SOMO:KATIKA YESU KILA JARIBU LINA MLANGO WA KUTOKA
ZABURI 139:11-16;
MATHAYO 4:1-11
*SOMO LA MAHUBIRI: DANIELI 3:19-23*
WIMBO: TMW 86
*UTANGULIZI*
Nebukadreza mfalme wa Babeli aliishinda Yerusalemu na kuwachukua watu mateka wakiwepo kutoka katika nyumba ya kifalme, huu ulikuwa wakati wa Mfalme Yehoyakimu wa Yuda, pia vyombo vya nyumba ya Bwana vilichukuliwa hadi Babeli. Hii ilikuwa hukumu ya Mungu kwa uasi wa ufalme wa Yuda. Kwa upande mwingine huu ulikuwa mwanzo wa mpango wa Mungu ndani ya uhamisho (Danieli 1:1-2). Mateso na majaribu hayamaanishi kwamba Mungu hayupo. Mfalme Nebukadreza akamwagiza Ashpenazi Mkuu wa matoashi amtafutie vijana wa Kiebrania wenye vinasaba vya kifalme, wasio na mawaa, wazuri wa uso, wajuzi wa hekima, werevu kwa sababu ya maarifa yao, wenye kufahamu elimu, watakaoweza kusimama katika jumba la kifalme. Ili wafundishwe lugha ya Wakaldayo, elimu ya kifalme, na utamaduni mpya. Vijana hawa wanne hata majina yao yalibadilishwa kama jaribio la kubadili utambulisho wao wa kiimani lakini ilishindikana walibaki na Imani yao (Danieli 1:3-7). Vijana hao ni: Danieli – Belteshaza Hanani – Shadraka Mishaeli – Meshaki Azaria – Abednego Hawa vijana walionesha msimamo usiokuwa wa kawaida walikataa kula chakula cha kifalme walichoagizwa walishwe miaka mitatu wao wakala mtama na maji na afya zao zikawa nzuri kuliko wale vijana waliokula chakula cha mfalme. Mungu aliwapa neema na hekima na mwisho wa siku walipoingizwa mbele ya mfalme kwa usaili walionekana kuwa bora mara kumi zaidi ya waganga na wachawi waliokuwa katika ufalme wake (Danieli 1:-20). Ilitokea kwamba mfalme aliota ndoto ambayo ilifadhaisha roho yake na usingizi kumwacha. Alitoa amri ya kuitwa kwa waganga, wachawi, wasihiri na wakaldayo ili watoe tafsiri ya ndoto ambayo alikuwa ameisahau. Wakaldayo wakajibu na kusema kuwa Hapana mtu duniani awezaye kulionesha neno hili la mfalme kwa maana Hapana mfalme wala bwana aliyetaka neno kama hili. Ni neno la ajabu analotaka mfalme, hakuna awezaye kumwonesha mfalme neno hilo ila miungu wasio na kikao Pamoja na mwenye mwili. Mfalme akakasirika mno akatoa amri ya kuua wenye hekima wote wa Babeli (Danieli 2:1-12). Wenye hekima wakawa wanatafuta kuuawa na Danieli na wenzake ambao hawakuwepo wakati wale wengine wanashindwa akawa anawatafuta Pamoja na wenzake ili wauawe. Danieli akamuuliza Arioko Akida wa walinzi wa mfalme aliyetumwa kuwaua, akasema, mbona amri ya mfalme inau kali hivi? Akaomba aingie kwa mfalme na akaomba apewe muda wa Kwenda kutafuta hiyo tafsiri. Danieli akawapasha Habari wenzake watatu kwamba waombe rehema na kupewa tafsiri au siri ya ile ndoto. Usiku Danieli akapewa ile ndoto ambayo mfalme aliota Pamoja na tafsiri yake. Mfalme Aliona sanamu kubwa. Kichwa cha dhahabu – Babeli (Ufalme wa Nebukadreza). Kifua na mikono yake ya fedha – Ufalme unaofuata. Tumbo na viuno vyake vya shaba – ufalme mwingine Miguu ya chuma nyayo zake nusu chuma na nusu udongo – Falme zinazogawanyika. Maana yake falme hizi ni za muda na dhaifu. Jiwe lililochongwa bila mikono, liliipiga sanamu miguu ikavunja vipande vipande huu ni ufalme wa Mungu wenye nguvu na utadumu milele (Danieli 2:13-45). Mfalme Nebukadreza akamtukuza Mungu akampa Danieli cheo cha kuwa mkuu juu ya Uliwali wote na mkuu wa wote wenye hekima wa Babeli na Danieli akawaombea nafasi wale wenzake watatu (Danieli 2:46-49). Tunapoanza na masilimulizi ya sura ya tatu inaonekana kuwa mfalme Nebukadreza aliazimia kupinga maelekezo ya Mungu ambayo yalitolewa na Danieli katika tafsiri ya ndoto. Aliamua kutengeneza sanamu ya dhahabu tupu kama kuashiria kuwa ufalme wake hautakoma kinyume na ujumbe wa ndoto. Nebukadreza aliamuru watu wote waabudu sanamu ile na kutofanya hivyo ilitafsiriwa kama kosa la uhaini (treason). Watu wote walitii isipokuwa watatu (Shadraka, Meshaki na Abednego). Kufuatia habari zilizopo sura ya pili, Danieli alipandishwa cheo na hivyo akawa anatumika ikulu, kwa hiyo hakujumuika nao. Huu ulikuwa mtihani wao na Danieli alipewa mtihani wake peke yake baadaye (Danieli 6). Inaonekana watu walikuwa wanawafuatilia wakagundua kuwa hawa jamaa wamegoma kuabudu sanamu, wakapeleka taarifa kwa mfalme Nebukadreza. Inaonekana kulikuwa na wivu wa kisiasa kwani hawa wageni walipewa nafasi za utawala. Nebukadreza hakutaka kuwachukulia hatua kwa maneno ya kusikia akawaita na kuwahoji. Je, ni kweli mmekataa kuabudu sanamu? Akawapa nafasi ya kufanya hivyo na kwamba wakikataa watatupwa kwenye tanuru la moto ili aone ni mungu yupi atakaye waokoa na mkono wake na pia na tanuru la moto. Na hapa ndipo alipokosea kumhusisha Mungu katika hoja zake. Wakamjibu kuwa hawakuwa na haja ya kujitetea, kosa wanalijua lakini Mungu wanayemtumikia atawaokoa na tanuru na mkono wa mfalme. Wakasema wazi kuwa hawakuwa tayari kutumikia miungu ya Nebukadreza wala kuabudu sanamu yake (Danieli 3:1-18). Ndipo linafuata somo letu la mahubiri (Danieli 3:19 -23). Mfalme Nebukadreza akastaajabu, akainuka haraka, akauliza kuwa je, hatukutupa watu watatu wakiwa wamefungwa? Mbona anaona watu wanne wamefunguliwa, wanatembea Katikati ya moto na hauna madhara na yule wa nne ni mfano wa mwana wa miungu. Akawaita Shadraka, Meshaki na Abednego kuwa ni watumishi wa Mungu aliye juu kuwa watoke nje. Nebukadreza akamhimidi Bwana na kuweka amri kwa kila kabila za watu, kila taifa na kila lugha kuwa yeyote atakaye nena neno lolote lisilopasa juu ya huyo Mungu wa Shadraka, Meshaki na Abednego atakatwa vipande vipande na nyumba zao kufanywa jaa kwa kuwa hakuna Mungu mwingine awezaye kuokoa namna hii. Kisha akawapandisha vyeo katika wilaya ya Babeli (Danieli 3:24-30). 2. *DANIELI 3:19-23 HASIRA YA MFALME NA MOTO MKALI DHIDI YA SHADRAKA, MESHAKI NA ABEDNEGO* Shadraka, Meshaki na Abednego walikataa kuabudu sanamu ya Mfalme Nebukadreza kwa sababu ya uaminifu wao kwa Mungu mmoja, aliye hai na ndiye pekee anapaswa kuabudiwa. Mfalme akawatisha juu ya uamuzi wao na kwamba angewachoma moto. Bado walikaza uamuzi wao na kutamka wazi kwamba moto hauna nguvu juu ya nguvu za Mungu. Mfalme kwa hasira akaamuru tanuru lichochewe mara saba kuliko kawaida. Hasira ya Nebukadreza inadhihirisha uasi wa mwanadamu dhidi ya Mungu. Hasira ya mfalme ilitokana na ushuhuda wa kishujaa uliotolewa na wale vijana watatu. Kabla hawajatoa msimamo wao mkali juu ya Imani yao katika Mungu aliye hai alikuwa akiwasemesha kama watoto wake. Hawakuona aibu kumshuhudia Mungu wao. Mfalme akatumia tanuru ambayo inasimama kama ishara ya hukumu, mateso, mauti. Kwa hakika tunaweza kuona kivuli cha msalaba katika tukio hili. Kwani hata Yesu alihukumiwa na mamlaka za dunia hii kama akina Shadraka, Meshaki na Abednego walivyohukumiwa. Baada ya moto huo mkali kuandaliwa walitafutwa vijana wenye nguvu, wakawafunga watumishi wa Mungu na kuwatupa katika tanuru la moto, wale waliowabeba Shadraka, Meshaki na Abednego moto uliwalamba wenyewe wakafa. Mle ndani wakaonekana akina Shadraka, Meshaki na Abednego wakiwa huru hawajafungwa tena. Mfalme alishangaa mno kwani halikuwa tukio la kawaida. Katika tafsiri ya toleo la Septuagint inasema, mfalme alishituka kusikia wale vijana wanne wakiimba nyimbo za sifa ndani ya tanuru. Moto ulikula Kamba zilizowafunga lakini haukugusa nguo zao wala nywele wala hata harufu tu ya moto hawakuwa nayo. Mle ndani akina Shadraka, Meshaki na Abednego hawakuwa peke yao walikuwa na mtu wa nne aliyeonekana kuwa ni mwana wa Mungu. Kumbe Yesu aliingia nao katika tanuru. Sio lazima Mungu akaepushe na majaribu au mateso wakati mwingine anakwenda na wewe, usiogope hupo peke yako. Hatuna uhakika kama akina Shadraka, Meshaki na Abednego walijua kuwa wapo Pamoja na Yesu mle ndani ya tanuru ya moto. Kwa hiyo tuwe tunaona au hatuoni Yesu yupo Pamoja nasi. Mfuasi wa Kristo pia ana tanuru za aina mbali mbali ambazo anakutana nazo katika maisha. Kuna tanuru ambazo mtu mwenyewe anajitengenezea, zipo ambazo zinatengenezwa na Shetani na nyingi zinaandaliwa na Mungu. Kwa hiyo Mungu anaweza kutuokoa kutoka katika majaribu au akatuwezesha kubeba au kushinda jaribu hilo.
3.*KATIKA YESU KILA JARIBU LINA MLANGO WA KUTOKA*
Habari za vijana wanne Danieli, Shadraka,Meshaki na Abednego zinatuonesha kuwa vijana hawa walikuwa Hodari na wenye ufanisi mkubwa tangu kuitwa kwao. Ufanisi wao haukuwa kwa sababu ya elimu tu wala nafasi zao nzuri serikalini bali ulitokana na msingi wa kiroho ambao uliongoza maisha yao yote. Ushindi wao juu ya majaribu haukupatikana katika siku moja bali ulishuhudia aina ya watu walivyo na jinsi walivyoishi na Mungu. (a) Walikuwa wameandaliwa toka nyumbani na mfalme alitafuta watu wenye sifa. (b) Walikuwa na uamuzi moyoni juu ya kumtii Mungu. Danieli na wenzake waliazimia moyoni kutojitia unajisi na vyakula vya mfalme hata kama vilionekana kuwa vyenye sifa wao wakala mtama na kunywa maji (Danieli 1:8). Kwa hiyo mafanikio yao yalianza moyoni kwa uhusiano sahihi na wauaminifu na Mungu. (c) Walidumisha maisha ya utakatifu na hofu ya Mungu Katikati ya maisha ya kipagani. Shadraka, Meshaki na Abednego waliposhurutishwa kusujudia sanamu walikataa hata walipotishwa na tanuru la moto. Walichagua kuwa waaminifu kwa Mungu na kuuacha usalama wa maisha yao mikononi mwa Mungu (Danieli 3). (d) Walikuwa watu wa maombi na kumtegemea Mungu kila siku. Maisha ya ushindi hayaanzi na mbinu bali na uhusiano. Danieli alipata ushindi kwa sababu aliishi mbele za Mungu kila siku (Danieli 6:10). Danieli hakuanza kuomba baada ya tishio bali aliomba kama ilivyokuwa desturi yake na akaendelea hata baada ya amri ya kutokuomba kutangazwa. Hatuanzi kuomba baada ya kuingia majaribuni tunahitaji kuishi maisha ya maombi. (e) Mungu alisimama upande wao. Moto haukuwaunguza (Danieli 3) na simba hawakumwangamiza Danieli (Danieli 6). Mungu hatuzuii tusipitie majaribu bali anapita nasi katika majaribu. Alienda na akina Shadraka ndani ya tanuru la moto, alienda na Danieli ndani ya tundu la simba na kuwafumba vinywa vyao. Mungu hakungoji nje bali anaenda Pamoja nawe. Majaribu ni njia ya kuuendea ushindi. Ndio maana wapo ambao hufika kwenye ushindi na wengine hurudia njiani. (f) Walitumia ujuzi na karama zao kwa utukufu wa Mungu. Hawa vijana wanne walikuwa na hekima, maarifa na nafasi za juu katika serikali kule Babeli lakini walielekeza utukufu kwa Mungu sio kwao. Katika somo letu tunajifunza kuwa Kristo yupo na watu wake katika moto. Yesu hatuokoi akiwa mbali kama mtazamaji bali anaingia katika mateso, anaingia mwenyewe katika tanuru la moto uliokolezwa mara saba. Majira haya tumeanza safari ya Kwaresma tangu jumatano ya majivu (18/02/2026), ni majira ya kutafakari mateso ya Bwana Yesu, kutubu dhambi na kujifunza juu ya tumaini la msalaba. Neno letu limetupeleka Babeli kwenye tanuru la moto ambako vijana wale watatu walikataa kusujudia sanamu, wala miungu ya Wakaldayo. Walikuwa tayari kupitia mateso hata kifo kwa ajili ya Imani yao. Kipindi hiki cha kwaresma tunamwona yule Yesu ambaye alikuwa na wale vijana ndani ya tanuru la moto, anauendea msalaba kwa ajili ya ukombozi wetu wanadamu. Kuonekana kwake ndani ya tanuru ulikuwa udhihirisho wa Yesu kabla hajazaliwa katika mwili. Uwepo wa Yesu ndani ya tanuru la moto ni ujumbe kwamba Mungu hayuko mbali na mateso ya watu wake. Haangalii toka toka mbinguni bali alifanyika mwili na kupita nasi katika mateso. Mungu anaingia ndani ya moto wa dhambi ambazo zilitutesa, hii ndio injili ya Kwaresma, ukombozi kwa njia ya msalaba. Pamoja na Yesu ndani ya tanuru akina Shadraka walikuwa huru wakitembea, hawajafungwa na wala hawakuungua. Moto upo lakini hauwezi kutuangamiza, kifo kipo lakini Yesu ni mshindi w amauti, mateso yapo lakini sio mwisho kwa sababu Yesu yumo ndani ya moto Pamoja nasi. Ujumbe wa msalaba unasema, Yesu huokoa si kwa kuondoa mateso kwanza, bali kwa kuwa Pamoja nasi ndani yake. Tukiangalia masomo yetu yote matatu tuliyopewa katika kalenda Zaburi 139:11-16; Mathayo 4:1-11 na Danieli 3:19-23 yote yanatutaka tuelekeze macho yetu kwenye siri ya ushindi wa Mungu Katikati ya giza, majaribu na moto. *Zaburi 139:11-16* Mungu alimwona Daudi na kumuandaa kabla ya vita. Hakuna giza linaloweza kumficha mtu mbele za Mungu. Mungu alimuumba mtu kwa jinsi ya ajabu tangu tumboni na kupanga siku zake zote. Kabla ya jaribu halijaja Mungu tayari anajua na ameandaa ushindi. Tumeumbwa kwa jinsi ya ajabu kiasi kwamba maarifa hayo hatuwezi kuyafikia na kuyaelewa. Kwa hiyo kwa kufuata Zaburi yetu hatuingii vitani, majaribuni peke yetu bali tunaingia tukiwa tunajulikana na Mungu. Mungu hutuandalia mlango wa kutoka kabla hatujaingia. Yeye hutangaza mwisho tangu mwanzo (Isaya 46:10). *Mathayo 4:1-11.* Yesu anajaribiwa jangwani, tena alipelekwa na Roho Mtakatifu. Alipata majaribu matatu: Jaribu la mwili, mkate; jaribu la kujionesha aruke kutoka hekaluni na jaribu la mamlaka na umiliki bila msalaba. Yesu alichukua mamlaka kwa njia ya msalaba na kumiliki vyote (Waefeso 1:18-23). Katika majaribu hayo yote Yesu alishinda kwa Neno la Mungu kila mara akisema, Imeandikwa … Kama Yesu alishinda kwa neno, na sisi hatuwezi kushinda kwa nguvu zetu bali kwa Neno ambalo pia ni Yesu mwenyewe. Katika somo la Danieli *(Danieli 3:19-23)* tumeona wale vijana wakiwa na mtu wa nne ndani ya moto. Mungu haji kabla ya jaribu, huingia ndani ya jaribu Pamoja nasi. Kumbe moto ambao ulipanga kutuangamiza unageuka kuwa mahali pa ufunuo wa uwepo wa Mungu na mahali pa Mungu kutukuzwa na kuabudiwa na watu wote.
Uwe na Kwaresma nje
Category Archives: Uncategorized
IBADA YA TAREHE 06 AGOSTI 2023 SIKU YA BWANA YA 9 BAADA YA UTATU
Somo:TUENENDE KWA HEKIMA
ZABURI 119:161–168; MATHAYO 10:5–15, MITHALI 1:1–7*
WIMBO: TMW 294
MAFAFANUZI
1. UTANGULIZI: Mithali 1:1
Kitabu kinaitwa Mithali za Sulemani, mwana wa Daudi, mfalme wa Israeli. Kitabu hiki ni mkusanyiko wa misemo ya hekima kuhusu hali halisi ya maisha ya kila siku yenye busara na haki ikigusa mada mbali mbali. Kitabu kinatoa mafundisho yenye mafumbo ambayo yalikuwa ya kawaida katika Maisha yao ya wakati ule. Ni misemo mifupi mifupi ambayo ni rahisi hata kuikariri. Kama vile Mfalme Daudi alivyo chimbuko la Zaburi katika Israeli ndivyo Mfalme Sulemani alivyo chimbuko la hekima katika Israeli. Inatajwa kuwa Sulemani aliandika Mithali 3,000 na nyimbo 1,005 wakati wa maisha yake (1 Wafalme 4:32–34). Na wakaenda Mataifa yote kwa Sulemani ili waisikie hekima yake.
Kitabu hiki kinaitwa Mithali za Mfalme Sulemani wa Israeli, lakini ni hakika kwamba Sulemani hakuziandika zote. Nyingine zinatajwa kuwa ziliandikwa na Aguri bin Yake (Mithali 30:1–33) na Mfalme Lemueli (Mithali 31:1–9), na wengine wametajwa kuwa wenye hekima bila kutajwa majina yao (Mithali 22:17 na 24:23). Mkazo ni kufundisha hekima ya jinsi ya kuishi maisha yanayompendeza Mungu. Sura nne za kwanza ni mkazo juu ya asili ya hekima na umuhimu wake na sura zinazofuata ni mkusanyiko wa mistari miwili miwili mifupi yenye mithali zenye nguvu zinazogusa mambo mbali mbali ya maisha kama ndoa, upendo, uvivu, bidii ya kazi, maonyo kuhusu ulevi na uasherati.
Mfalme Sulemani alifahamika kwa umaarufu na upekee wa hekima ya ajabu. Sulemani alipopewa nafasi na Mungu katika ndoto ya kuomba jambo lolote atakalo, aliomba hekima ya kuliongoza taifa la Israeli na Mungu alijibu ombi lake (1 Wafalme 3:3–13). Zipo habari katika kitabu cha Wafalme wa kwanza zinazoonyesha jinsi alivyotumia hekima aliyopewa na Mungu. Mfano maarufu ni wa kesi ya wanawake wawili makahaba ambao walimgombania mtoto aliye hai wakimkataa aliye kufa (1 Wafalme 3:16–28).
2. MITHALI 1:2-7 KUSUDI KUU LA KITABU
Mwanzoni kabisa mwa kitabu Sulemani anaelezea kusudi la kitabu cha Mithali. Ni kujenga maisha ya uadilifu yanayofaa kimwili na kiroho. Kumpatia msomaji hekima, busara na maarifa ya Kimungu. Yanatajwa makusudi makuu matatu:
(a) Ili kuwapa wajinga werevu (Mithali 1:4).
Kuwapa wajinga, au watu wa kawaida werevu au busara. Hao ni watu wasio wasomi, hawa ndio wenye kiu ya kupokea mafundisho. Kitabu hiki kinapaswa kuwafundisha hawa wasio na uzoefu ili kujua nini cha kufanya na wafanye namna gani katika maisha yao. Na kijana atapata utambuzi au ufahamu hata kwa mambo ambayo hakuyafahamu. Sifa moja wapo kubwa ya watu wa kawaida (simple people) au ambao wametajwa kuwa wajinga ni wepesi. Mithali 14:15 inasema: Mjinga huamini kila neno, bali mwenye busara huangalia sana aendavyo. Huyu mtu ni mwepesi au hata inaweza kusemwa kuwa ni mjinga, anaweza kuwa na maoni lakini akakosa hoja za nguvu.
(b) Kuwapa vijana maarifa na tahadhari (Mithali 1:4)
Vijana na wale watu wepesi wapo kuelekea utu uzima au kwenye hekima. Kitakachowapa tahadhari na uchaguzi sahihi katika maisha haya ni kukubali kufundishwa hekima. Hata nyakati za sasa kuna mambo mengi yanahitaji kuchambua kwa hekima na kuishi maisha ya tahadhari. Nyenzo ya kuishi maisha ya tahadhari ni hekima.
(c) Kuwaongezea elimu wenye hekima na mwenye ufahamu ayafikie mashauri yenye njia (Mithali 1:5-6) waweze kuishi maisha ya uadilifu.
Kumbe kitabu cha mithali hakipo kwa ajili ya wajinga na wale wasio na uzoefu tu bali hata kwa wale wenye hekima. Kwa kupitia mafundisho ya mithali hizi wenye hekima wataongezewa elimu zaidi na zaidi. Mwenye ufahamu atafikia mashauri yenye njia, yanayomwezesha kutatua matatizo magumu kama ilivyokuwa na mfalme Sulemani alipoletewa kesi ya wale wanawake wawili waliogombania mtoto. Kumbe hakuna mwisho katika kutafuta maarifa na hekima.
Anasema mithali zinampelekea mtu kujua hekima na adabu, kutambua maneno ya ufahamu na kufundishwa matendo ya busara katika haki na hukumu na adili. Katika kujua hekima ifahamike kwa kizazi chetu kinaitwa cha habari na upeanaji wake (information age) lakini sio wengi katika kizazi hiki wanaotafuta hekima. Kujua maneno ya ufahamu maana yake yameandikwa yanapaswa kusomwa au kuangaliwa. Mithali 3:21 anasema Mwanangu, yasiondoke haya machoni pako, shika hekima kamili na busara.
Kujua hekima: Kuna tofauti kati ya hekima (wisdom) na maarifa (knowledge). Mtu anaweza kuwa na maarifa au ufahamu lakini asiwe na hekima. Kwani maarifa (knowledge) ni mkusanyiko wa ukweli wa mambo (facts about things) lakini hekima (wisdom) ni matumizi sahihi ya vile ambavyo tunavifahamu katika maisha yetu. Maarifa au ufahamu (knowledge) yanaweza kutuelezea namna mfumo wa utawala wa fedha lakini hekima ndiyo itasimamia matumizi sahihi ya fedha, kwa mfano kusimamia makisio ni hekima zaidi kuliko utaalamu. Shida yetu leo watu wengi wamejikuta wanatafuta fedha na sio hekima. Wengi tunaweka nguvu katika kupata elimu na sio hekima. Swali linakuja, hekima inatafutwaje? Mithali 1:7 na Zaburi 111:10 zinaweka wazi kuwa kumcha Bwana ndio mwanzo wa hekima. Kumbe hekima na maarifa vyanzo vyake ni kumcha Bwana. Na ukienda kwa Ayubu 28 unaona maelezo marefu kabisa.
Kufundishwa matendo ya busara/hekima
Mithali zipo kama shule au chuo cha hekima. Lakini tuingie chuoni tukiwa na moyo pamoja na akili wazi kupokea mafunzo. Tukifanya hivi haki, hukumu na adili/usawa vitatokea katika maisha yetu.
Lakini msingi mkuu wa hekima na maarifa ni kumcha Bwana ambacho ndicho chanzo cha maarifa yote (Mithali 1:7; Zaburi 111:10). Kitabu cha mithali kimeweka mkazo wake katika mambo halisi ya maisha na sio nadharia. Lakini kinatupa ukweli kwamba msingi ni fundisho la kitheologia kuwa maarifa na hekima yanatokana na kumcha Mungu, kuwa na hofu ya Mungu. Hofu ya Mungu ni kumjua Mungu, kujitoa kwa Mungu, kujinyenyekesha kwa Mungu.
3. TUENENDE KWA HEKIMA
Wiki iliyopita tuliongozwa na kichwa kinachosema uchaguzi wa busara na leo tunazunguzia hekima. Mara nyingi tunajikuta tunatumia maneno haya mawili kwa wakati mmoja, hekima na busara. Nimeeleza kwa kirefu tofauti zake katika kitabu cha Mafafanuzi ya Mahubiri ya mwaka 2020 ukurasa wa 199 na ukurasa wa 205. Kwa haraka utaona kuwa hekima ni pana kuliko busara. Hekima inasimama kama usukani wa kuendesha busara.
Somo letu linatuhimiza kuenenda kwa hekima katika dunia ambayo imebadilika mno katika mfumo wake. Mahusiano katika ndoa yameingia changamoto kubwa mno. Migogoro katika ndoa ni mingi. Ukiangalia kwa undani utagundua kuwa kuna vitu vya msingi vinakosekana. Maarifa ya maisha ya ndoa na hekima za Kimungu zimekosekana. Na mahali fulani imeelezwa kuwa ndoa za watu walioenda shule ndio zinaongoza kuleta shida, kumbe maarifa na elimu vimeshindwa kuleta maelewano katika ndoa. Biblia imeshatuambia chanzo cha maarifa na hekima ni kumcha Bwana. Mungu asipopewa nafasi halisi katika maisha yetu hakuna usalama.
Hata wale wanaoonekana kama wacha Mungu, watu wa dini sana wamepata shida hiyo hiyo kwa sababu ya kukosekana kwa misingi ya kweli ya neno la Mungu. Akili zimeshindwa kufundishika. Neno linasema: Nitakufundisha na kukuonyesha njia utakayoiendea, nitakushauri jicho langu likikutazama (Zaburi 32:8). Mfano wa ndoa ni mmoja tu. Zipo changamoto nyingi zaidi ya hizo ambazo zinahitaji hekima za Mungu.
Kuna hitaji hekima katika malezi ya watoto na mahusiano kati ya wazazi na watoto, katika kutunza mazingira yetu, katika kutafuta na kutumia fedha.
Mambo yote haya kwa kutumia maarifa yetu hatuwezi kuyamudu, maana adui yupo kazini wakati wote. Tunahitaji uongozi wa Mungu. Na uzuri wake ni kwamba, ndani yetu huishi Roho wa Mungu. Huyu ndiye hekima yetu na mwongozo wetu kwa kila jambo. Maana yake, ili kuenenda kwetu kuwe kwa hekima, lazima tuhakikishe tupo na yeye aliye asili ya hekima. Mungu atusaidie tumpe nafasi Roho wake maana ni katika yeye tutakuwa na hekima na hivyo tutaweza kuenenda kwa hekima. Amen.
IBADA YA TAREHE 30 JULAI 2023 SIKU YA BWANA YA 8 BAADA YA UTATU
Somo:WEMA WA MUNGU WATUVUTA TUPATE KUTUBU
ZABURI 27:5-10; 2 KOR. 7:7-12;HOSEA 14:1-3*
WIMBO: TMW 149
MAFAFANUZI
1. UTANGULIZI
Ujumbe wa kitabu cha Nabii Hosea uliwasilishwa kwa njia ya kuigizwa katika Maisha ya nabii mwenyewe. Kwa mtazamo wa utumishi na ufuasi haikuwa njia rahisi ya kuwasilisha ujumbe. Nabii Hosea aliagizwa na Mungu kuoa mwanamke kahaba na kuzaa naye watoto. Mungu alisema anafanya hivyo kwa sababu nchi imefanya uzinzi mwingi. Mwanamke aliyemwoa aliitwa Gomeri (Hosea 1:2-3). Hata baada ya kuolewa na Nabii Hosea, Gomeri aliendelea kwenda kufanya uzinzi na wanaume wengine na Hosea aliendelea kumrudisha na hata kumnunua kwa fedha ( Hosea 3:2).
Katika mlango wa tatu nabii anafafanua alichoagizwa na Mungu kufanya na sababu za kufanya hivyo. Aliagizwa ampende mwanamke apendwaye na Rafiki yake naye ni mzinzi, kama vile Mungu awapendavyo wana wa Israel ingawa wamegeukia miungu mingine (Hosea 3:1).
Ndani ya ujumbe wa Hosea kuna onyo kwamba kama Israeli hataacha uzinzi (kuabudu miungu mingine) ataadhibiwa vikali. Lakini kumbuka, adhabu huwa na lengo la kumrekebisha mkosaji. Hukumu ndio shida. Labda mhukumu awe na huruma. Sura zinazofuata Hosea 4-13 zinahusu Mungu na Israeli asiye mwaminifu. Ndani yake sura za 4 na 5 zinazungumzia uzinzi ambao Israeli anaufanya kwa kuabudu miungu mingine. Sura ya 6 Efraimu alirudi kuadhibiwa. Njooni tumrudie Mungu maana yeye amerarua na yeye atatuponya (Hosea 6:1); Sura za 7-12 Israeli (Efraimu) atapona hukumu kama atamrudia Mungu anayempenda. Efraim ni kabila ambako wafalme wengi walitoka. Sura ya 13 Israeli atahukumiwa sasa na sura ya 14 inaonyesha kuwa Israeli ataokolewa baadaye.
Ukijumlisha ujumbe wa Hosea unakuwa tabia yao ya kutokuwa waaminifu ndio sababu ya hukumu itakayokuja. Hii sura ya mwisho ni ya matumaini kwa taifa lililotubu. Hosea aliitwa kuhudumu katika taifa lililochanganyikiwa na limepoteza maadili na uchaji. Alipewa wajibu mkubwa mno wa kuoa kahaba na yeye kubaki mwaminifu katika ndoa yake kama Mungu alivyo hata kama mke wake alikwenda kwa wanaume wengine.
Fikiria tu njia hii ya kuwasilisha uasi ambao umefanywa na wana wa Israeli angepewa mchungaji mmojawapo leo. Kwanza, yeye mwenyewe angesema hiyo sio sauti ya Mungu na wale wanaoogonzwa naye wengi wangetia mashaka kama kweli ni Mungu ameruhusu hilo.
2. HOSEA 14:1-3
Sura hii ya mwisho ya kitabu cha Hosea inakuja na kitu cha pekee baada ya kutupitisha kwenye ujumbe wa hukumu. Anakuja na ujumbe wa rehema. Rehema ni msaada unaoambatana na huruma. Mungu mwenyewe anatoa maelekezo namna ya kufanya toba ili kumrudia Mungu. Anaelekeza ili kufikia toba nini cha kusema na nini cha kufanya. Ujasiri wa kutubu unajengwa na utayari wa Mungu kuwapokea wenye dhambi wanaporudi. Mungu anasema nitawaponya kurudi nyuma kwao, nitawapenda kwa ukunjufu wa moyo kwa maana hasira yangu imemwacha (Hosea 14:4,8). Pia zipo faraja kubwa ambazo ameziandaa kwa ajili ya Israeli anayetubu (Hosea 14:5,7). Ujumbe unahitimishwa kwa swali kwamba ni nani aliye na hekima na atayafahamu mambo haya? Na nani mwenye busara atakaye yajua? Ni maswali yanayotuhusu sisi sote katika ukweli wa kuyapokea haya (Hosea 14:9).
Hosea 14:1 Israeli mwenye dhambi anaitwa kurudi (kutubu).
Kumbe kila mtu anahitaji ujumbe wa toba hata walio ndani ya agano kama Israeli. Kwa hiyo hata Wakristo ndani ya kanisa wanahitaji ujumbe wa toba kila siku. Israeli mrudie Mungu wako kwa maana umeanguka kwa sababu ya uovu wako. Na kurudi ni kurejesha uhusiano (fellowship) uliopotea au uliovunjika. Ulipotea au kuvunjika namna gani? Ni pale walipoanguka au kujikwaa kwa sababu ya kuabudu miungu mingine na kumwacha Mungu aliye hai ambaye anawapenda. Ndio picha ya ndoa ya Hosea na Gomeri. Wanarudi kwa njia gani? Ni kwa kutubu na kutengeneza.
Hosea 14:2 Chukueni maneno pamoja nanyi
Wanaporudi wameelekezwa maneno ya kwenda nayo ambayo ni kumwambia Bwana: Ondoa maovu yote, uyatakabali yaliyo mema. Na hivyo ndivyo mtakavyotoa sadaka za midomo yetu kana kwamba ni ng’ombe.
Wanapomrudia Bwana hawaendi kimya kimya na lazima waende kama Bwana anavyotaka na anavyoelekeza. Hataki wafikiri tu mioyoni na kujisikia hatia ya dhambi bali wakiri maneno hayo kwa midomo yao. Wamwambie Mungu kwamba tunakupenda na kwamba tumekukosea. Hata katika mahusiano yetu mfano ya mume na mke huwa ina nguvu kumwambia mwenzi kwamba unampenda, hata kwenye viapo vya ndoa wenzi huwa wanakiri kwa midomo yao kueleza upendo wao na kujitoa kwao katika ndoa. Katika viapo hivyo tunabeba maneno pamoja nasi. Mtume Paulo katika Warumi 10:8-10 anasema mtu kwa moyo huamini hata kupata haki na kwa kinywa hukiri hata kupata wokovu.
Je, tunachukua maneno gani pamoja nasi?
Hayo maneno sahihi ya kwenda nayo tunayapata kutoka kwa Mungu mwenyewe katika neno lake. Mfano Mdo 3:19 tunaambiwa tubuni basi mrejee, ili dhambi zenu zifutwe. Na Mathayo 3:2 Yohana alihubiri tubuni mwache dhambi zenu. Na Yesu alianza huduma yake kwa kuagiza toba, Mathayo 4:17 tubuni.. Upo umuhimu wa kukiri maasi yetu kwa midomo yetu. Zaburi 32:5 c; Nalisema nitayakiri maasi yangu kwa Bwana. Katika toba kuna umuhimu mkubwa wa mtu kukiri kosa alilofanya. Katika mifumo mingi ya kanisa wapo watu waliopewa wajibu wa kuwasikiliza wengine wanapotengeneza mambo yao na Mungu. Kuna wachungaji waliokula kiapo cha kufanya hivyo. Kuna watu wanafundisha kuwa inatosha kumwambia Mungu makosa yako, sawa lakini kuna mahali hali na hatia ya dhambi haiishi hadi mtu amekiri kwa midomo yake. Shida ni pale ambapo huduma imeingiliwa na watu ambao hawana dhamana ya kufanya hilo na kusimama kama mawakili wa siri za Mungu au wale wenye dhamana wanapokengeuka na kuharibu huduma. Lakini ukweli utabaki kuwa katika toba upo umuhimu wa kukiri kwa midomo yetu.
Tunamwambia nini Mungu katika toba yetu?
Ondoa maovu yote na utupokee kwa rehema zako. Hata katika sala ya Bwana Yesu alitufundisha kukiri makossa yetu mbele za Mungu ili atusamehe. Tunaporudi kwa Mungu lazima tunyenyekee mbele zake na kukubali kwamba tumekosa, tumefanya dhambi na tunahitaji msaada wake. Tunamhitaji yeye tu hatuna lolote la kufanya Zaidi ya kujiachia mikononi mwake.
Na ndivyo tutatoa sadaka ya midomo yetu kama sadaka ya ng’ombe. Maana yake maneno yetu ya toba na sifa mbele za Mungu ni sadaka ya kuteketezwa mbele za Mungu. Katika toba hiyo tutakiri wazi na kutengeneza mambo matatu:
(a) Kukataa kutegemea mataifa ya kigeni (Ashuru). Mungu pekee yake ndiye mwokozi wetu.
(b) Tutaacha kutegemea uwezo wa kivita kama kutegemea farasi (Zaburi 20:7).
(c) Tutakataa kutegemea sanamu, kazi za mikono yetu bali tutamtegemea Mungu pekee yake.
Wito wa nabii Hosea katika kifungu hiki (Hosea 14:1-3) ni kuwaita Israeli kurudi kwa Mungu kwa moyo wa dhati. Amewapa maneno ya kuomba wanaporejesha uhusiano wao na Mungu. Mwana mpotevu katika Luka 15:11-32 yeye alipanga maneno ya kusema anaporudi nyumbani kwa baba.
Kitabu cha Hosea kinahusu mambo ya dhambi na hukumu lakini pia upendo na huruma za Bwana kwa watu wasiostahili kama ambavyo Gomeri hakustahili kuwa mke wa nabii. Na Upendo huo wa Mungu umeonyeshwa kwa njia ya ndoa hiyo ya nabii Hosea na mwanamke Gomeri. Ni picha inayoumiza moyo kwa mtazamo wa kibinadamu, je, kwa Mungu mtakatifu sio zaidi?
3.WEMA WA MUNGU WATUVUTA TUPATE KUTUBU
Kutokana na mafunzo ya kitabu hiki utagundua kuwa kumbe Mungu anapomtendea mema huyu mwanadamu aliye mwovu sio kwamba anataka aendelee kutenda uovu bali anataka avutwe na upendo wa Mungu na hivyo aweze kugeuka na kujinyenyekesha kwa toba.
Mungu atujalie tutambue hilo na kutumia neema hiyo ya nguvu ya toba.
Amen.
KIPIMO CHA IMANI
Tangu nimeokoka nimebahatika kusikia mafundisho mengi sana mazuri kuhusu imani, wakati mwingine nilijifunza kuwa huhitaji imani kubwa kung’oa mlima, na nilipoijaribu imani ndogo kung’oa mlima, mlima uliishinda imani yangu ndogo. Je! Wapi hasa nilikosea mpaka kushindwa kuung’oa mlima mkubwa kwa imani ndogo? ( nadhani nilihitaji imani inayokua kama mbegu ya haladali, mpaka kuzidi ukubwa wa mlima ndipo niung’oe)
Leo ninataka kukueleza kipimo cha imani yako kwa maelezo haya.
Kama imani yako ya kufa ni kubwa kuliko ya kuishi basi jua huna imani au imani yako ni haba, hivyo kikubwa lazima kishinde kidogo.
Kama imani yako ya kutokupona ina nguvu kuliko kupona basi huna imani, au imani yako haba na chenye nguvu kitashinda.
Kama imani yako ya kukosa ni hakika kuliko ya kupata basi imani yako ni ndogo hivyo kukosa kutashinda, na kama imani yako ya laana ni zaidi ya baraka nakuhakikishia kila utakapoongea, utakachowaza, utakachoota, utakacokiona na kukikiri kitakuwa ni laana, balaa, mikosi na chenye nguvu kwenye akili yako, moyo wako na kinywa chako ndicho kitakachoshinda na kutokea kwenye maisha yako.
Nadhani umeshajipima kwenye eneo lako, sasa ni kazi yako kuhakikisha unaifanya imani yako iwe kubwa kuliko, mlima, magonjwa, madeni, na mahusiano ndipo utakapoweza kubadilisha mwonekano wa kinachokutisha kwa imani. KUMBUKA CHENYE NGUVU, UZITO, NA UHAKIKA NDICHO HUSHINDA.
Wakati wewe unaona haiwezekani kuna watu imewezekana, tofauti yako na yao ni kile unachokiona kigumu wao walikiona chepesi. Iga mwenendo wao utafanikiwa
Bwana akibariki sana.
#victoriousyear2020
contact 0768386606
SIKU YA BWANA YA 13 BAADA YA UTATU
wazo la wiki: JIRANI YANGU
Masomo:
Zaburi 28:1-4
Mathayo 12:46-50
Matendo 28:7-10*
Rangi: KiJANI
Wimbo:TMW 410
UTANGULIZI
Leo tunatafakari juu ya mada ya Jirani zetu tukilitazama neno la Mungu kutoka
Matendo 28:7-10
> Jirani kulingana na tafsiri ya Kiswahili ni mtu yeyote aliye karibu na mahali
unapoishi.
> Jirani mi mtu muhimu sana katika maisha ya kila mtu, yawezekana anaweza kuwa
rafiki yako au adui zako.(Hekima inahitajika kuishi nae)
> Biblia tangu Agano la kale inaelekeza kuwa kila mtu anapaswa kumpenda jirani
yake kama nafsi yake( Law 19:17 – 18)
> Upendo wa namna hii haukuwa rahisi hivyo watu wengi walijitahidi kukwepa
wajibu huo na mara nyingi walihoji ni watu gani wanapaswa kuwa majirani.
Hata kipindi cha Yesu watu walijitahidi kumuuliza swali hili, na Yesu aliweka wazi
kuwa jirani ni :-
a. Mtu yeyote aliye na dhiki ni jirani yetu ( Lk 10: 29 – 37)
b. Jirani ni watu wote hata kama ni adui yetu ( Mt 5: 43 – 47)
Wajibu mkubwa aliopewa mwanadamu ni kumpenda Mungu na Jirani ( Mt 22:36-40,
Rum 13:8-10,Gal5:14,Yak2:8, 1 Yoh 4:20, Mt 3:28, 14:21)
Somo ambalo tumepewa kujifunza juu ya jirani kwa mwaka huu tunajifunza juu ya
jinsi ya kumtendea jirani hasa wale ambao tunafikiria hawawezi kuwa majirani.
1. AMRI IPO TUNAPOSHINDWA KUJITAWALA JUU YA JIRANI ZETU
> Mtu akifanyiwa ovu hupenda kulipa ovu kubwa zaidi na kuanzisha mashindano
baina ya watu waliogombana au kufanyiana maovu.
> Kutokana na kushindwa huku kujitawala hisia zao, kulisababisha haki kukosekana
katikati ya watu.(Law 24: 19 -20)
> Watu walipewa sheria ili iweze kusaidia ili adhabu iweze kulingana na Kosa.
2. WANA WA MUNGU WANAWAZA MEMA JUU YA JIRANI ZAO
> Kama nilivyoeleza kuwa jirani ni mtu yeyote mwenye dhiki hata kama akiwa adui
yako na unapaswa kumpenda kama nafsi yako
> Wajibu huu mzito wa kumpenda jirani kama nafsi yako uliendelea kuwatesa watu
wengi hadi kipindi cha Yesu.
> Kazi kubwa ya kukamilisha torati aliyoifanya Yesu katika mahubiri ya mlimani pia
aligusia suala la jinsi ya kukaa na watu kwa mtazamo mpya wa wana wa Mungu.
Anawataka watu wa Mungu wasiwe na Mashindano juu ya uovu. Ukishindana
na uovu utajikuta inakuondolea uthamani wa kuwa mwana wa Mungu.
Mtu akikufanyia jambo la kukuonea wewe usinung’unike fanya kwa upendo
utakaomshangaza mtesi wako; Jitahidi kuwa mkarimu kwake (Rum 12:20)
Tusing’ang’ane kukariri neno la Mungu pasipo upendo wa kweli ndani yetu
kwa Mungu na jirani zetu
Kuweka haja za wenzetu mbele kuliko matakwa yetu
Tuwe na mizigo juu ya wengine (Mith 3:29)
3. MATENDO MEMA KWA JIRANI YANA MALIPO YAKE.
Jirani mtendee mema hata kama unaona hastahili, sababu unavyofanya hivyo sio
kwake tu bali unajitengenezea malipo yako Mbinguni na kujipa kibali cha kuwa
mwana wa Mungu ( Lk 6:35)
HITIMISHO
Mungu atuwezeshe tuweze kutambua thamani ya watu wengine zaidi kuliko makosa
wanayotutendea ili tuweze kuwatendea mema hata pale wanapotuudhi.
AMEN.
imeandaliwa na
Ev.John
MAHUBIRi Ya SIKU YA BWANA YA 12 BAADA YA UTATU
SOMO: TUTUMIE VYEMA NDIMI ZETU
masomo:
Zaburi 134
Mithali 10:11-13
Mathayo 8:1-4*
SHABAHA: WASIKILIZAJI WAELEWE YA KWAMBA KILA NENO LA ULIMI LAZIMA LITATOLEA HESABU KAMA JEMA AU BAYA SIKU YA HUKUMU
UTANGULIZI
Usemi ni uwezo mmojawapo wa mwanadamu wenye nguvu zaidi, kwa sababu kwa maneno yake anaweza kuleta manufaa makubwa, lakini pia anaweza kuleta hasara kubwa ( Mit 12:18,25; Yak 3:5,9)
Mtu awezaye kutawala ulimi wake anaweza kutawala nafsi yake yote ( Yak 3:1-4,7)
Uovu wa mtu huonekana kwa ulimi ambao haujatawaliwa ( Mk 7:21 – 23; Yak 3:6)
Maneno mengi ya mtu huonyesha upumbavu wake hivyo kila mmoja anapaswa kuutawala ulimi wake, utawala huo lazima uwe wa kweli isiwe ni kutumia maneno matamu tu ili afiche mawazo yake, yeye ni mnafiki na unafiki sio mzuri ( Zab 41: 5-6, Mit 10:18, Mt 22:15 – 18)
Ugeuzi wa maneno kwa ujanja au hila ni aina ya uongo ( Mit 12:19, 2Kor 4:2, Efe 4:25) Iwapo mtu anataka aseme ukweli kila wakati pia anatakiwa afanye hivyo kwa roho ya Upendo na maneno yake yaonyeshe tabia yake ( Mit 10:11, 20 – 21; 16:23; Efe 4:15, Yak 1:19)
Usemi wako unaonyesha hali yako ya kiroho na usemi huo utatumiwa siku ya hukumu kama ushahidi wako ( Mt 12: 36 – 37)
Hakuna neno ambalo Mungu halijui katika yale yote unayonena (Zab 139:4)
• Katika mistari hii miwili kutoka katika kitabu cha mithali inatufundisha mambo muhimu yafuatayo kuhusu matumizi ya Ulimi.
1. USEMI WA MWENYE HAKI UNA HEKIMA NA WEMA
Mtu aliye na hekima wakati wote anajua kuutunza ulimi wake, maneno yake wakati wote ni maneno yaliyokolea busara.
Maneno ya mtu wa haki yanatamani kuona mema kwa wengine na yamejaa hekima(Mith 10:20 – 21)
Mtu mwenye hekima si mwepesi wa kusema na akisema maneno yake yamejaa baraka na mema.
2. USEMI WA MTU MWOVU WAKATI WOTE UNADANGANYA NA KUUMIZA(Zab 10:7)
Mtu mwovu wakati wote huwaza mabaya kwa wengine na hupenda kutamka laana kwa watu wengine(Zab 52: 2 – 4)
Maneno yake yamejaa uongo na kujipendekeza( baadhi ya vitu asivyopenda Mungu Mith 6:17)
Mtu mwovu huwa mnafiki na kutaka kujionyesha kuwa ni mwema mbele za watu tu.
3. ULIMI MWOVU UTAADHIBIWA
Mungu atamharibu na kumuondolea mbali mwenye maneno mbaya ( Mith 10:31)
Atakuondoa katika nyumba yako( Zab 52:5)
Kifo kitampata mwenye ulimi wenye hila (Mith 17:20)
HITIMISHO
Mungu atusaidie tuweze kutumia ulimi wetu vizuri tukijua kuwa maneno yetu ipo siku tutayatolea hesabu.
AMEN.
imeandaliwa na mwinjilist John
KKKT -SD Njombe
#0768386606
JUMAPILI YA 11 BAADA YA UTATU 23/08/2020
Somo:TUWE WANYENYEKEVU
fungu;LUKA 21:28-33
Bwana Yesu asifiwe…..
Unyenyekevu ni nini? Unyenyekevu ni hali ya moyo na akili inayomfanya mtu ajikubali alivyo na awakubali wengine walivyo. Kwa njia ya unyenyekevu mtu anatambua analopaswa kutenda na analitenda na pia asilopaswa kulitenda na halitendi. Kwa njia ya unyenyekevu, mtu anawapa wengine nafasi ya kuwa wanavyotakiwa kuwa katika haki. Kwa njia ya unyenyekevu, tunakomesha vilema vyetu vyote vya majivuno, kiburi, maringo, kujionaona na kujikweza.
Fadhila ya unyenyekevu inachukuliwa kuwa ya msingi na kiongozi wa fadhila nyingine zote. Martin luther anaendelea kusema kuwa “Kimsingi ni katika unyenyekevu mtu anafanywa kuwa mfuasi wa Kristo, na kwa hilo roho inaandaliwa kuungana na Mungu.” Mambo yote ni lazima yapate msingi wake katika unyenyekevu. Unyenyekevu unachukua nafasi ya kwanza kwa vile, unafukuza majivuno.
Fadhila ya unyenyekevu inatudai kujishusha ili tuinuliwe. Inatufanya tujione si kitu ili tuonekane kuwa ni kitu. Inatufanya tuwajali zaidi watu kuliko kujijali na kujipendelea sisi wenyewe. Inatufanya tuoneshe upendo wetu zaidi kuliko kutaka kupendwa. Inatufanya tuwaheshimu zaidi wenzetu kuliko kutaka kuheshimiwa.
Kwa njia ya unyenyekevu, tunaweza kufundishwa, kuelekezwa, kuongozwa, kuonywa, kulindwa, kutetewa na kukuzwa kwa ujumla. Ni fadhila ya msingi sana katika maisha ya mahusiano ya kila siku katika familia na katika jumuiya yoyote ile ya watu. Hata marafiki wa kawaida tu, au wachumba wakikosa unyenyekevu basi mahusiano yao daima hayatakosa malumbano, matusi, dharau, ukandamizaji na kila aina ya mateso.
Pengine watu wengi hushindwa kuishi na sisi kwa sababu tunakosa unyenyekevu, na ndio maana, hatuonyeki, haturekebishiki hatupendeki, hatuelekezeki, hatufundishiki, daima tunajiona kuwa ndio wenye haki sana mbele za watu na mbele za Mungu. Kukosa unyenyekevu kunatutenga na fadhila za Mungu. Tazama yule mfarisayo aliyekosa unyenyekevu akajiona kuwa yeye ndiye mwenye haki sana. [Lk 18:9-14]
Familia isiyojua unyenyekevu, ni uwanja wa vita daima. Vita za maneno na za mikono hazitakwisha. Tangu mwanzo wa malezi watoto wafundishwe juu ya umuhimu wa unyenyekevu. Unyenyekevu ni tendo la kijasiri kwa sababu linakudai kujishusha, kukomesha maringo, kiburi, kujikweza na majivuno. Walio wanyenyekevu daima hupata kibali machoni pa Mungu. Neno linasema “…Mungu huwapinga wajikwezao, bali huwapa neema wanyenyekevu” (Yak 4:6).
Wazazi katika familia, wakinyenyekeana wao kwa wao hapo wanakuza zaidi upendo wao. Kiburi, maringo, dharau na majivuno, hufukuza upendo. Lakini unyenyekevu hukuza na kudumisha upendo. Inapotokea kwa sababu zozote wazazi wanaoneshana umwamba, hakuna anayetaka kujishusha hata pale linapotokea kosa au kwazo la wazi, hapo upendo na furaha ya maisha ya ndoa huingia katika dosari kubwa.
Ndoa nyingi zimeingia katika migogoro ya kudumu sio kwa sababu ya matatizo makubwa, hasha! Pengine ni makosa madogomadogo ya kawaida kabisa ya kibinadamu. Lakini kwa vile hakuna ile hali ya unyenyekevu, kuwa tayari kujishusha, kila mtu anataka kujionesha yeye ni zaidi, na yupo sahihi zaidi ya mwenzake; hapo ndipo mgogoro hukuzwa zaidi.
Hapa rai ya moja kwa moja tunaipeleka kwa wanandoa! Wanandoa tukitaka amani, utulivu na maelewano ndani ya ndoa zetu, tuwe wanyenyekevu. Tukomeshe vilema vya kiburi, dharau, kujiona na maringo. Unyenyekevu ni daraja ya kufikiana na kuafikiana. Ukiwa mnyenyekevu, hata pale unapopatwa na tatizo, mwenzi wako ni rahisi kukuelewa, kukupokea na kukuinua. Lakini ukikosa unyenyekevu, utamfanya mwenzio ashangilie ukipatwa na mabaya.
Unyenyekevu, ni kiti cha kutuweka katika mazungumzo yenye mwafaka daima. Bila unyenyekevu, kila neno utakalotamka litakuwa na virusi vya fujo. Wazazi tukiwa wanyenyekevu, watoto wetu wataiga mwenendo wetu wa unyenyekevu nao pia tutawafundisha unyenyekevu. Sisi wazazi ndio waalimu wa maadili katika Kanisa la nyumbani, basi, na tujitahidi kuwa wanyenyekevu.
Na mtume Paulo anaelekeza kuuambata unyenyekevu, kwani ndiyo njia ya kujenga usitawi. Anasema “msifanye chochote kwa moyo wa fitina au majivuno ya bure; muwe na unyenyekevu ninyi kwa ninyi, na kila mmoja amwone mwenzake kuwa bora kuliko yeye mwenyewe. Pasiwe na mtu anayetafuta faida yake mwenyewe tu, bali faida ya mwenzake” (Fil. 2:3-4).
MWISHO
Bwana, anatualika sisi sote tuwe wanyenyekevu akisema ”jifunzeni kutoka kwangu kwa kuwa mimi ni mpole na mnyenyekevu wa moyo, nanyi mtapata raha nafsini mwenu”. (Mt. 11:29). Na pengine anatuasa akisema “Anayejikweza atashushwa, na yeyote anayejushusha atakwezwa (Mt 23:12). Unyenyekevu ni ngazi ya kupanda juu, zaidi na zaidi.
“Mtiini Mungu mpingeni shetani naye ata wakimbia”
AMEN.
imeandaliwa na
mwinjilist John
#0768386606
MAHUBIRI YA SIKU YA 10 BAADA YA UTATU
SOMO: LUKA 19: 41 – 44
UTANGULIZI
• Mungu ametupa kibali kukumbushana kuwa HAKI HUINUA TAIFA BALI DHAMBI NI AIBU KW WATU WOWOTE, msemo huu ni hakika hebu tuangalie mistari hii “kwa hiyo, kama kwa mtu mmoja, dhambi iliiingia ulimwenguni, na kwa dhambi hiyo mauti; na hivyo mauti ikawafikia watu wote kwa sababu wote wamefanya dhambi” (Warumi 5:12)
• Dhambi ya mtu mmoja ilitufanya watu wote tuwe wadhambi ndio maana jamani hiii kitu dhambi ni aibu kwa watu wowote wanaojihususha nayo. Zaidi hebu tuone na hii “Basi tena, kama kwa kosa moja, watu wote walihukumiwa adhabu, kadhalika kwa tendo moja la haki watu wote walihesabiwa haki yenye uzima kwa sababu kama kwa kuasi kwake mtm mmoja watu wengi waliingizwa katika hali ya wenye dhambi kadhalika kwa kutii kwake mmoja watu wengi wameingizwa katika hali ya haki”(Rumi 5: 18 – 19)
• Wewe ukitenda haki taifa zima linapata kuinuliwa kwa haki uliyoitenda. Kila mmoja ajitahidi kuhakikisha taifa lake linainuliwa.
• Kwa mwaka huu kanisa letu linatukumbusha kwa kupitia injili iliyoandikwa na Luka kuwa ili uweze kuliinua taifa lako unapaswa KUZITAMBUA SIKU
• Kisa hiki ni cha Yesu akiingia Yerusalemu kwa shangwe yeye aliulilia mji wa Yerusalemu kwa kutokufahamu siku na muda wake wa kujiliwa. Katika kisa hiki tunajifunza
1. MUNGU ANAHUZUNIKA KWA WEWE KUTOKUZINGATIA MUDA WAKO
• Yesu anapoukaribia Mji anaulilia na kusikitika kwa wao kutokutambua kuwa kwa kuja kwake walipaswa kwenda kumpokea kwa furaha kwa sababu kwa kuja kwake ilikuwa ndio ukobozi wa Israel.
• Siku ya kujiliwa ni siku ya kufurahi, kuabudu, kusifu na ni siku ya amani kwa watu wote.
• Kwa nini watu hawaoni wala kutambua umuhimu wa siku ya Mungu.
a. Kwa sababu wanaongozwa na viongozi vipofu ambao hawaoni yatakayotokea mbeleni.
b. Wengine hawaoni sababu ya nafasi walizonazo, kama vile cheo, mal ink
c. Wengine wamekosa kuiona siku ya Mungu kwa sababu ya kujiinua na kujiona wao wanathamani kuliko kumuabudu Mungu
• Hata sasa wapo watu hawatambui nguvu za Mungu wala hawaoni umuhimu wa kuhudhuria ibada, jumuiya na matukio ya kiibada kwa mojawapo ya sababu nilizozitaja hapo juu, viongozi wengine wamewafanya watu kuwaona wao na kuwaabudu wao kuliko Mungu.
2. IPO HASARA KUBWA KWA WALE WALIO MBALI NA MUNGU
• Kwa wa Israel kutokutambua nyakati kwa sababu mbalimbali Yesu anaona mabaya juu ya mji wao wa Yerusalemu kuwa
a. Hekalu litabomolewa
b. Mji wa Yerusalem kuharibiwa na uzuri wake kupoea
c. Maadui zake watatawala juu ya Yerusalemu
• Hayo yote yanatokea kwa sababu tu wameshindwa kutambua wakati wa kujiliwa kwao. Kutambua na kuheshimu uwepo wa Mungu utakuepusha na matatizo mengi.
• Tujitahidi kwa wingi kuhakikisha kuwa Mungu anakuwa pamoja nasi wakati wote. Tukiutambua wakati amani itatulia juu ya maisha yetu na juu ya familia na taifa letu kwa ujuma.
HITIMISHO
• Yesu akiwa ndani yetu, akawa kiongozi wetu kwa neema yake atatuwezesha kutenda haki kwa ajili yetu na kwa ajili ya taifa letu.
• Kutenda dhambi sio tu kunamchukiza Mungu na kutupati mauti bali pia inasababisha taifa kuwa katika mabaya na machukizo mbele ya Mungu.
• Tujitahidi wote kutenda haki kwa neema ya Mungu ili baraka zake zidumu nasi milele na aweze kututahadharisha juu ya kesho yetu.
AMEN
Ev.john
SIKU YA BWANA YA 9 BAADA YA UTATU
IBADA YA TAREHE 09 AGOSTI 2020
TUENENDE KWA HEKIMA
ZABURI 119:25-32; LUKA 12:44-48
MAHUBIRI: KOLOSAI 4:2-6
1. UTANGULIZI
Katika mafafanuzi/mahubiri ya juma lililopita tuliangalia uhusiano uliopo kati ya hekima na busara. Tukawa tumesema kwamba hekima ni pana kuliko busara na ipo kama usukani wa kuiendesha busara. Busara ni namna ya kuamua jambo kwa akili kufuata mazingira. Na pia tukasema busara ni hekima inavyoonekana katika matendo. Na mkazo wetu ulikuwa katika uchaguzi wa busara. Mimi katika mahubiri nilikaza nguvu ya uchaguzi (the power of choice) na nikasema hivi tulivyo ni matokeo ya uchaguzi, nikamnukuu Dkt. John C. Maxwell aliyeandika “life is full of choices and every choice you make, makes you” (maisha yamejaa uchaguzi na kila uchaguzi unaoufanya unakutengeneza wewe). Mwisho niliorodhesha kanuni 4 za kutuongoza tunapofanya uchaguzi ili hekima ijidhihirishe katika maisha yetu.
(a) Zingatia vipaumbele na utabiri matokeo ya uchaguzi wako. Vipaumbele vinaongozwa na tunu ulizo nazo, maono na dhamira (values, vision and mission). Maana, changamoto mara nyingi sio kuchagua kati ya baya na jema bali kati ya zuri na zuri zaidi.
(b) Usikubali hisia zikuongoze. Epuka kufanya uchaguzi ukiwa na furaha sana ama huzuni/hasira
(c) Fikiria njia mbadala nyingi kabla ya kufanya uchaguzi na maamuzi.
(d) Jifunze kusikiliza dhamiri (Roho Mtakatifu). Je, unasikia amani moyoni na lile unalochagua? Amani ya Kristo iamue mioyoni mwenu (Kolosai 3:15).
Leo tunaambiwa tuenende kwa hekima mbele za wasioamini. Na somo letu Kolosai 4:2-6 ligusa suala la uinjilisti tunaweza kufanya kwa njia ya wengine kwa kuwaombea (4:2-4) au tunaweza kufanya wenyewe moja kwa moja kwa kuuendea ulimwengu (4:5-6). Mungu anatutaka tuwe makini na maisha ya sala binafsi na pia namna ya kuhusiana na watu wa dunia hii, namna ya kuishi katika ulimwengu kwa hekima.
2. DUMUNI KATIKA KUOMBA
Yesu aliwahi kufundisha pia juu ya kuomba bila kukoma katika Luka 11:5-10. Mtu aliyefikiwa na rafiki usiku wa manane akiomba asaidiwe mikate kwa ajili ya mgeni, Yesu anasema ataamka kwa vile hataki kuendelea kusumbuliwa. Na pia katika Luka 18:1-8 Yesu alitoa mfano wa kadhi aliyemsaidia mwanamke mjane kwa kuona anamsumbua kila siku kuomba amsaidie.
Paulo akawahimiza Wakolosai kuendelea kuomba kwa bidii kama yeye alivyowaombea pia (Kolosai 1:3-8). Na anaposema dumuni katika kuomba tafsiri nyingine zinatupeleka kwenye maana ya kuwa uwe na nguvu (be strong). Uwe na juhudi kubwa. Huwezi kuendelea katika maombi kama huna pumzi na juhudi katika maombi. Ni kupambana, ni vita ya kuangusha ngome za Shetani.
Maombi sio tukio la mara moja katika maisha ya mkristo. Maombi ni jambo la kila siku mbele za Mungu (1 Thesalonike 5:17).
3. MKESHE KATIKA KUOMBA NA KUSHUKURU
Paulo anawahimiza Wakolosai kuwa macho, kukesha. Hii ni lugha ya kiulinzi au kiaskari. Walinzi hodari husimama usiku mzima ili kuhakikisha lindo lao lipo salama. Kwa hiyo wanapaswa kuwa macho wakati wa maombi wasilale usingizi. Mara nyingi mwana maombi anakumbana na uchovu wa mwili na hivyo kumfanya alale usingizi wakati wa kuomba.
Yesu aliwahimiza wanafunzi wake kukesha katika maombi katika matukio mawili muhimu. Pale alipokuwa nao mlimani katika tukio la kugeuka sura (Luka 9:28-33), Petro, Yakobo na Yohana walilemewa na usingizi na kushindwa kuomba. Mahali pengine ni katika Bustani ya Gethsemani (Mathayo 26:36 -46). Walilala na akawauliza, je, hamkuweza kukesha nami hata saa moja? (26:40).
Ipo vita wakati wa maombi. Unaweza kufikiri ni vita kati ya maombi na usingizi, lakini kama unaona rohoni, kuna nguvu nyuma yake. Hakuna wajibu unaweza kufanyika kwa ufanisi bila maombi. Lakini kila uombapo kuna upinzani! Pamoja na kuomba walipaswa kumshukuru Mungu.
Maombi siyo ”Mungu nipe hiki na kile na kile! Tunasogea mbele zake kwa shangwe na shukrani kwa Mungu. Katika shukrani tunamshukuru Mungu kwa namna alivyo na atendavyo. Ukuu wake, uaminifu wake, upendo wake, neema yake, hekima yake, na mengine mengi! Bila Mungu kututendea kwa namna atendavyo, hatuwezi kudumu hata siku moja.
Katika maombi, tunaomba ufalme wake uje. Ufalme wa Mungu ukija, tunapata mahitaji yetu na kwa namna Mungu aonavyo inafaa. Tunapoomba tunashukuru sio kwa sababu tumepata tayari, bali kwa sababu tunaamini kuwa tunapata, maana Mungu ni mwaminifu. Shukrani inatuhakikishia kuwa tunamwendea Mungu tunayemwamini kuwa anajibu.
4. MTUOMBEE MUNGU ATUFUNGULIE MLANGO WA NENO TUNENE SIRI YA KRISTO
Wakolosai wanahimizwa kuomba kwa ajili ya viongozi wao wa kiroho. Viongozi wa kiroho wasipopata neema au kibali machoni pa Mungu watakwamisha shughuli za kiroho. Paulo hakuwahimiza kuomba kwa ajili ya mahitaji yake binafsi bali Mungu afungue mlango kwa neno la Mungu, yaani fursa ya kuhubiri injili, tena ili anene siri ya injili impasavyo sio kama atakavyo yeye. Hapa kuna siri kubwa! Sio kila anayesimama mimbarani na kuhubiri anahubiri Neno la Mungu. Kwa hiyo Paulo anaomba Wakolosai wamwombee ili ahubiri Neno la Mungu. Paulo anasema kuwa alikuwa kifungoni kwa sababu ya uaminifu wa kuhubiri injili ya Kristo na alikuwa tayari kupokea matokeo ya uaminifu huo hata kupata vifungo zaidi. Ukihubiri Neno la Mungu katika kweli yake, wakuu wa giza kupitia watumishi wao watatikisika na kupanga njama za kukuangamiza! Ukiweza soma habari za Danieli. Au jifunze vizuri upinzani uliokuwepo katika huduma ya Bwana Yesu. Lakini wajapojipanga kwa upinzani wa aina yoyote ile, kuna nguvu ya Mungu itujiayo katika maombi! Katika maombi tunajadiliana na kusemezana na Mungu. Mungu huja kututia nguvu na kufanyika ngao yetu.
5. ENENDENI KWA HEKIMA MBELE YA WASIO AMINI/ULIMWENGU
Paulo anawakumbusha Wakosolai kuwa maisha ya kiroho sio tu kujifungia ndani kwa maombi bali wanahitaji kuishi hekima yao kwa vitendo, kuwa na busara kama tulivyojadili somo lililopita. Hii itawaongoza namna ya kuongea na kuishi. Kwa wakati ule, tayari kulikuwa na picha mbaya kuhusu ukristo. Lakini kwa njia ya hekima na mwenendo wao walitakiwa kuiondoa ile picha mbaya na kuuonesha ulimwengu uzuri ulio katika Bwana unaodhihirika katika maisha ya Wakristo. Mienendo yetu ni mahubiri yanayoishi. Tunapaswa kumdhihirisha Yesu Kristo katika maisha yetu pia, sio maneno tu!
6. MUUKOMBOE WAKATI
Neno kuukomboa wakati linabeba maana zifuatazo: kutumia wakati kwa njia nzuri kabisa (making the best use of time) kutumia kwa makini kila fursa inayojitokeza (making the most of every opportunity), au kutumia kwa ufanisi kila wakati unalionao (make effective use of our time). Mtume Paulo kwa Waefeso 5:15-20 anasema enendeni kwa hekima mkiukomboa wakati kwa maana zamani hizi ni za uovu na wasiwe wajinga. Kila nafasi katika maisha ni muhimu lazima itumike kwa ukamilifu wote na kwa manufaa. Ndio maana imesemwa kuwa wakati ni mali. Kiroho ni kama alikuwa anawaambia kuwa wakati ni mfupi tusikubali mtu afe bila kumjua Yesu. Lakini hata wakati huu wenye mabadiliko makubwa ya kiuchumi, muda ni moja kati ya rasilimali muhimu sana katika kuleta maendeleo. Wanaojua wanatumia vizuri. Kwa bahati mbaya wapo watu ambao hawajaelewa thamani ya muda hawatunzi muda mahali wanapo hitajika.
Kuna mtu alisema hivi: nilipokuwa mtoto sikuwa na cha kufanya zaidi ya kutambaa na kusubiri nisaidiwe hiki na kile, wakati huo muda ulikuwa unatambaa. Nilipokuwa kijana nilianza kuona hili na lile, nikawa ninaongea pia, lakini muda ulianza kutembea. Nilipokuwa mtu mzima tayari ninajua maana ya maisha, nilianza kushughulika na mambo muhimu, muda ulikuwa unakimbia kweli. Nimekuwa mzee, ninataka nirekebishe nilipokesea, muda umepaa! Haupo tena! Mhubiri anasema vizuri: ”Mkumbuke Muumba wako siku za ujana wako kabla hazijaja siku utakaposema…” (Mhubiri 12:1). Usipotumia wakati vizuri, utakuja kujuta!
Bwana Yesu alionesha kuwa wana wa ulimwengu, yaani walio wa ufalme wa giza wanajua kuutumia wakati (Luka 16:8). Lakini wana wa nuru ni wazito kweli! Kwa nini wana wa ulimwengu wanajua kuukomboa wakati? Mkuu wao anajua kuwa anao muda mfupi sana! Kwa hiyo amejipanga vya kutosha na watumishi wake wanamtii! Watu wa Mungu, tusipoukomboa wakati, tutapoteza dira. Mambo mengi yataharibika na hivyo tutamletea hasara Bwana wetu pasipo sababu! Lazima tuenende kwa hekima na kuuomboa wakati!
7. MANENO YENU YAJAE NEEMA NA MUNYU NA MPATE KUJUA JINSI YA KUJIBU
Njia nyingine ya kumtangaza Kristo ilikuwa ni kwa njia ya usemi wao. Anasema maneno yao yawe na neema na munyu. Yawe na chumvi ambayo kazi yake ni kutunza kitu kisiharibike na kutia ladha nzuri. Na busara (hekima iliyo katika matendo) ingewawezesha hata kujua jinsi ya kumjibu kila mtu. Walipaswa kujibu kufuata mafundisho ya biblia sio kwa jinsi wanavyojifahamu. Na kwa vile walidhaniwa kuwa wajinga wasio na akili, basi kwa njia ya usemi wao wangedhihirisha kuwa sio watu wa kawaida. Walitakiwa kutafuta neema ya kuwa wazungumzaji wazuri.
8. JUMLISHO
Kuenenda kwa hekima katika ulimwengu ulioanguka sio rahisi. Yesu alipokuwa anawatuma wanafunzi kwenda kuhubiri aliwaambia, ninawatuma kama kondoo katikati ya mbwa mwitu. Kuweni na hekima kama nyoka lakini wanyenyekevu kama njiwa. Kondoo wakati wote yupo na mchungaji wake. Bwana Yesu anatutaka tujue kuwa peke yetu hatuwezi. Ndio maana hapa Paulo anakaza kuomba na kuombeana. Mbwa mwitu wapo kila mahali, tena hata mahali tunapodhani tupo salama. Bila Mungu kutufumbua macho, hatutastahimili. Tunamhitaji Bwana wakati wote. Ndio maana tunaambiwa tuenende kwa hekima. Hekima ya kweli hutoka kwa Bwana. Tukiwa na Bwana, tunahakikishwa hekima. Atatuwezesha kunena na kutenda kama itupasavyo. Lililo kuu katika kuenenda kwetu, tuukoboe wakati. Maana tupo kwa kitambo. Muda hautusubiri. Basi Mungu aliyetuita atuwezeshe kuenenda kwa hekima nyakati zote. Amen
Na mchg. Dkt. George Mark Fihavango
Askofu
From Mwinjilist Joseph Mshana
MAHUBIRI YA SIKU YA BWANA YA 8 BAADA YA UTATU
Somo:UCHAGUZI WA BUSARA
Masomo:
Zaburi 37:1-8
Marko 1:40-45
Mathayo8:11-13
UTANGULIZI
✏ Siku ya leo tunajifunza juu ya uchaguzi wa busara natumepewa injili mbili Marko 1:40-45; Mathayo 8:11-13. Uchaguzi ni kitendo chaku angalia ama kuoanisha kipi kinafaa ama kipihakifai.
✏Busara ni hekima au maamuzi sahihi
✏Sasa UCHAGUZI WA BUSARA maana yake ni kitendo cha kuangalia kipi kinafaa tena kwahekima.Maana unaweza ukachagua nakuona kinafaa lakini ukakosa hekima kwenye uchaguzi wako bado utakiacha kinacho faa zaidi kuliko hicho ulicho kichagua.Katika injili mbili za leo pamoja na zaburi tunajifunza mambo yafuatayo kutokana na kichwa hichi cha UCHAGUZI WA BUSARA;
1.HEKIMA KATIKA UCHAGUZI NI MWANZO WA MAFANIKIO
✏ Unaposoma injili ya Marko1:40-45 tunamwona mtu mwenye ukoma alimwendea Yesu akisema “Ukitaka, waweza kunitakasa” kwakauli hiyo alitumia hekima ya hali ya juu kumwomba Yesu amtakase kwamba kama Yesu mapenzi yake nikumuona mzima bas amtakase kama simapenzi yake amuache
✏Sisi kanisa la leo kuna mambo yanahitaji uchaguzi wenye hekima ndani yake ilituweze kufanikiwa kwa mfano unapomchagua kristo kuwa Bwana na mwokozi wa maisha yako tambua huyo Bwana hataki mtu mzembe FANYA KAZI KWA BIDII
✏Lakini pia familia yenye mafanikio huatanguliwa na hekima ndani yao baba akiwa naheshima kwa mama na watoto watafanya hivo kwasababu baba amechagua fungu jema nala baraka
2.MATAIFA WATATUTANGULIA KUINGIA MBINGUNI KABLA YETA SISI TULIO OKOKA.
✏Biblia inasema katika Mathayo 8:12″bali wana wa ufalme watatupwa katika giza la nje, ndiko kutakuwako kilio na kusaga meno”
✏Yesu ananza kwakusema watakuja watu kutoka mashariki na magharibi kaskazini na kusini watakuja kuketi kwa ibarahim,isaka,na Yakobo maana yake walioamini nawasio amini wote wataenda mbio kila moja njia yake lakini wale waliowagiza(wana waufalme mathayo8:13) ndio anasema watatupwa nje katika ufalme wagiza sasa kwanini tulioamini tutatupwa nje ni kwasababu ndani yetu wengi tumemchagua kristo lakini tunashwindwa kwend sawasawa na kanuni zake wengi tumekuwa wasengenyaji na mambo mengi laini mataifa wengine hawasali lakini wanajikita katika kutenda mema nandio maana tusipo kaasawa watatuzidi hata sisi
✏Ndugu zangu nawasihi tufanye kazi ya Mungu kungalibado mchana tuachague natufanye maamuzi saa hii wasitushinde wasio amini sisi tunanguvu zaidi yao.
3.NJIA ZETU NA MIPANGO YETU TUNAPASWA KUMKABIDHI BWANA
✏Mwimba zaburi anatuambia katika zaburi 37; 5 “Umkabidhi Bwana njia yako, Pia umtumaini, naye atafanya”
✏Kumbe sisi tunaomwamini kristo tunatakiwa kumchagua Kristo kuwa kiongozi wa mipango yetu nanirahisi tu nikukabidhi na kutumaini( kutarajiA au kuwa naimani) naye nilizima afanye tu sasa sasa kwanini watu wengi tunamkabidhi lakini hafanyi kwasababu;
✏Tumekuwa tunaishi maisha ya changanya changanya hatujachagua ninani wakusimamia mipango hiyo ingawaje wengine wanaileta kanisani lakini wakitoka wanaenda kwa waganga nandiomaana haifanikiwi kumbe sisi tulio amini tunapaswa kukabidhi na kuamini au kutumaini tu mwisho tusiongeze mengine yasiyo na mantiki
✏Tuanaambiwa kitarajiwacho kikikaiwa moyo huugua ni kwamba Unapo mkabidhi Bwana mipango yako tambua kuwa anafanya kwa mapenzi yake hapelekeshwi na yeyote hivyo jenga moyo wa UVUMILIVU
4.RIDHIKA NA HALI ULIYO NAYO
✏Ukisoma Zaburi 37:6 ” Ataitokeza haki yako kama nuru, Na hukumu yako kama adhuhuri”
✏Unajua mda wingine Mungu huwa anakuweka kwenye zone(sehemu) furani ili ujifunze sasa watu wengi tunapokuwa kwenye eneo hili huwa tunachagua hukumu mfano anapitishwa kwenye gumu fulani imani inashuka kanisani haendi anaacha kabisa kumbe swala ni kumuamini tu yeye ataitokeaza haki yako kama nuru
✏Mungu anatabia ya kujitukuza katika ya pito unalopitia hivyo mpendwa unapopitishwa kwenye gumu ama pito fanya uchaguzi wa busara usikurupuke maana anasema”Ataitokeza haki yako kama nuru,……”
MWISHO
✏Wito wangu kwenu naombeni mfanye maamuzi sahihi siku ya leo kama neno la Mungu linavyosema katika Joshua 24:15 “inasema chagueni hivemaeo mtakaye mtukatika”
AMEN.