hakuwahimiza kuomba kwa ajili ya mahitaji yake binafsi bali Mungu afungue mlango kwa neno la Mungu, yaani fursa ya kuhubiri injili, tena ili anene siri ya injili impasavyo sio kama atakavyo yeye. Hapa kuna siri kubwa! Sio kila anayesimama mimbarani na kuhubiri anahubiri Neno la Mungu. Kwa hiyo Paulo anaomba Wakolosai wamwombee ili ahubiri Neno la Mungu. Paulo anasema kuwa alikuwa kifungoni kwa sababu ya uaminifu wa kuhubiri injili ya Kristo na alikuwa tayari kupokea matokeo ya uaminifu huo hata kupata vifungo zaidi. Ukihubiri Neno la Mungu katika kweli yake, wakuu wa giza kupitia watumishi wao watatikisika na kupanga njama za kukuangamiza! Ukiweza soma habari za Danieli. Au jifunze vizuri upinzani uliokuwepo katika huduma ya Bwana Yesu. Lakini wajapojipanga kwa upinzani wa aina yoyote ile, kuna nguvu ya Mungu itujiayo katika maombi! Katika maombi tunajadiliana na kusemezana na Mungu. Mungu huja kututia nguvu na kufanyika ngao yetu.

5. ENENDENI KWA HEKIMA MBELE YA WASIO AMINI/ULIMWENGU
Paulo anawakumbusha Wakosolai kuwa maisha ya kiroho sio tu kujifungia ndani kwa maombi bali wanahitaji kuishi hekima yao kwa vitendo, kuwa na busara kama tulivyojadili somo lililopita. Hii itawaongoza namna ya kuongea na kuishi. Kwa wakati ule, tayari kulikuwa na picha mbaya kuhusu ukristo. Lakini kwa njia ya hekima na mwenendo wao walitakiwa kuiondoa ile picha mbaya na kuuonesha ulimwengu uzuri ulio katika Bwana unaodhihirika katika maisha ya Wakristo. Mienendo yetu ni mahubiri yanayoishi. Tunapaswa kumdhihirisha Yesu Kristo katika maisha yetu pia, sio maneno tu!

6. MUUKOMBOE WAKATI
Neno kuukomboa wakati linabeba maana zifuatazo: kutumia wakati kwa njia nzuri kabisa (making the best use of time) kutumia kwa makini kila fursa inayojitokeza (making the most of every opportunity), au kutumia kwa ufanisi kila wakati unalionao (make effective use of our time). Mtume Paulo kwa Waefeso 5:15-20 anasema enendeni kwa hekima mkiukomboa wakati kwa maana zamani hizi ni za uovu na wasiwe wajinga. Kila nafasi katika maisha ni muhimu lazima itumike kwa ukamilifu wote na kwa manufaa. Ndio maana imesemwa kuwa wakati ni mali. Kiroho ni kama alikuwa anawaambia kuwa wakati ni mfupi tusikubali mtu afe bila kumjua Yesu. Lakini hata wakati huu wenye mabadiliko makubwa ya kiuchumi, muda ni moja kati ya rasilimali muhimu sana katika kuleta maendeleo. Wanaojua wanatumia vizuri. Kwa bahati mbaya wapo watu ambao hawajaelewa thamani ya muda hawatunzi muda mahali wanapo hitajika.

Kuna mtu alisema hivi: nilipokuwa mtoto sikuwa na cha kufanya zaidi ya kutambaa na kusubiri nisaidiwe hiki na kile, wakati huo muda ulikuwa unatambaa. Nilipokuwa kijana nilianza kuona hili na lile, nikawa ninaongea pia, lakini muda ulianza kutembea. Nilipokuwa mtu mzima tayari ninajua maana ya maisha, nilianza kushughulika na mambo muhimu, muda ulikuwa unakimbia kweli. Nimekuwa mzee, ninataka nirekebishe nilipokesea, muda umepaa! Haupo tena! Mhubiri anasema vizuri: ”Mkumbuke Muumba wako siku za ujana wako kabla hazijaja siku utakaposema…” (Mhubiri 12:1). Usipotumia wakati vizuri, utakuja kujuta!
Bwana Yesu alionesha kuwa wana wa ulimwengu, yaani walio wa ufalme wa giza wanajua kuutumia wakati (Luka 16:8). Lakini wana wa nuru ni wazito kweli! Kwa nini wana wa ulimwengu wanajua kuukomboa wakati? Mkuu wao anajua kuwa anao muda mfupi sana! Kwa hiyo amejipanga vya kutosha na watumishi wake wanamtii! Watu wa Mungu, tusipoukomboa wakati, tutapoteza dira. Mambo mengi yataharibika na hivyo tutamletea hasara Bwana wetu pasipo sababu! Lazima tuenende kwa hekima na kuuomboa wakati!

7. MANENO YENU YAJAE NEEMA NA MUNYU NA MPATE KUJUA JINSI YA KUJIBU
Njia nyingine ya kumtangaza Kristo ilikuwa ni kwa njia ya usemi wao. Anasema maneno yao yawe na neema na munyu. Yawe na chumvi ambayo kazi yake ni kutunza kitu kisiharibike na kutia ladha nzuri. Na busara (hekima iliyo katika matendo) ingewawezesha hata kujua jinsi ya kumjibu kila mtu. Walipaswa kujibu kufuata mafundisho ya biblia sio kwa jinsi wanavyojifahamu. Na kwa vile walidhaniwa kuwa wajinga wasio na akili, basi kwa njia ya usemi wao wangedhihirisha kuwa sio watu wa kawaida. Walitakiwa kutafuta neema ya kuwa wazungumzaji wazuri.

8. JUMLISHO
Kuenenda kwa hekima katika ulimwengu ulioanguka sio rahisi. Yesu alipokuwa anawatuma wanafunzi kwenda kuhubiri aliwaambia, ninawatuma kama kondoo katikati ya mbwa mwitu. Kuweni na hekima kama nyoka lakini wanyenyekevu kama njiwa. Kondoo wakati wote yupo na mchungaji wake. Bwana Yesu anatutaka tujue kuwa peke yetu hatuwezi. Ndio maana hapa Paulo anakaza kuomba na kuombeana. Mbwa mwitu wapo kila mahali, tena hata mahali tunapodhani tupo salama. Bila Mungu kutufumbua macho, hatutastahimili. Tunamhitaji Bwana wakati wote. Ndio maana tunaambiwa tuenende kwa hekima. Hekima ya kweli hutoka kwa Bwana. Tukiwa na Bwana, tunahakikishwa hekima. Atatuwezesha kunena na kutenda kama itupasavyo. Lililo kuu katika kuenenda kwetu, tuukoboe wakati. Maana tupo kwa kitambo. Muda hautusubiri. Basi Mungu aliyetuita atuwezeshe kuenenda kwa hekima nyakati zote. Amen

Na mchg. Dkt. George Mark Fihavango
Askofu
From Mwinjilist Joseph Mshana

MAHUBIRI YA SIKU YA BWANA YA 8 BAADA YA UTATU

Somo:UCHAGUZI WA BUSARA

Masomo:
Zaburi 37:1-8
Marko 1:40-45
Mathayo8:11-13

UTANGULIZI
✏ Siku ya leo tunajifunza juu ya uchaguzi wa busara natumepewa injili mbili Marko 1:40-45; Mathayo 8:11-13. Uchaguzi ni kitendo chaku angalia ama kuoanisha kipi kinafaa ama kipihakifai.
✏Busara ni hekima au maamuzi sahihi
✏Sasa UCHAGUZI WA BUSARA maana yake ni kitendo cha kuangalia kipi kinafaa tena kwahekima.Maana unaweza ukachagua nakuona kinafaa lakini ukakosa hekima kwenye uchaguzi wako bado utakiacha kinacho faa zaidi kuliko hicho ulicho kichagua.Katika injili mbili za leo pamoja na zaburi tunajifunza mambo yafuatayo kutokana na kichwa hichi cha UCHAGUZI WA BUSARA;
1.HEKIMA KATIKA UCHAGUZI NI MWANZO WA MAFANIKIO
✏ Unaposoma injili ya Marko1:40-45 tunamwona mtu mwenye ukoma alimwendea Yesu akisema “Ukitaka, waweza kunitakasa” kwakauli hiyo alitumia hekima ya hali ya juu kumwomba Yesu amtakase kwamba kama Yesu mapenzi yake nikumuona mzima bas amtakase kama simapenzi yake amuache
✏Sisi kanisa la leo kuna mambo yanahitaji uchaguzi wenye hekima ndani yake ilituweze kufanikiwa kwa mfano unapomchagua kristo kuwa Bwana na mwokozi wa maisha yako tambua huyo Bwana hataki mtu mzembe FANYA KAZI KWA BIDII
✏Lakini pia familia yenye mafanikio huatanguliwa na hekima ndani yao baba akiwa naheshima kwa mama na watoto watafanya hivo kwasababu baba amechagua fungu jema nala baraka

2.MATAIFA WATATUTANGULIA KUINGIA MBINGUNI KABLA YETA SISI TULIO OKOKA.
✏Biblia inasema katika Mathayo 8:12″bali wana wa ufalme watatupwa katika giza la nje, ndiko kutakuwako kilio na kusaga meno”
✏Yesu ananza kwakusema watakuja watu kutoka mashariki na magharibi kaskazini na kusini watakuja kuketi kwa ibarahim,isaka,na Yakobo maana yake walioamini nawasio amini wote wataenda mbio kila moja njia yake lakini wale waliowagiza(wana waufalme mathayo8:13) ndio anasema watatupwa nje katika ufalme wagiza sasa kwanini tulioamini tutatupwa nje ni kwasababu ndani yetu wengi tumemchagua kristo lakini tunashwindwa kwend sawasawa na kanuni zake wengi tumekuwa wasengenyaji na mambo mengi laini mataifa wengine hawasali lakini wanajikita katika kutenda mema nandio maana tusipo kaasawa watatuzidi hata sisi
✏Ndugu zangu nawasihi tufanye kazi ya Mungu kungalibado mchana tuachague natufanye maamuzi saa hii wasitushinde wasio amini sisi tunanguvu zaidi yao.
3.NJIA ZETU NA MIPANGO YETU TUNAPASWA KUMKABIDHI BWANA
✏Mwimba zaburi anatuambia katika zaburi 37; 5 “Umkabidhi Bwana njia yako, Pia umtumaini, naye atafanya”
✏Kumbe sisi tunaomwamini kristo tunatakiwa kumchagua Kristo kuwa kiongozi wa mipango yetu nanirahisi tu nikukabidhi na kutumaini( kutarajiA au kuwa naimani) naye nilizima afanye tu sasa sasa kwanini watu wengi tunamkabidhi lakini hafanyi kwasababu;
✏Tumekuwa tunaishi maisha ya changanya changanya hatujachagua ninani wakusimamia mipango hiyo ingawaje wengine wanaileta kanisani lakini wakitoka wanaenda kwa waganga nandiomaana haifanikiwi kumbe sisi tulio amini tunapaswa kukabidhi na kuamini au kutumaini tu mwisho tusiongeze mengine yasiyo na mantiki
✏Tuanaambiwa kitarajiwacho kikikaiwa moyo huugua ni kwamba Unapo mkabidhi Bwana mipango yako tambua kuwa anafanya kwa mapenzi yake hapelekeshwi na yeyote hivyo jenga moyo wa UVUMILIVU
4.RIDHIKA NA HALI ULIYO NAYO
✏Ukisoma Zaburi 37:6 ” Ataitokeza haki yako kama nuru, Na hukumu yako kama adhuhuri”
✏Unajua mda wingine Mungu huwa anakuweka kwenye zone(sehemu) furani ili ujifunze sasa watu wengi tunapokuwa kwenye eneo hili huwa tunachagua hukumu mfano anapitishwa kwenye gumu fulani imani inashuka kanisani haendi anaacha kabisa kumbe swala ni kumuamini tu yeye ataitokeaza haki yako kama nuru
✏Mungu anatabia ya kujitukuza katika ya pito unalopitia hivyo mpendwa unapopitishwa kwenye gumu ama pito fanya uchaguzi wa busara usikurupuke maana anasema”Ataitokeza haki yako kama nuru,……”
MWISHO
✏Wito wangu kwenu naombeni mfanye maamuzi sahihi siku ya leo kama neno la Mungu linavyosema katika Joshua 24:15 “inasema chagueni hivemaeo mtakaye mtukatika”
AMEN.

MUHTASARI WA MAHUBIRI YA LEO TAREHE 26/07/2020

SOMO: Mwanzo 41:41-45

UTANGULIZI
Bwana Yesu asifiwe, leo tunaangalia juu ya “NEEMA YA MUNGU YATUWEZESHA” yote tunayofanikiwa kuyafanya hapa duniani pamoja na magumu yote tunayopitia neema ya Mungu peke yake ndio inayotuwezesha kuonekana tulivyo, hatuwezi kujivunia akili zetu wala nguvu zetu wenyewe ila wakati wote yote tuyafanyayo tujue kuwa ni Mungu ametuwezesha.
Waandishi na mafarisayo wao walikuwa ni watu wa kushika sheria sana na kujitahidi kwa nguvu zao kuonyesha kuwa wanafahamu juu ya usafi na uchafu wa mtu ila Yesu anapotokea kwao anataka kuwabadiisha namna ya kufiki na kutambua mapenzi ya Mungu na kuondokana na mapokeo ya wazee.
Kwa somo hili tunajifunza haya yafuatayo

1. ASILI YA KWELI YA UNAJISI.
• Wayahudi walikuwa na sheria mbalimbali juu ya vyakula wakionyesha vingine ni safi na vingine ni najisi na hata jinsi ya kujiandaa kula. Walipoona wanafunzi wa Yesu wanakula bila kunawa mikono waliwahesabu kuwa ni najisi.
• Yesu anawataka watu wake kuelewa kuwa unajisi wa kweli hauwezi kuasilishwa na nguvu za nje bali kwa nguvu za ndani.
• Kile unachokipokea na kukiingiza katika mwili wako ndio kinachosababisha nguvu ya kutoa kile kilichopo ndani yako hivyo tunapaswa kuwa makini zaidi.

2. UTAMADUNI/MAZOEA YANAWEZA KUKUFANYA USIMUELEWE YESU
• Wanafunziwakiwa ni miongoni mwa wayahudi kwa kusikia mafundisho ya Yesu juu ya UNAJISI kutokana na maelekezo na torati walizoishi nazo kwa muda mrefu (Walawi 11: 1 – 47, Mt 5:17 – 18) hawakuelewa fundisho la Yesu walifikiri kuwa amekosea na kutaka mafafanuzi zaidi.
• Yesu aliwashangaa kwa kuzingatia walichokizoea zaidi kuliko kuisikiliza sauti yake na kuelewa ukweli wa neno la Mungu kama ilivyo kwetu sasa watu wengi kutokana na mazoea ya maishahawasikilizi Mungu anawata kufanya nini.

3. MATOKEO MAZURI AU MABAYA YA MAISHA YA MTU YANATOKA MOYONI
• Moyo wa mwanadamu ndio unaoleta matokeo ya aina zote ya mwanadamu, yawe mazuri au mabaya. (mithali 4:23)
• Moyo ukiathiriwa na dhambi ndiko ambapo mabaya yote hutokea (Mhubiri 9:3, Yer 17:9) na huwa mwanzo wa maovu yote (Mk 7: 20 – 23)

HITIMISHO
Wote tunapaswa kuelekeza macho yetu na umakini wetu wote katika mioyo yetu na kuilinda isiingiliwe na dhambi na kusababisha sisi kuwa waasi mbele za Mungu. ( Efeso 4:17 – 24, 1Petro 4: 1-3,) Haya yote yanawezekana ikiwa tutakuwa watii kwa neno la Mungu wakati wote na kujifunza kwa Mungu ( Mdo 2:28, 22: 16)
Kwa akili zetu ni Ngumu ila neema ya Mungu iliyokuu sana Kwetu inatuwezesha kufanya yote.
AMEN

MUHTASARI WA MAHUBIRI YA LEO 19/07/2020

Somo:HURUMA YA MUNGU

MASOMO
zaburi1:1-69
2Wakoritho7:5-10
Mathayo9:1-8*
UTANGULIZI
▶Jumapili ya leo tunajifunza juu ya huruma ya Mungu kwa wanadamu
▶Katika tafakari hii ya huruma za Mungu tumepewa kutoka injili ya mathayo9:1-8, ambapo tunamwona Yesu akiwa anaponya na kupoza wagonjwa ambapo kila alieponywa aliambiwa “umesamehewa dhambi zako” chukua godoro lako na uende zako
▶Kitendo hicho cha kusema “umesamehewa dhambi” zako kiliwaudhi mafarisayo wakaanza kusemezana wao kwa wao huyu ninani hata asamehe dhambi lakini wasitambue nini wana kisema.
▶Mafarisayo waliendelea kusemezana wao kwawao nanafsi zao kwamba Yesu anakufuru(anaasi) kusema kwa mgonjwa amesamehewa dhambi hii ili kuwa nikutotambua mamlaka ya Yesu duniani ama Kristu ninani.
▶Kupitia kisa hiki cha Mathayo9:1-8Tunajifunza mambo yafuatayo juu ya huruma ya Mungu

1.MATESO NA MASUMBUFU TUNAYOPITIA WAKRISTO NI KUTOKANA NA DHAMBI
▶Ndugu zanguni Wakristo Mungu anasema amejaa huruma na neema nyingi lakini utashangaa wakristo wengi wanapita katika magumu nikutokana na dhambi. Ukitaka kuishi maisha ya raha tunza Utakatifu wako.
▶ Kuna wakati unajikuta unapita kwenye majaribu mazito sana kumbe nikutokana na dhambi kumbe dawa ya kuishi maisha ya raha ni kukimbilia huruma za kristo Yesu
▶Tunamwona mwanamke aliopooza aliambiwa umesamehewa dhambi zake .

2.MAGONJWA MENGI HULETWA NA DHAMBI
▶Ukiangalia dunia ya sasa inakabiriwa na magonjwa mazito mfano ukimwi kama tutamua kufuata kanuni nasheria ambazo Mungu ameagiza hakika hatutoweza kupigwa na magonjwa ya ajabu
▶lakini kwa huruma yake anasema “atatuponya magonjwa yetu yote na ataukomboa uhai wetu na kaburi” kumbe hata kama tumemtenda dhambi Tuombe toba ili huruma yake iendelee kutembea nasi.

3.TUNATAKIWA KUTAFAKARI MASHAURI YETU MBELE ZA MUNGU
▶Wakati Yesu anaponya wagonjwa mafarisayo walianza kusema inakuaje anasamehe dhambi hili lili kuwa nishauri ambilo kwao waliona ni kufuru.
▶Wakristo wa leo ili kuikimbikia huruma ya Bwana tunatakiwa kulifuata shauri la Bwana tutakuwa salama maana ndimo huruma ya kristo hutembea kuwahudumia walio wake.(Zaburi1:1-6)

4.MUNGU PEKEE NDIO MFARIJI WA KWELI
▶Ndugu zangu washarika tunatakiwa tutambue kuwa Yesu kristo ndio mfariji pekee ama chaguo la kwanza la kukimbilia wengine huenda kutafuta faraja kwa wagaga,marafiki,na watu wengine lakini faraja yao ni ya mda tu kimbia sasa mbio mbele za kristo akufute machozi.2Wakoritho7:5-10
▶Nandiomaana anasema njooni kwangu msumbukao na kulemewa na mizigo nami nitawapumzusha.

MWISHO
▶Siku ya leo tunaitwa na huruma hii katika Isaya 1:18 ya kwamba twende tukasemezane naye iliatubadirishe na kututengeneza haijalishi mwanzo wetu ulikuwaje
KUMBUKA:Mabadiriko huanzia ndani ya Moyo wako
▶Mungu anisaidie na akusaidie ili tuweze kutambua huruma yake maishani mwetu.
AMEN.

MUHTASARI WA MAHUBIRI YA LEO 12/07/2020

SOMO: UFUASI NA UANAFUNZI

Yohana 6:66-71
Yeremia 1:17-19

UTANGULIZI
 Jumapili ya leo tunajifunza juu ya Ufuasi na Uanafaunzi
 UFUASI ni hali ya kufuata itikadi, mwenendo au kitu Fulani
 UANAFUNZI ni hali ya kuwa katika mafunzo
 Kwa maelezo haya mtu huwezi kuwa mwanafunzi kabla kuwa mfuasi, sababu lazima uwe na itikadi ambayo unataka kujifunza ili uweze kuwa mwanafunzi
 Mkristo ni mtu aliyekubali kumfuata Yesu Kristo na Yesu anamfanya kuwa mwanafunzi wake ili aweze kujifunza kwake(Yesu) ( Luka 9:62)
 Somo ambalo tunatafakari leo juu ya mada hii ni kutoka Yeremia 1:17 – 19
 Nabii Yeremia ni mfuasi na mwanafunzi wa Yesu ambapo katika mistari hii Mungu Mungu anamwambia Yeremia pamoja na sisi jinsi ya kuwa mfuasi na mwanafunzi mzuri kwake.

1. UFUASI NA UANAFUNZI UNAHITAJI UTII NA UAMINIFU
 Mtumishi mwaminifu wa Mungu anakuwa mtii kwa yote anayoelezwa na Mungu. Mtumishi asiyemwaminifu Mungu anasema mtu wa namna hiyoa ataadhibiwa sana
 Mungu anatutaka tuifanye kazi yake kama alivyotupa wito tulipokubali kuwa wafuasi na wanafunzi wake.

2. UFUASI NA UANAFUZNI UNAHITAJI UVUMILIVU NA USTAHIMILIVU
 Mkristo anao uwezo wa kukabiliana na changamoto zote anazokabiliana nazo kwa kulifahamu neno la Mungu (Mt 4: 1 – 11)
 Wanaokuchukia wasikuyumbishe wala kukurudisha nyuma katika ufuasu na uanafunzi wako kwa sababu ni wale ambao wanapinga kweli ya neno la Mungu ( Yn 15:18 – 25)
 Pamoja na upinzani wote mfuasi na mwanafunzi wa Yesu anapaswa kusimamia neno la Mungu katika uaminifu na utakatifu wake huku akilisema neno la Mungu bila upendeleo wowote.

3. UFUASI NA UANAFUZNI UNAHITAJI KUTOKUYUMBISHWA.
 Majaribu na vikwazo ni sehemu ya utumishi wetu, hivyo tusiogope maana Mungu yu pamoja nasi ( Yer 37:16, Yer 38:6)
 Mtumishi anayemtii Mungu lazima atashinda pamoja na changamoto zote atakazokutana nazo ( Rum 8:35 – 39)

HITIMISHO
 Mungu alikuja kwa watu wake na wote waliompokea aliwapa uwezo wa kufanyika watoto wake na hao ndio wale waliaminio jina lake.
 Mungu atusaidie ili tuwe wafuasi na wanafunzi waaminifu kwa Mungu wetu na tufanyike watoto wake.
AMEN.

MUHTASARI WA MAHUBIRI YA LEO TAREHE 05/07/2020 SIKU KUU YA VIJANA

MASOMO
Zaburi 37:25-40
1samwel 17:38-45
Mathayo 11:25

Wazo la wiki:NGUVU YA VIJANA KATIKA KANISA
____________________________

Somo:MAISHA YA USHINDI YA KIJANA MKRISTO

Fungu:1 YOHANA 2: 12 – 17

UTANGULIZI
• Jumapili ya Leo Tunajifunza maisha ya ushindi ya kijana Mkristo. Yohana ambaye alianza huduma ya uanafunzi wa Yesu akiwa na umri mdogo tu wa miaka 16 na sasa amekuwa mzee na anawaandikia wakristo wote akiwapa ushauri jinsi ya kuendenda kwenye ulimwengu huu huku wakihakikisha kuwa wanaupata ufalme wa Mungu.

• Katika mistari hii tuliyoisoma katika waraka huu Yohana anawagawanya wasomaji wake katika makundi matatu

TOBA NI MWANZO WA ULINZI WA MUNGU KATIKA MAISHA YETU.
• Kundi la kwanza ni watoto ambao wao ndio wameupokea ukristo anawaambia kuwa safari yao ya Ukristo inaanza na msamaha wa dhambi na anawahakikishia kuwa uhusiano wao na Mungu umerudishwa kama uhusiano wa baba na mtoto.

• Kundi la pili na la kina baba, hawa ni wakristo wa muda mrefu anawaonyesha uhuhimu wa kuwa na kumbukumbu katika maisha yao na kujua kuwa hata kama wana uzoefu wa Kiroho namna gani huwezi kumshinda Mungu bado unapaswa kuendelea kumtegemea wakati wote.

• Kundi la tatu ni vijana, anazungumza na kundi hili akilionyesha kuwa lina nguvu, limekuwa na uwezo wa kumshinda shetani na neno la Mungu linakaa kwa wingi ndani yao.

• Sifa hizi ni sifa za kundi hili la vijana, kuwa wana nguvu, neno la Mungu linakaa ndani yao na limewawezesha kumshinda yule mwovu.

• Analiambia kundi hili kuwa mapambano yapo katika maisha yao ila uwezekano wa kushinda upo sababu wapo kwenye nafasi nzuri ya kushinda.

• Neno la Mungu lililopo kwa wingi ndani yao ni chanzo chema cha hekima ya kujua jinsi ya kumpinga yule mwovu. ( Lk 4:1 – 13, Mt 4:1 – 11)

• Makundi yote haya matatu Yohana anayataka, kwanza, yanapaswa kupendana na pili yanapaswa kuchukia mambo ya giza ambayo anayaita mambo ya dunia na anatutaka tujitenge mbali na dunia kwa sababu hatuwezi kupenda dunia na Mungu ( 1Yoh 2:15, Mt 6:24)

a. Ni Dunia gani anayoizungumzia Yohana?
b. Dunia hii ni ya aina gani?
c. Dunia hii ina sifa hani?
d. Je, tunaweza vipi kuishinda dunia hii?

NI DUNIA GANI ANAYOIZUNGUMZIA YOHANA?
• Yohana hazungumzii dunia hii iliyoumbwa na Mungu ( Mdo 17:24) wala kuhusu dunia ya utu wa mtu ( Yn 3:16)

• Dunia anayoitaja Yohana inatokana na neno Kosmos lenye maana ya utaratibu au mpango wa mfumo wa utaratibu wa mwanadamu

• Dunia hii ni mfumo wa mawazo na matendo yanayomhusu mtu katika jambo Fulani. MF. Juma yupo kwenye dunia ya siasa, maana yake Juma anajishughulisha na siasa zaidi.

• Dunia hii ni maisha na mpango wa mwanadamu vinavyotengenezwa bila kumkali Mungu na mapenzi yake na katika hali hiyo ni chini ya shetani

DUNIA HII NI YA AINA GANI?
• Dunia hii na tamaa zake zitapita sio za milele na yule anayeitegemea pia hatadumu (1Yoh 2:17) na hata kama mtu huyo anaonyesha kushinda sasa ila mwisho wake utafika ( Uf 20:7 – 10, uf 21:1- 4)

• Dunia hii inamshambulia mwanadamu katika ukamilifu wake ( 1Thes 5:23) Kiroho, kimwili na kisaikolojia. Anatushambulia kiroho ili tusimpende Mungu, kimwili ili tusiweze kuishi kwa ajili ya Mungu na kisaikolojia ili tushindwe kujifunza kwa Mungu. Mfano wakati wa anguko. ( Mwa 3)

a. Hawa aliona mti unapendeza macho na kumuondoa katika kumpenda Mungu(mashambulizi ya rohoni)
b. Mti Watamanika kwa Maarifa, hapo shetani anamuondoa Hawa katika kujifunza kwa Mungu( mashambulizi ya kisaikolojia)
c. Wafaa kwa chakula anamuondoa Hawa katika maisha ya kuishi kwa ajili ya Mungu na kumtegemea yeye (mashambulizi ya Kimwili)

DUNIA HII INA SIFA GANI?
Biblia inatueleza wazi sifa za Dunia hii
a) Dunia ya namna hii ina kiongozi wake ambaye ni shetani ( 2Kor 4:14, Yn 12:31)
b) Ni dunia ya uovu ( 1Yoh 5:19)
c) Dunia hii ina watoto wake ( Lk 16:8)
d) Dunia hii ina hekima yake yenyewe ( 1Kor 2:6)
e) Dunia hii ni chafu ( 2Pet 1:4)
f) Dunia hii ndio iliyomsulubisha Yesu ( 1Kor 2:8)

TUNAWEZAJE KUSHINDA DUNIA HII?
Ili kuwaeza kuishida dunia hii lazima upambane nayo kimwili, Kiroho na kisaikolojia (nafsi)
a) Njia ya kushinda ulimwengu huu kimwili ni kujitenga na dhambi(1Thes 5:22) Ruhusu hamu yako ya kuishi kwa ajili ya Mungu iongoze njia na kazi zako
b) Ili uweze kuishinda dunia hii kisaikolojia ( 1 Yoh 5:4b) Ruhusu hamu ya kujifunza kwa Mungu ikuze ufahamu wako na uelewa wako
c) Ili uweze kupambana Kiroho ni kujisalimisha kwa Mungu ( Yak 4:7) Ruhusu hamu ya kumpenda Mungu iongoze maamuzi yako.

HITIMISHO
• Tunapaswa kujua kuwa ulimwengu unapita ila Mungu atadumu nasi milele ( 1 Tim 6: 11 – 12)

MAHUBIRI YA JUMAPILI TAREHE 28/06/2020

Somo:NEEMA YA MUNGU ITUOKOAYO
Masomo:
Zaburi 59:1-9
Matendo 11:1-15
*Luka 8:26-39

SHABAHA: Wasikilizaji waweze kuelewa kuwa ili kupata ahadi za Mungu tunapaswa kumtegemea Mungu.

“Kwa kuwa mwana wa Adamu alikuja kutafuta na kuokoa kile kilichopotea” (Lk 19:10)

UTANGULIZI: Leo ikiwa ni siku ya tatu baada ya utatu tunaangalia mada izungumzayo juu ya Neema ya Mungu ambayo inatuwezesha sisi kuupata wokovu.

> Neema maana yake ni mafanikio aliyonayo mtu kutokana na majaaliwa ya mwenyezi Mungu au kwa juhudi zake mwenyewe.

> Hivyo:- tunaweza kusema kuwa leo tunazungumzia juu ya mafanikio aliyonayo mtu kutoka kwa mwenyezi Mungu ambayo yanaleta wokovu katika maisha ya mtu.

> Katika kutafakari Neema hii ya Mungu iletayo wokovu tumepewa kisa kutoka katika biblia Luka 8:26 – 39. Kisa hiki ambacho kimeelezwa hapa pia kimeelezwa katika kitabu cha mathayo 8:28-34 na kitabu cha Marko 5:1-20 ikizungumza habari ya mtu aliyepagawa na pepo wachafu ambao wamejitambulisha kwa jina la Legion maana yake ni jeshi kubwa la warumi lenye nguvu lililokwa na idadi ya wanajeshi 6000.

Katika kisa hiki unajifunza mambo yafuatayo:-

SHETANI NI MHARIBIFU

Mtu huyu ambaye amepagawa nna pepo tunaambiwa kuwa alikuwa Uchi, aliishi makaburini, na alikuwa akijikatakata na mawe (Marko 5:3) Shetani anapoingia kwetu hahurumii hata miilil yetu atatutaabisha na kuwa wahitaji wakati wote.

ULINZI WA KIBINADAMU HAUJITOSHELEZI

Mtu huyu alifungwa kwa pingu na hata kwa minyororo ila aliikata yote na wanadamu wakakata tama nay eye na kumuacha alivyo. Unaweza kutegemea wanadamu wanaweza kukusaidia ila ni kwa kitambo kidogo na utabaki katika shida yako.

BINADAMU WENGI WANAANGALIA KITU KULIKO UTU

Tunaelezwa kuwa baada ya mtu huyu kuponywa watu wa mji ule walimfukuza Yesu kwa sababu walipiga hesabu ya hasara ya nguruwe 2000 waliofia majini waliona mwenzao amepata hasara kubwa sasa hawakujua nani angefuata wakaogopasana wakaamua kumwambia aondoke kwao.

MUNGU ANAJISHUGHULISHA NA MAHITAJI YETU

Yesu alivyoona kuwa mtu huyu yupo uchi, anaishi makaburini mbali na watu na alikuwa akijikata mwili kwa mawe alijua kuwa anahitaji msaada hivyo aliona nguruwe hawana umuhimu kama mtu wake akayaelekeza mapepo kwa nguruwe na kumponya yule kijana. Mapepo yalikwepa kwenda kuzimu yakidani kuwa yakiingia kwa nguruwe yatakuwa salama ila baada ya kuingia nguruwe walikufa wote na mapepo bado yakaenda kuzimu.

UKIMKUBALI MUNGU UTAKUWA SALAMA

Baada ya mtu huyu kuponywa alitulia chini ya miguu ya Mungu akiwa amevaa nguo na akiwa na akili yake timamu. Amani ya kweli inapatikana kwa kumkubali Yesu

MEMA ANAYOKUTENDEA MUNGU ANATAKA UMTUMIKIE

Mtu aliyeponywa alitaka kandamana na Yesu ila yesu alimwambia aende kuelezea habari njema za Yesu kwa watu wa nyumbani kwake kwa kuwa eneo lile liikuwa ni eneoo la wapagani nao waone wema wake. Baraka tunazopata tunatumwa tukahubiri.

HITIMISHO

Bora kuwa mlinzi wa getini kwa Mungu kuliko kuwa mfalme au malkia nje ya Mungu sababu huko hakuna mafanikio ya kweli, mafanikio ya kweli yaletayo wokovu yanapatikana kwa Mungu tu.

MUHTASARI WA MAHUBIRI YA LEO TAREHE 21/06/2020

siku ya 2 baada ya utatu

SOMO: TUKAE PAMOJA KWA UMOJA
MASOMO Yohana17:20-21
?Efeso 5:8-14
? Zaburi 133

UTANGULIZI
• Jumapili ya Leo ni sikukuu kubwa ya KKKT, tuanze mafundisho yetu ya leo kwa kumtakia ndugu yako heri ya siku kuu.
• Leo ni jumapili ambayo tunaazimisha kuunganika kwa makanisa saba ya Kilutheri Tanganyika ambayo ni:-
a) Kanisa la kiinjili la Kilutheri la Iraqw
b) Kanisa la Kiinjili la Kilutheri la kaskazini mwa Tanganyika
c) Kanisa la Kiinjili la Kilutheri la Kaskazini Magharibi mwa Tanganyika
d) Kanisa la Kiinjili la Kilutheri la Kati mwa Tanganyika
e) Kanisa la kiinjili la Kilutheri la Kusini mwa Tanganyika
f) Kanisa la Kiinjili la Kilutheri la Usambara Digo
g) Kanisa la Kiinjili la Kilutheri la Uzaramoni – Uluguru

• Makanisa haya saba yalipoungana yalikwa na washarika laki tatu (300,000) tarehe 19/06/1963 hadi kufikia leo hii kanisa moja la Kilutheri lina zaidi ya dayosisi 25 na waumini zaidi ya milioni sita. (6,000,000)
• Siku ya leo tunaadhimisha miaka mia moja na thelathini (133) ya ulutheri Tanzania.
• Mwaka huu neno linalosindikiza sikukuu hii ni kutoka YOHANA 17;20-21 ambalo linaendelea kukaza juu ya umoja katika kanisa.
• Mlango huu wa 17 ni mlango wenye sala ya Yesu, kwanza anaanza kwa kujiombea yeye mwenyewe, kisha anawaombewa wanafunzi wake na anahitimisha kwa kuwaombea waumini wote wawe na umoja.
• Kipengele tulichosoma kinatufundisha mambo kadhaa

1. YESU NDIE MWANZILISHI WA KANISA
• Aliwaita wanafunzi na kuwaandaa kwa kazi maalumu ya kulihubiri neno lake ( Marko 3:14)
• Aliwaandaa kuifanya kazi aliyokuwa anaifanya yeye mwenyewe
• Aliwataka wawe na umoja ili waweze kuwa na lengo moja
• Maswali ya kujiuliza sisi wenyewe
a) Wewe umeandaa watu wa kufanya kazi ambayo unaifanya?
b) Je, wewe katika kazi/ huduma unayoifanya unazingatia umoja? Au unatengeneza makundi?

2. LENGO LA YESU NI KUONA KANISA MOJA
• Mungu anawataka waumini wote wawe na umoja na kuweka tofauti zao pembeni(Yesu anajua kuwa tunazo tofauti ila tukubali kuziweka pembeni na kuwa na umoja katika lengo moja)
• Umoja huu anataka ufanane na umoja wa Mungu na Yesu yaani umoja usio wa Kinafiki, umoja ambao hauwezi kutenganishwa. ( Umoja wetu katika utofauti wetu ufanye hata watu kushangaa tumeweza vipi kuwa wamoja)
• Umoja huu uwe ni umoja uliofungwa katika upendo wa kweli ( Yohana 13:34 – 35)
• Swali la kujiuliza waumini wale wanaojitenga na ibada kama vile kutokuwa kundini na kuanzisha madhehebu mengine bado Yesu anawahesabu kama wanafunzi wake? Wengine hata kukwepa majukumu ya kazi za umoja kama vile sadaka za umoja nk ni wafuasi wa Yesu Kweli?

3. UMOJA WA KIKRISTO UWE UMOJA WENYE MALENGO
• Umoja huu unapaswa uwe umoja unaoendelea kukua kama tulivyoona historia ya kanisa letu.
• Umoja huu uwe ni umoja wenye imani moja
• Umoja huu uwe ni umoja unaoendeleza utukufu wa Mungu ulimwenguni kote.
• Umoja unaosogeza waumini wote kuwa familia moja, kijiji kimoja. Tukitambua kuwa Yesu ndie mwanzilishi wa utandawazi ( Matayo 28:19 – 20, Mdo 1:8)
• Kanisa la Kiinjili la Kilutheri kwa kutambua kwamba misioni ya Bwana Yesu inaendelea kukua na kupanuka imeendelea kujitahidi kuleta umoja kwa kuweka uwiano wa sadaka za umoja ili kukidhi hitaji hili ambazo zinafanya kazi ya:-
a) Kutuma wachungaji maeneo ya misioni ya ndani na nje ya nchi
b) Kuhisani masomo ya wanafunzi wanaotoka maeneo ya misioni
c) Kuendesha vituo vya kazi za umoja kama vile Ofisi kuu ya kanisa, Shule ya viziwi mwanga na Njombe, Radio sauti ya injili, Seminari ndogo ya Morogoro nk.
Mimi na wewe tumeshiriki vipi katika misioni hii ya Yesu?

HITIMISHO
• Roho mtakatifu atusaidie kutambua kusudi la Yesu kwa kanisa lake nasi kama wafuasi wa kweli tuungane kwa upendo kuliendeleaza kanisa la Mungu.
• Umoja ni silaha kubwa sana katika huduma yetu ya uinjilisti. Ubora wa ushirikiano wetu unawavuta watu wengi kwa Mungu na udhaifu wa umoja wetu unalitawanya kundi la Mungu na kulipoteza huku ushuhuda wetu ukiendelea kuwa dhaifu
• Tuwavute watu kwa Mungu kwa kudumisha umoja miongoni mwetu.
AMEN.

MAHUBIRI YA SIKU YA BWANA YA 1 BAADA YA UTATU TAREHE 14/06/2020

MADA: MUNGU AU ULIMWENGU

MASOMO:
ZABURI 78: 17 – 22
YOHANA 7:40 – 52,
MATENDO YA MITUME 5: 34 – 42

SHABAHA: Wasilkilizaji waweze kutambua kuwa uchaguzi sahihi nu ule wa kuchagua Mungu kwa sababu wakati wote yupo sahihi.

UTANGULIZI
Biblia inatufundisha kuwa Mungu sio nguvu Fulani tu inayomuwezesha mwanadamu kufanya jambo Fulani bali ni nafsi hai na hili huonekana wazi mtu unapokubali kumjia yeye na kupata mahusiano na ushirika nae (Yn 17:3)

Mungu ni nafsi hai iliyojidhihirisha kwenye nafsi tatu ili kumsaidia mwanadamu asibaki tu na ujuzi mdogo au hisia tu.(Yer 1:1 – 3, 2Pet 1:21)

Mungu ni wa milele asiyetawaliwa. Hawezi kupimwa kwa kipimo cha wakati, kwa sababu yeye hana mwanzo wala mwisho (Zab 90:2, Isa 48:12, Yn 5:26) Hana haja ya kutoa hesabu mahali popote wala kwa kiumbe chochote na hana haja ya kutoa sababu kwa uamuzi wake wala kuelezea matendo yake (Zab 115:3, Mdo 4:48) ingawa katika neema yake mara nyingine anafanya hivyo (Mwa 18:17 – 19, Efe 1:9) Hekima yake haina kikomo na hivyo iko nje ya uwezo wa mwanadamu ( Zab 50: 10 – 13, Mdo 17:24 – 25) Jambo lolote analolitenda analitenda kwa sababu ameamua hivyo, wala si kwa sababu alilazimika kufanya hivyo (Efe 1:11)
Mungu ni mwenye enzi na mamlaka yote. Hakuna kikomo kuhusu kuwepo kwa Mungu au ujuzi wake. Jambo hili ni kweli kwa furaha na hofu. Kwa furaha sababu hakuna mtu amtegemeaye ataweza kutengwa naye; na kwa hufu kwa sababu hakuna dhambi inayoweza kufichwa mbele zake ( Zab 139: 1 – 12, Ebr 4:13).

Mungu habadiliki lakini anajibu na kuitikia, Mungu asiyebadilika maana yake hana kikomo wala mwanzo wala mwisho hivyo hana namna ya kuongeza au kupunguza hali na sifa zake. (Kut 34:6 – 7) kutokubadilika kwa Mungu kuna maana kuwa yeye ni thabiti katika matendo yake yote(Ebr 6:17 – 18, Yak 1:17)

Biblia inaeleza ulimwengu ni vitu vilivyoumbwa na Mungu au watu wanaoishi katika ulimwengu (Zab 90:2, 98:7,9) kwa sababu ya dhambi ulimwengu ulikuwa sehemu ambamo shetani anatawala katika maisha ya watu (Yn 12:31, Rum 5:12 1Yoh 5:19) mara nyingi biblia inasema juu ya ulimwengu kuwa ni jambo lililo ovu au kinyume cha Mungu (Yn 7:7, Yak 4:4). Ulimwengu katika maana hii ni jambo la wanadamu wenye dhambi pamoja na tabia mbaya zilizo alama za wanadamu wenye dhambi.

Mkristo hawezi kushinda majaribu ya ulimwengu kwa kutumia mbinu za ulimwengu. Njia moja tu ya kushida ulimwengu ni kutegemea nguvu ya Kristo, aliyemshinda shetani aliye mkuu wa ulimwengu huu (Yn 12:31, 1Yoh 5: 4 – 5)
Kwa kuzitegemea nguvu za Mungu wanadamu wanao uwezo wa kuushida ulimwengu na kuishi maisha yanayompendeza Mungu. Wote tunaalikwa kati ya Ulimwengu na Mungu basi tuchague Mungu Huku tukifahamu haya ambayo neno la Mungu linatufunza katika somo nililolisoma kuwa:-

1. KAZI YA MUNGU HAIHITAJI KUJIHURUMIA KULIKO KUMTEGEMEA YEYE
 Wanafunzi wakiwa na ujasiri wa hali ya juu pamoja na kutambua wivu uliotawala kwa ajili ya mafanikio yao, huku wakiwa wamepigwa marufuku kali kufundisha kwa kutumia jina la Yesu na ufufuo wake na wakitambua mamlaka ya baraza lile na uwezo wa wanachoweza kuwafanyia hata kuwaua ila waliendelea kuwaeleza wazi kuwa wao ndio waliomuuua Yesu pasipo kujali nini kitawapata kutokana na ukweli huo.

 Hii ndio kazi ya wakristo wote kutokufungia macho uonevu unaojitokeza na kueleza ukweli wote kwa yeyote pasipo kujali chochote ambacho kinataka kukuondoa kwenye imani ya kumtegemea Mungu

2. UKIWA NA UHAKIKA NA NGUVU ZA MUNGU MAMBO YA DUNIA HAYAWEZI KUYUMBISHA IMANI YAKO
 Jumapili iliyopita tulijifunza juu ya Farisayo aitwae Nikodemu ambaye alikuwa mwanafunzi wa siri wa Yesu Kristo ambaye alikuwa mwalimu wa torati, tajiri na aliyeheshimika na sasa wanafunzi wake wanapoanza huduma tunakutana na Mfarisayo mwingine ambaye ni mwalimu wa torati, tajiri na aliyeheshimika sana ambaye anaonyesha anakuballiana na mafundisho ya Yesu na anatoa maamuzi ya hekima kuwa mambo amabyo yameanza ambayo asili yake sio Yesu Kristo basi hufa ila kama yameanzishwa na msingi wa Yesu Kristo kamwe hayawezi kuvunjika na ni hatari kupambana nayo. Na Ushauri huu unapokelewa.

 Yanaweza kutokea mambo ambayo huyaelewi ila kwa vile una uhakika na nguvu za Mungu basi mwachie Mungu mwenyewe ni hakimu mwenye haki.

3. HATUHITAJI KUWAOMBEA MABAYA ADUI ZETU
 Wanafunzi wanachapwa viboko na wanapoachiwa wanaondoka kwa furaha kuwa wamehesabiwa mateso kwa ajili ya Yesu na wanadumu wakiomba na kufundhisha juu ya uweza na Mungu huku wakitambua kuwa ulimwengu hauwezi kuwafanya chochote.

 Adui zetu wakikaza kutuudhi nasi tuzidi kuongeza kiasi cha furaha yetu tukitambua kuwa nguvu za Mungu zitatupatia haki yetu.

HITIMISHO
Mungu atuwezeshe tuweze kumtumikia kwa uaminifu na ujasiri pasipo kuogopeshwa na vitisho vya wote wanaoukataa ukweli pasipo kujihurumia sababu Mungu mwenyewe asiyetawaliwa wala kubadilika atatulinda daima.